Mama Nehemiah
JF-Expert Member
- Sep 9, 2018
- 275
- 475
Leo 14/07/2025 wanafunzi wa darasa la tatu wanaosoma shule ya msingi Goba Mpakani iliyoko Dar es Salaam ambao jumamosi ya 12/07/2025 hawakwenda tuisheni wamechapwa fimbo na walimu wao. Mwalimu mkuu wa S/msingi Goba Mpakani tunaomba uliangalie suala hili kwa umakini.
Kwanini wanafunzi wanawaambia watoto wa darasa la tatu kwamba wasipoenda Jumamosi na shilingi 500 kwa ajili ya kusoma tuisheni watachapwa?
Suala la mwanafunzi wa darasa la tatu kwenda tuisheni Jumamosi liwe ni hiari na sio lazima. Mwalimu mkuu na walimu wenzako mjiulize.
1) Vipi kwa mzazi ambaye hana uwezo wa kumpa hiyo sh 500 mtoto wake kwa ajili ya tuisheni?
2) Kwanini mwanafunzi tena malaika wa darasa la tatu achapwe fimbo kisa tu ameshindwa kwenda tuisheni J,mosi na sh 500?
3) Wanafunzi watapata muda wa kupumzika saa ngapi(siku ipi?)ili hali kuanzia jumatatu hadi ijumaa wanaondoka asubuhi sana na kurudi jioni kabisa wakiwa hoi(ba siku hizi za masomo wanakuwa wameunganisha na tuisheni j,tatu -ijumaa).
N:B Muelewa wazazi hatupingi swala la tuisheni kwa wanafunzi tatizo linakuja suala hili linapokuwa ni LAZIMA na mtoto asipokuja anachapwa hasa ikizingatiwa ni siku ya jumamosi ya watoto wadogo hawa kupata muda wa kupumzika.
Kwanini wanafunzi wanawaambia watoto wa darasa la tatu kwamba wasipoenda Jumamosi na shilingi 500 kwa ajili ya kusoma tuisheni watachapwa?
Suala la mwanafunzi wa darasa la tatu kwenda tuisheni Jumamosi liwe ni hiari na sio lazima. Mwalimu mkuu na walimu wenzako mjiulize.
1) Vipi kwa mzazi ambaye hana uwezo wa kumpa hiyo sh 500 mtoto wake kwa ajili ya tuisheni?
2) Kwanini mwanafunzi tena malaika wa darasa la tatu achapwe fimbo kisa tu ameshindwa kwenda tuisheni J,mosi na sh 500?
3) Wanafunzi watapata muda wa kupumzika saa ngapi(siku ipi?)ili hali kuanzia jumatatu hadi ijumaa wanaondoka asubuhi sana na kurudi jioni kabisa wakiwa hoi(ba siku hizi za masomo wanakuwa wameunganisha na tuisheni j,tatu -ijumaa).
N:B Muelewa wazazi hatupingi swala la tuisheni kwa wanafunzi tatizo linakuja suala hili linapokuwa ni LAZIMA na mtoto asipokuja anachapwa hasa ikizingatiwa ni siku ya jumamosi ya watoto wadogo hawa kupata muda wa kupumzika.