Tetesi: Walimu kupandishwa madaraja mwisho wa mwezi huu

Wewe ndo KICHWA NGUMU,mwaka wa pesa unaanza mwezi wa ngapi!? Ikiwa walipanda mwezi wa tano,au hujui hata mwaka wa fedha wa serikali huanza lini,ngoja nikuelimishe,mwaka wa fedha wa serikali huanza mwezi wa saba,hivyo waliopanda mwezi wa tano mwaka huu walipanda kwa bajeti ya mwaka jana,bajeti ya mwaka huu bado watu hawajapanda ndo hao wanaotegemewa kupanda
Una kichwa kigumu,hao waliopanda ni mwaka wa fedha ambao haujaisha.
 
Sio rahisi watu kula mselekeko. Ikitokea hiyo alhamisi Kila sekunde utatokea Uzi wa kumpongeza mama. Madogo wengi wanaJF walianza 2013-2016
 
Kuna tetesi kuwa serikali iko mbioni kuwapandisha madaraja walimu walioajiriwa miaka ya 2014 na 2015 ambao walikutana na mkono wa chuma wa JPM.

Kama ni kweli, naona kabisa ni maandalizi ya kuelekea uchaguzi 2025.
Hii ni kwa watumishi wote. Wametoa kitu kinaitwa kundi rika. Hapa mnufaika zaidi ni ajira 2015.
 
Ili uishi kwa amani km ww ni mwalimu hakikisha kazi ya ualimu usiiweke kabisa akilini
Usipo iweka akilini ualimu utatekelezaje majukumu yako kwa ufanisi?
Kikubwa kila mtumishi ajishughulishe na majukumu mengine ya ziada kuongezea kipato.
 
Back
Top Bottom