Walimu msikubali kuingia kwenye mtego huu wa wanasiasa

Molembe

JF-Expert Member
Dec 25, 2012
9,821
11,527
Hivi karibuni waziri wa elimu ameibuka na hoja ya kuwataka walimu wafanye mtihani ili waweze kuajiriwa, nawabieni ndugu zangu walimu mnaosubiri ajira huu ni mtego mkiingia katika huu mtego mtadhalilishwa na kutukanwa sana, jiulize swali dogo tu imekuwaje wizara imeshindwa kuvuamini vyombo vyake kama NECTA na TCU iamue kutunga mitihani yenyewe, mtego.

Ukweli ni kwamba serikali inataka kukwepa jukumu lake la kuajiri, inataka kupunguza walimu waliojaa mtaani ilihali shule hazina walimu, mkifanya hii mitihani idadi kubwa itafelishwa halafu wanasiasa wataibuka na kusema walimu hawana uwezo ni vilaza na jamii itawaamini na kuwaona nyie ni mbumbumbu kweli.

Kama serikali inataka kuajiri walimu walio bora ni bora ingesema walimu wafanyiwe usaili kama zinavyofanya shule za private kuliko hiyo mitihani yao ya sasa, huwezi kupima ubora wa mtu aliyekaa mtaani miaka nane(8) kwa mtihani tu.

Kama serikali inataka walimu bora basi ikubali kuingia gharama iwarudishe vyuoni hata kwa mwaka mmoja hawa walimu waliopo mtaani iwajengee uwezo upya, na sio kuleta mitihani ya siku moja ili kupima uwezo wa walimu.
 
Hivi karibuni waziri wa elimu ameibuka na hoja ya kuwataka walimu wafanye mtihani ili waweze kuajiriwa, nawabieni ndugu zangu walimu mnaosubiri ajira huu ni mtego mkiingia katika huu mtego mtadhalilishwa na kutukanwa sana, jiulize swali dogo tu imekuwaje wizara imeshindwa kuvuamini vyombo vyake kama NECTA na TCU iamue kutunga mitihani yenyewe, mtego.

Ukweli ni kwamba serikali inataka kukwepa jukumu lake la kuajiri, inataka kupunguza walimu waliojaa mtaani ilihali shule hazina walimu, mkifanya hii mitihani idadi kubwa itafelishwa halafu wanasiasa wataibuka na kusema walimu hawana uwezo ni vilaza na jamii itawaamini na kuwaona nyie ni mbumbumbu kweli.

Kama serikali inataka kuajiri walimu walio bora ni bora ingesema walimu wafanyiwe usaili kama zinavyofanya shule za private kuliko hiyo mitihani yao ya sasa, huwezi kupima ubora wa mtu aliyekaa mtaani miaka nane(8) kwa mtihani tu.

Kama serikali inataka walimu bora basi ikubali kuingia gharama iwarudishe vyuoni hata kwa mwaka mmoja hawa walimu waliopo mtaani iwajengee uwezo upya, na sio kuleta mitihani ya siku moja ili kupima uwezo wa walimu.
Mitihani yote ya ualimu hutungwa kwa syllabus husika.

Mwalimu amefaulu na kupewa cheti tangu std 7, form 2, form 4 na huo wa ualimu.

Atapewa mtihani kwa mtaala na syllabus ipi??
 
Wanavyonyanyaswa Ni Kama vile huwa wanalipwa mabilioni ya pesa.
Kwani kada zingine wanalipwa mabilioni? Hata wa TGS B wanafanyishwa Mtihani. Ndio maana nasema walimu wengi hawajielewi, mitihani inafanywa mwaka wa 12 huu, kwa kuwa nje ya ualimu hakuna mnachofatilia ndio maana mnaona ajabu.

Secretary tu anafanyishwa Mtihani, secretary analipwa mabilioni?
 
Mitihani yote ya ualimu hutungwa kwa syllabus husika.

Mwalimu amefaulu na kupewa cheti tangu std 7, form 2, form 4 na huo wa ualimu.

Atapewa mtihani kwa mtaala na syllabus ipi??
Ngoja nikuulize swali, engineers wanaofanya Mtihani kwenye interviews wao hawakufaulu std 7? Form 2? Form 4??

Wewe unaelewa vipi unapoambiwa interview itakua ya mtihani? Ni nani kasema kuna mambo ya syllabus? Ndio maana nasema walimu hamna exposure

Mitihani ya aptitude test huwa wanafata syllabus? Hamjawahi kuomba kazi mashirika makubwa?
 
Walimu ni vilaza kweli watu waliofeli katika walimu kumi ukimpata mmoja mwenye division one nimekaa pale
 
Ngoja nikuulize swali, engineers wanaofanya Mtihani kwenye interviews wao hawakufaulu std 7? Form 2? Form 4??

Wewe unaelewa vipi unapoambiwa interview itakua ya mtihani? Ni nani kasema kuna mambo ya syllabus? Ndio maana nasema walimu hamna exposure

Mitihani ya aptitude test huwa wanafata syllabus? Hamjawahi kuomba kazi mashirika makubwa?
We ng'ombe, hao kada yao inafuata utaratibu huo na hata wanaposoma wanafahamu hilo.

Walimu wanaposoma wanafahamu kuwa wanapohitimu mafunzo ya nadharia na vitendo, kinachofuata ni ajira.

Tofautisha misingi ya kada.
 
Walimu ni vilaza kweli watu waliofeli katika walimu kumi ukimpata mmoja mwenye division one nimekaa pale
Hadi sasa bado hawajaelewa nini maana ya written interview. Nikisoma comments zao nabaki nashangaa tu

Mwalimu anauliza serikali ikiweka interview ya Mtihani watafata syllabus ipi, nchi ngumu

Hawajui kabisakuwa Mtihani wainterview huwa haufuati syllabus, huwa unapima knowledge kwenye kada husika. Mfano mchumi anaweza kuulizwa nini athari za Tanzania kubinafsisha bandari na zipi faida kiuchumi
 
Walimu wakifanyishwa mitihani kweye interview ni kuwanyanyasa, Ila engineers, wahasibu, maHR, maafisa ardhi, wachumi n.k, wao wakifanyishwa sio manyanyaso?
Walimu huwa hawajitambui mbona kada zingine mbona wanafanya interview pumbavu zao
 
We ng'ombe, hao kada yao inafuata utaratibu huo na hata wanaposoma wanafahamu hilo.

Walimu wanaposoma wanafahamu kuwa wanapohitimu mafunzo ya nadharia na vitendo, kinachofuata ni ajira.

Tofautisha misingi ya kada.
Hiyo unapohitimu kinaachofata ni ajira ndio ujinga unaenda kuisha kwa sasa. Ilikua hivyo sababu mahitaji yalikua makubwa, hata hao engineers wenyewe zamani kabisa enzi za mkapa hawakuwa wanafanya hata interview, walichukuliwa tu direct kama walimu

Nikuulize swali nyie walimu mnaosema mnasubiri ajira ndio mnachojua, kwani huwa hamjawahi ku-apply kazi kwenye mashirika binafsi? Nyie mnajua kazi yenu ni kufundisha tu wanafunzi?

UN Kuna kipindi walitoa tangazo wanahitaji graduate wa education Kama protection officer. Vipi huwa mnahisi hakuna interview?
 
Walimu huwa hawajitambui mbona kada zingine mbona wanafanya interview pumbavu zao
Mmoja hapo anasema walimu wao wanasoma ili kusubiri ajira sio interview. Ndio uone tatizo la Hawa watu, hawajui hata hizo kada zingine zamani ilikua hivyo sababu watu walikua wachache
 
Hadi sasa bado hawajaelewa nini maana ya written interview. Nikisoma comments zao nabaki nashangaa tu

Mwalimu anauliza serikali ikiweka interview ya Mtihani watafata syllabus ipi, nchi ngumu

Hawajui kabisakuwa Mtihani wainterview huwa haufuati syllabus, huwa unapima knowledge kwenye kada husika. Mfano mchumi anaweza kuulizwa nini athari za Tanzania kubinafsisha bandari na zipi faida kiuchumi
Binafsi katika kujipatia kipato nakata mapindi sio mwalimu by proffesional so nawafahamu hawa watu ,walimu wengi ualimu kwao ni bahati mbaya baada ya plan A zote kugoma ndio wakaangukia huko ....nawajua sana walimu acha wadharaulike kwa tabia zao mbovu ambzo naamin zinatokana na kuwa na shule ndogo kichwani we umesikia nchi gan ina ualimu daraja la 3.....?
 
We ng'ombe, hao kada yao inafuata utaratibu huo na hata wanaposoma wanafahamu hilo.

Walimu wanaposoma wanafahamu kuwa wanapohitimu mafunzo ya nadharia na vitendo, kinachofuata ni ajira.

Tofautisha misingi ya kada.
Acha kukariri mambo wewe.
 
Mmoja hapo anasema walimu wao wanasoma ili kusubiri ajira sio interview. Ndio uone tatizo la Hawa watu, hawajui hata hizo kada zingine zamani ilikua hivyo sababu watu walikua wachache
Kuna mmoja yeye haombagi private anasubiri za serikali maana za private anajua hatoboi interview zao kwan contents hana kichwani na kimalikia kinampiga chenga anasubiri shule za umma akawalipulie watoto wetu na huko kwa vile wanasoma wototo wa kajamba nani haina hawapati shida maana hata shule nzima ikipata zero salary inasoma kama kawa.
 
Back
Top Bottom