Wale wa TRA mkeka upo hewani

Wale wa TRA mkeka upo hewani

Ndo inakuja ishu ya ubora wa vyuo, maana huwezi kuipata GPA kubwa kwenye vyuo makini kama ukiwa kilaza.
Ubora wa vyuo unapimwaje kaka? Kwa kufaulisha sana au kwa kufundisha vizuri au kutoa mitihani mepesi au migumu? Hebu fikiria hili na lipo sana vyuoni, chuo ni bora sana ila mwanafunzi anajibebisha kwa walimu wamuongezee marks na wengine wanajiliza kabisa na kutoa sababu kemkem kama Mimi ni maskini nikifeli nitaenda wapi? Mwalimu anashikwa na huruma anamuongezea hata marks 10 kwenye coursework na ikatokea final UE akapambana akapata B+ ,unataka kusema huyo akipata GPA 4 Kwa nyongeza za marks atakuwa na uwezo mkubwa kuliko aliyepata 3.8 bila nyongeza ya marks?
 
Kweli kabisa .

Sema wachangiaji wengi humu ni lower performance ndio maana wanatetea kuacha kwa wenye GPA kubwa sababu ya wivu n.k.
Ni mawazo yako tu. jifunze kufanya vitu Kwa umakini uone faida zake. Unaweza kuta kampuni inatangaza ajira huambiwi uambatanishe vyeti wala nini ila utume CV tu au mara nyingine CV na Barua. Unadhani hii kampuni itatumia kigezo Cha ufaulu au GPA kufanya shortlisting wakati umetuma CV tu?
 
You are bitter and sour, mafanikio hayaji ukiwa na mentality hiyo. Huyo wa Lower maana yake amejiuza vizuri kwenye CV na Cover letter, huko kazini hawaendi kufundisha bali kuperform sasa GPA ni jambo moja na performance ya kazi kwa kutumia pattern zile zile kila siku zinahitaji mtu mchakalikaji,mbunifu na anayejua kujieleza.

Unaonekana hata ofisini akija mteja utakuwa unamtishia na GPA. Tumia huu muda kuandaa CV nzuri hawa TRA hawatachukua muda watatangaza kazi nyingine sasa kama wewe utakuwa umekaa kuringia GPA badala ya kuangalia ulipo jikwaa na zenyewe zitakupita ingawa nakuombea ufanikiwe.

Jumapili njema.
Kama una gpa ndogo ni dalili kwamba wewe sio mtu uliye serious na hujitumi.

Huwezi linganisha mtu mwenye 4.5 na mtu mwenye 2.1 gpa.
 
Ni muhimu sasa kuvipima hivi vyuo vyetu kama vinatoa elimu yenye ubora unaotakiwa.......nilitegemea watu waliosoma kozi ya aina moja na wakapata first class wawe na uwezo uleule bila kujali chuo walichosoma.
Kwa hiyo unategemea watu wanaosoma feza boys au girls secondary wawe na uwezo sawa kama wale wanaosoma makamba secondary Kwa sababu wote wanasoma masomo yaleyale ya sekondari?

Huwezi kutegemea hivyo Kwa sababu ya heshima na ubora vyuo vilivyojijengea. Hata Kwa Marekani Havard ni chuo Bora kuliko vingine ,ipo hivyo. Mtu aliyesoma Havard na kupata GPA ya 3.5 ya uchumi ni bora kuliko aliyesoma IAA na kupata GPA 4.8 kwenye uchumi
 
Kuna mtu ako na GPA ya 4 lakini jina halijatoka shortlisted

Lakini wenye lower second majina yametokea kwenye shortlisted,

Hii inaingiaje akilini?
We jamaa mshamba wa wapi ?kama GPA Ya uwizi.

Kweny shortlisted wanaangalia vigezo vya ghafla tena vya nje vya kufuata taratibu hapo hawajakagua GPA.

Kama ni wewe akili zako na uwezo ni mdogo labda ulikuwa wazee wa kuiba paper na kuhonga kuboost ufaulu.

Vigezo vya awala kama uandishi wa barua na kujaza taarifa nyingine mpaka kufika asimilia kadhaa ....Utakuta wenzio wamejaza taarifa zenye ushawishi na wewe una asilimia 60 tu ....Tafuta kazi ya kufanya.
 
Kama una gpa ndogo ni dalili kwamba wewe sio mtu uliye serious na hujitumi.

Huwezi linganisha mtu mwenye 4.5 na mtu mwenye 2.1 gpa.
Kwa hiyo GPA ya 4.5 ya IAA ni bora GPA ya 3.0 kutoka Havard? Mwenye GPA kubwa ya IAA na GPA ya Havard ,nani anauzika zaidi?
 
Kwa hiyo unategemea watu wanaosoma feza boys au girls secondary wawe na uwezo sawa kama wale wanaosoma makamba secondary Kwa sababu wote wanasoma masomo yaleyale ya sekondari?

Huwezi kutegemea hivyo Kwa sababu ya heshima na ubora vyuo vilivyojijengea. Hata Kwa Marekani Havard ni chuo Bora kuliko vingine ,ipo hivyo. Mtu aliyesoma Havard na kupata GPA ya 3.5 ya uchumi ni bora kuliko aliyesoma IAA na kupata GPA 4.8 kwenye uchumi
Naongelea vyuo vya hapa ndani maana vyote viko regulated na TCU......kwa nini ionekane vyuo vingine vinafyatua vilaza wenye first class, tatizo linakuwa ni nini? kwa hilo la sekondari umebugi maana hizo feza boys na girls ni majina tu ndo maana kijana aliyesomea sekondari ya kata anaweza kuongoza kitaifa kwa sababu ni kichwa kuliko hao wa feza boys na girls. Na pia kuna vichwa wa kutokea vyuo vya kiafrika ambao wanaweza kufanya maajabu wanapoenda kusoma post-graduate huko Havard.​
 
Naongelea vyuo vya hapa ndani maana vyote viko regulated na TCU......kwa nini ionekane vyuo vingine vinafyatua vilaza wenye first class, tatizo linakuwa ni nini?
GPA za vyuo ni kitu universal ndio maana Kwa degree iliyopatika mlimani inatambuliwa pia Marekani lakini swali ni kwamba hata kama elimu ya chuo ni universal ,ni kweli Havard ni sawa na UDSM kwenye ubora?

Ipo hivyo dunia nzima na hata Marekani GPA ya Havard ni tofauti na za vyuo vingine
 
GPA za vyuo ni kitu universal ndio maana Kwa degree iliyopatika mlimani inatambuliwa pia Marekani lakini swali ni kwamba hata kama elimu ya chuo ni universal ,ni kweli Havard ni sawa na UDSM kwenye ubora?

Ipo hivyo dunia nzima na hata Marekani GPA ya Havard ni tofauti na za vyuo vingine
Kuna swala la uwezo binafsi wa mtu haijalishi kasomea chuo gani, kama contents za UDSM ziko sawa na Havard hapo kinachoamua ni kichwa na siyo jina la chuo.
 
Kuna swala la uwezo binafsi wa mtu haijalishi kasomea chuo gani, kama contents za UDSM ziko sawa na Havard hapo kinachoamua ni kichwa na siyo jina la chuo.
Unanifurahisha sana. Tuzungumze Kwa mifano halisi sana: kama content za Havard na za UDSM zipo tofauti ina maana ya kwamba content za Havrard ni Kwa mazingira ya Marekani na Content za UDSM ni Kwa mazingira ya Tanzania ,swali: Mbona watanzania waliosoma UDSM Uchumi wanaenda kufanya kazi Marekani na wakati content za UDSM hazijawaanda Kwa mazingira ya Marekani?
 
Kuna swala la uwezo binafsi wa mtu haijalishi kasomea chuo gani, kama contents za UDSM ziko sawa na Havard hapo kinachoamua ni kichwa na siyo jina la chuo.
Tuzungumzie suala la uwezo binafsi wa mtu Kwa kuangalia na suala la ajira kwa hiyo unakubaliana na Mimi kwamba GPA sio kigezo rasmi Cha kupima uwezo wa mtu kwenye ajira Kwa sababu inawezekana mwenye uwezo mkubwa sana lakini kwa kusoma Havard akashindwa kupata GPA kubwa lakini mwenye uwezo mdogo lakini Kwa kusoma IAA akapata ufaulu mkubwa sana. Je, kwenye suala la ajira tumfanye huyu mwenye GPA kubwa ni genius na huyu mwenye ndogo ni kilaza Kwa sababu tunaangalia GPA?

Ndio maana nimesema hapo juu kwamba wakati wa kufanya Maombi baadhi ya taasisi huhitajiki kuambatanisha vyeti ila ni CV na Barua tu na Kwa kufanya hivyo yawezekana mwenye GPA kubwa akaachwa na mwenye ndogo akachukuliwa ,je mpaka hapo mchakato utakuwa na dosari Kwa sababu mwenye GPA kubwa kaachwa?

Tuje kwenye uhalisia halisi ambao ni suala la ajira za TRA ,je umejuaje kama suala la GPA limeangaliwa ? Kwa sababu vyeti vimeambatanishwa? Je, kama walitaka kujiridhisha kama kweli una kiwango Cha elimu kinachohitajika?
 
Wenye GPA zao Wana hasira Sana. Vumilieni Tu that's how life works.
Maisha ni kutesa Kwa zamu.
 
Wandugu kama una desa lolote la Tax Mgt officer tafadhali tuwekee hapa, tuwafanyie wepesi ndugu zetu wapate pakuanzia, karibuni tafadhali
 
Back
Top Bottom