Walidhani Ezekiel Wenje na Lawrence Masha hawatoki kanda ya Ziwa?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,976
Watanzania hatujawahi kufikiria ukanda katika maisha yetu ya kijamii na kisiasa. Mimi kuna watu ninafanya nao kazi/biashara hata siwafahamu kabila lao achilia mbali sehemu wanayotoka.

Walichofanya CHADEMA kupitia kwa Tundu Lissu kinafanya tuanze kuuliza maswali ambayo wao wenyewe wana majibu kwa sababu wanaziangalia siasa nchini kwa jicho la ukanda na ukabila.

CHADEMA inayolalamika kuwa Rais Magufuli anapendelea kanda ya Ziwa imesahau kuwa ilipeleka majina mawili ya Ezekiel Wenje na Lau Masha ambao ni wanachadema kutoka kanda ya Ziwa ili wakachaguliwe kuwa wabunge wa bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki wakati ina wanachama katika maeneo mengine ya nchi.

Kupeleka bungeni watu wawili wanatoka katika kanda moja na dini moja hawakuona kama ni kupendelea kanda ya Ziwa?

CHADEMA haikuona kuwa kufanya hivyo ni kuendelea kutoa nafasi/vyeo/madaraka kwa watu wa kanda ya ziwa? Au huo ukanda wanauona kwa wengine tu?

Kama vigezo vya kuwateua havikuhusu ukanda, kwa nini wanadhani wengine watateua kwa vigezo vya ukanda?

Kilichoshangaza zaidi, CHADEMA ilipewa nafasi mbili za kuteua majina na ikatumia nafasi hizo kuteua majina ya watu wa kanda ya ziwa na wenye imani ya dini moja. Kwa nini hawakuteua majina kutoka kanda zingine ili ‘’kupunguza’’ wanaoteuliwa kutoka kanda ya Ziwa kama wanajua kuwa Rais Magufuli anapendelea watu wa kanda ya ziwa?

Wabunge hawakuwapa kura za ushindi kina Wenje na Masha ili kuingia EALA kwa sababu wanatoka kanda ya Ziwa bali walikataliwa kwa sababu wabunge walijua hawatoshi.

Mwandishi wa vitabu wa Kimarekani E. W. Howe aliwahi kusema, ‘’A thief believes everybody steals’’.

Mimi ninasema, mbaguzi hudhani kila mtu ni mbaguzi.

pic+EALA+results.jpg

Ezekiel Wenje na Lawrence Masha wakiwa kanisani.
 
Huu ndio mtazamo wangu

Kinacho endelea sasa ni Edward Lowassa na CHADEMA wanajaribu kujinasua kwenye tuhuma zao zile za uchochezi wa kidini kwa kumgeuzia mpira Raisi Magufuli kwa kutumia reference ya teuzi zake

Edward Lowassa na CHADEMA karibia watashitakiwa kwa makosa ya kuwataka baadhi ya watanzania wawe wa moto, na la kuwatetea viongozi wa kikundi cha itikadi kali (UAMSHO)
 
Kuna tofauti kati ya technical decision and nepotism!!!!
Mleta mada haeleweki. Nia yake ni kuficha ukweli. Wakina wenje walichaguliwa na viongozi kwavigezo maalum. Ccm wakawatoa kwa ajili ya chukiwalizokuwa nao tangu wakihame chama chao. Badala yake kupendekeza amateurs wasio na uzoefu kabisa kuleta aibu Tanzania kwa ajili chuki. Shame on us. We cannot even look after the intetests of our nation.
 
Hizo tuhuma za Lissu ni bullshit.

Hao wote aliowataja jana [kuhusu kuteuliwa kwao na Magufuli na eneo watokako] mimi hata sikujua wanatoka huko.

Sikujua Kamanda Sirro ni mtu wa kanda ya ziwa.

Sikujua Mwanasheria mkuu ni mtu wa kanda ya ziwa.

Na sikujua mkuu wa majeshi ni mtu wa kanda ya ziwa.

Ukiona mtu anatumia matusi, lugha ya kejeli, anatoa tuhuma za ukabila, udini, jinsia, na kadhalika basi ujue mtu huyo kafilisika kifikra na ki hoja.

Tanzania hii, ukanda wa ziwa ni sehemu kubwa sana. Ni sehemu yenye watu wengi sana.

Sasa katika watu wote wenye asili ya huko watakosekana kweli walio na sifa za kushikilia nafasi mbalimbali za serikali ya nchi?

Huyo so called wakili msomi hatukumsikia akiwapinga hao alowataja kwa kusema kuwa hawana sifa za kushikilia hizo nyadhifa walizonazo.

Alitaja tu kuwa eti wanatokea kanda ya ziwa ambako ndiyo atokeako na rais pia.

Supposedly hiyo ndo objection yake dhidi yao.

Tundu Lissu is a fool.
 
Wewe sio mfanyibiashara tu ! Una biashara ya siasa pia.uzia ccm inawafaa sana ila wenye vichwa vyao,na vinavyowaza ipasavyo,humpati mtu.

Mtaishia kununua madiwani,ila wananchi wote kununuliwa na nyie, ni ngumu sana.barikiwa sana na uwe na amani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huoni kuwa kwa kusoma na kujadili hoja zangu unanipigia chapuo la biashara ya siasa?

Ungekuwa unawaza ipasavyo nadhani usingepoteza muda wako kusoma na kutoa komenti kwenye mada ya watu wasiowaza ipasavyo!
 
Huu ndio mtazamo wangu

Kinacho endelea sasa ni Edward Lowassa na CHADEMA wanajaribu kujinasua kwenye tuhuma zao zile za uchochezi wa kidini kwa kumgeuzia mpira Raisi Magufuli kwa kutumia reference ya teuzi zake

Edward Lowassa na CHADEMA karibia watashitakiwa kwa makosa ya kuwataka baadhi ya watanzania wawe wa moto, na la kuwatetea viongozi wa kikundi cha itikadi kali (UAMSHO)
Kama hiyo ndio mikakati yao basi wamepotea njia!

Wanachofanya ni kurusha mawe wakati wanaishi kwenye nyumba ya vioo!
 
Kuna tofauti kati ya technical decision and nepotism!!!!
Mleta mada haeleweki. Nia yake ni kuficha ukweli. Wakina wenje walichaguliwa na viongozi kwavigezo maalum. Ccm wakawatoa kwa ajili ya chukiwalizokuwa nao tangu wakihame chama chao. Badala yake kupendekeza amateurs wasio na uzoefu kabisa kuleta aibu Tanzania kwa ajili chuki. Shame on us. We cannot even look after the intetests of our nation.
Kama kina Wenje na Masha waliteuliwa kwa vigezo maalum, kwa nini unadhani wengine hawateui kwa vigezo maalum?

Talk about nepotism, hujui kuwa Tundu Lissu alimteua Dada yake kuwa Mbunge wa viti Maalum wa CHADEMA lakini watanzania wengi hatukuona kama ni nepotism bali ni uwezo wake wa kazi.

Wao wateue watu wa kanda hiyo kwa vigezo maalum halafu wengine wakifanya wanawaita wakanda.

Hoja yako inashangaza sana!
 
Hizo tuhuma za Lissu ni bullshit.

Hao wote aliowataja jana [kuhusu kuteuliwa kwao na Magufuli na eneo watokako] mimi hata sikujua wanatoka huko.

Sikujua Kamanda Sirro ni mtu wa kanda ya ziwa.

Sikujua Mwanasheria mkuu ni mtu wa kanda ya ziwa.

Na sikujua mkuu wa majeshi ni mtu wa kanda ya ziwa.

Ukiona mtu anatumia matusi, lugha ya kejeli, anatoa tuhuma za ukabila, udini, jinsia, na kadhalika basi ujue mtu huyo kafilisika kifikra na ki hoja.

Tanzania hii, ukanda wa ziwa ni sehemu kubwa sana. Ni sehemu yenye watu wengi sana.

Sasa katika watu wote wenye asili ya huko watakosekana kweli walio na sifa za kushikilia nafasi mbalimbali za serikali ya nchi?

Huyo so called wakili msomi hatukumsikia akiwapinga hao alowataja kwa kusema kuwa hawana sifa za kushikilia hizo nyadhifa walizonazo.

Alitaja tu kuwa eti wanatokea kanda ya ziwa ambako ndiyo atokeako na rais pia.

Supposedly hiyo ndo objection yake dhidi yao.

Tundu Lissu is a fool.
Mkuu;

Sikutegemea kusikia alichokisema.

Kinachoshangaza zaidi, Tundu Lissu sio siku nyingi alisema Rais Magufuli hamuamini Naibu Jaji Mkuu ndio maana mpaka sasa hajamteua kuwa Jaji Mkuu, Juzi tena anakuja na madai akisema Rais Magufuli amemteua Naibu Jaji Mkuu kwa sababu anatoka kanda ya Ziwa.

Sasa kama Rais Magufuli anateua kwa kupendelea kanda ya Ziwa, inakuwaje anamteua mtu kwa kigezo cha ukanda halafu hapo hapo anakuwa hamuamini? Hoja zake zinagongana kimantiki.

Jamaa amekuwa mropokaji mzuri sana na mbaya zaidi anasahahu hata alichokisema kabla ya kusema hoja nyingine.
 
Hii kauli mbiu unataka kuinyima haki.


''Where we dare to talk openly"
Basi nitasema. Suala la ukanda halina nafsi kikatba, kisheria wala kisiasa,kisiasa. kuongelea ukanda ni kupotoka. CCM ilipotoka pale waliposema kuwa wagombea ubunge Wenje na Masha wametoka jimbo moja, wilaya moja mkoa mmoja, kanda moja na dini moja. Na CHADEMA nayo imepotoka kuiga nyayo potovu za CCM kwenye jambo lilelile.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo tuhuma za Lissu ni bullshit.

Hao wote aliowataja jana [kuhusu kuteuliwa kwao na Magufuli na eneo watokako] mimi hata sikujua wanatoka huko.

Sikujua Kamanda Sirro ni mtu wa kanda ya ziwa.

Sikujua Mwanasheria mkuu ni mtu wa kanda ya ziwa.

Na sikujua mkuu wa majeshi ni mtu wa kanda ya ziwa.

Ukiona mtu anatumia matusi, lugha ya kejeli, anatoa tuhuma za ukabila, udini, jinsia, na kadhalika basi ujue mtu huyo kafilisika kifikra na ki hoja.

Tanzania hii, ukanda wa ziwa ni sehemu kubwa sana. Ni sehemu yenye watu wengi sana.

Sasa katika watu wote wenye asili ya huko watakosekana kweli walio na sifa za kushikilia nafasi mbalimbali za serikali ya nchi?

Huyo so called wakili msomi hatukumsikia akiwapinga hao alowataja kwa kusema kuwa hawana sifa za kushikilia hizo nyadhifa walizonazo.

Alitaja tu kuwa eti wanatokea kanda ya ziwa ambako ndiyo atokeako na rais pia.

Supposedly hiyo ndo objection yake dhidi yao.

Tundu Lissu is a fool.

Nimependa

Umemaliza sina la kuongeza kwa kweli.
 
Watanzania hatujawahi kufikiria ukanda katika maisha yetu ya kijamii na kisiasa. Mimi kuna watu ninafanya nao kazi/biashara hata siwafahamu kabila lao achilia mbali sehemu wanayotoka.

Walichofanya CHADEMA kupitia kwa Tundu Lissu kinafanya tuanze kuuliza maswali ambayo wao wenyewe wana majibu kwa sababu wanaziangalia siasa nchini kwa jicho la ukanda na ukabila.

CHADEMA inayolalamika kuwa Rais Magufuli anapendelea kanda ya Ziwa imesahau kuwa ilipeleka majina mawili ya Ezekiel Wenje na Lau Masha ambao ni wanachadema kutoka kanda ya Ziwa ili wakachaguliwe kuwa wabunge wa bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki wakati ina wanachama katika maeneo mengine ya nchi.

CHADEMA haikuona kuwa kufanya hivyo ni kuendelea kutoa nafasi/vyeo/madaraka kwa watu wa kanda ya ziwa? Au huo ukanda wanauona kwa wengine tu?

Kama vigezo vya kuwateua havikuhusu ukanda, kwa nini wanadhani wengine watateua kwa vigezo vya ukanda?

Kilichoshangaza zaidi, CHADEMA ilipewa nafasi mbili za kuteua majina na ikatumia nafasi hizo kuteua majina ya watu wa kanda ya ziwa na wenye imani ya dini moja. Kwa nini hawakuteua majina kutoka kanda zingine ili ‘’kupunguza’’ wanaoteuliwa kutoka kanda ya Ziwa kama wanajua kuwa Rais Magufuli anapendelea watu wa kanda ya ziwa?

Wabunge hawakuwapa kura za ushindi kina Wenje na Masha ili kuingia EALA kwa sababu wanatoka kanda ya Ziwa bali walikataliwa kwa sababu wabunge walijua hawatoshi.

Mwandishi wa vitabu wa Kimarekani E. W. Howe aliwahi kusema, ‘’A thief believes everybody steals’’.

Mimi ninasema, mbaguzi hudhani kila mtu ni mbaguzi.

pic+EALA+results.jpg

Ezekiel Wenje na Lawrence Masha kutoka kanda ya Ziwa wakiwa kanisani.

Safi sana

Sina la kuongeza
 
Huoni kuwa kwa kusoma na kujadili hoja zangu unanipigia chapuo la biashara ya siasa?

Ungekuwa unawaza ipasavyo waka usingepoteza muda wako kusoma na kutoa komenti kwenye mada ya watu wasiowaza ipasavyo!

Msemajiukweli kadiri mnavyojitahidi kuleta post nyingi kutaka kuonyesha kwamba Lissu kakosea ni kama mnatuona wajinga fulani hivi. Ungeniambia kwenye maelezo yake kuna sehemu kwenye maelezo yake alivuka mipaka ningekuelewa, lakini majibu ya jumla kwenye hoja zile ni kutuona watoto. Mbali ya aina ya uwasilishaji aliotumia Lissu kutowapendeza baadhi ikiwepo ww haimaanishi hakusema kweli.

Nadhani wanaccm mtakuwa mmesahau au mnajitoa ufahamu ama pia hamkutegemea mbegu ya ukabila na udini mliyopanda ingetoa mavuno haya. Ni ukweli ulio dhahiri wanaccm waliendesha siasa za majitaka dhidi ya cdm hadharani au kwa kificho baada ya kuzidiwa hoja. Nyie ccm ndio mliendesha kampeni chafu eti cdm ni chama cha wachaga kisa mwenyekiti wa cdm ni mchaga na baadhi ya viongozi wake walioisumbua ccm ni wachaga ikiwemo muanzilishi. Cdm walijitahidi kuondoa fitina ile kwa maelezo wachaga hao walipata nafasi zao kwa uwezo na uchaga ni coincedence tu. Lakini ilikuwa ngumu kwani mpaka viongozi waandamizi waliendelea kumwaga sumu hiyo. Leo hiyo sumu imesambaa mnashangaa nini wakati ni kazi ya mikono yenu?

Hamkuishia hapo bali mliihusisha cdm na ukristo kisa Dr. Slaa alimzidi JK hoja na wengi wa viongozi wa juu wa cdm ni wakristu. Kuna ubaya gani Lissu akitumia kisu mlichokinoa wenyewe kukatia mnofu?

Kwa aina ya utawala wa mkulu ni mtu anayeamini katika nguvu kuliko diplomasia hilo halina ubishi. Iwapo yeye anatokea kanda ya ziwa, cdf na Igp wote ni wa kanda ya ziwa ulitaka Lissu aseme nini zaidi ya alichokisema. Hao viongozi wawili wa juu wa jeshi ndipo ilipo roho ya Magufuli kutawala, katiba anaifuata pale isipombana tu. Kumbuka Lissu sio mwendawazimu bali ni mwerevu ila mwenye jazba na haiondoi ukweli wa kile alichokisema ukiachia mbali ya kuwa kuna sehemu alivuka mipaka.
 
Back
Top Bottom