kakuruvi
JF-Expert Member
- Sep 2, 2009
- 770
- 256
Salam JF's woote,
Valentine ndiyo hiyoo, tusubiri ya mwaka ujao panapomajaliwa, mwenzetu mmoja alipata msukosuko ila aliumaliza kiutu uzima.
Jamaa walikorofishana na mama watoto wake mpaka ikafikia mamaa kufungasha nguo zake ili asubuhi aondoke, usiku jamaa akamuuliza vipi mbona unafungasha? mkewe akajibu asubuhi naenda kwa mama yangu, jamaa hakupata usingizi, asubuhi akawahi kuamka mapema akaanza na yeye kufungasha mkewe akamuuliza mbona unafungasha? jamaa akamjibu naenda kwa mama yangu, mkewe kwa mshangao akamuuliza tena unaenda kwa mama yako watoto je? Jamaa akamjibu wataenda kwa mama yao..
Zoezi la kwenda kwa mama liliishia hapo na wote wakaelekea kazini. Wana JF nani mjanja hapo?
Valentine ndiyo hiyoo, tusubiri ya mwaka ujao panapomajaliwa, mwenzetu mmoja alipata msukosuko ila aliumaliza kiutu uzima.
Jamaa walikorofishana na mama watoto wake mpaka ikafikia mamaa kufungasha nguo zake ili asubuhi aondoke, usiku jamaa akamuuliza vipi mbona unafungasha? mkewe akajibu asubuhi naenda kwa mama yangu, jamaa hakupata usingizi, asubuhi akawahi kuamka mapema akaanza na yeye kufungasha mkewe akamuuliza mbona unafungasha? jamaa akamjibu naenda kwa mama yangu, mkewe kwa mshangao akamuuliza tena unaenda kwa mama yako watoto je? Jamaa akamjibu wataenda kwa mama yao..
Zoezi la kwenda kwa mama liliishia hapo na wote wakaelekea kazini. Wana JF nani mjanja hapo?