Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
Vijana wale wawili walikuwa wasomi, na walionekana kuwa asset kubwa katika chama kama ilivyokuwa kwa Tony Blair na Gordon Brown katika uongozi wa chama cha Labour. Vijana wale walipitia safari ndefu katika chama, hatimae waliwekwa makao makuu ya Chama Dodoma, mmoja akiwa msaidizi wa Pius Msekwa akiwa Speaker na mwingine akiwa msaidizi wa John Malecela akiwa waziri mkuu.
Wabunge wa wakati ule walipata shida sana ya usafiri wa kuwafikisha bungeni, magari yalisafiri usiku na wengi walilala njiani, wengine iliwachukua siku tatu/nne kufika bungeni. Ilipitishwa wabunge wote watakopeshwa mashangingi ili yawasaidie usafiri.
Waziri Mkuu alifanya biashara nzuri sana na kampuni ya Toyota, hakika wenye kampuni hawakutegemea kuwa kainchi masikini kale kanaweza kununua mashangingi zaidi ya 200 kwa mpigo tena kwa pesa taslimu. Makubaliano yalikuwa waziri mkuu apate 10% ya transaction ile.
Kama mnavyojua kuwa pesa za namna hii haziingizwi bank, basi wawakilishi wa kampuni ya Toyota walikuja na pesa kwenye briefcase wakimtamfuta waziri mkuu, bahati mbaya au nzuri waziri mkuu alikuwa safarini, lakini walipouliza, msaidizi wa waziri mkuu aliwakaribisha ofisini kwake, kijana mtanashati na mwenye sura ya kuvutia. Aliwaambia kama wana maagizo yeyote kwa waziri mkuu wamuachie yeye kwani yeye ni msaidizi wake. Ndipo briefcase lilipoachwa ofisini, msaidizi alifungua briefcase baada ya wageni kuondoka, alichokiona hakutegemea, alilichukua briefcase lile mpaka nyumbani kwake na kukaa kimya.
Waziri mkuu aliporudi aliuliza kama kuna wageni waliomfuata na kumkosa, alipewa habari yote lakini alipomuuliza msaidizi alikana, biashara yote ni ya mazabae, waziri mkuu hakuweza kulipeleka swala hili kokote.
Huu ndiyo mwanzo wa utajiri wa msaidizi na uhasama aliojijengea na watu wa chama.
Wabunge wa wakati ule walipata shida sana ya usafiri wa kuwafikisha bungeni, magari yalisafiri usiku na wengi walilala njiani, wengine iliwachukua siku tatu/nne kufika bungeni. Ilipitishwa wabunge wote watakopeshwa mashangingi ili yawasaidie usafiri.
Waziri Mkuu alifanya biashara nzuri sana na kampuni ya Toyota, hakika wenye kampuni hawakutegemea kuwa kainchi masikini kale kanaweza kununua mashangingi zaidi ya 200 kwa mpigo tena kwa pesa taslimu. Makubaliano yalikuwa waziri mkuu apate 10% ya transaction ile.
Kama mnavyojua kuwa pesa za namna hii haziingizwi bank, basi wawakilishi wa kampuni ya Toyota walikuja na pesa kwenye briefcase wakimtamfuta waziri mkuu, bahati mbaya au nzuri waziri mkuu alikuwa safarini, lakini walipouliza, msaidizi wa waziri mkuu aliwakaribisha ofisini kwake, kijana mtanashati na mwenye sura ya kuvutia. Aliwaambia kama wana maagizo yeyote kwa waziri mkuu wamuachie yeye kwani yeye ni msaidizi wake. Ndipo briefcase lilipoachwa ofisini, msaidizi alifungua briefcase baada ya wageni kuondoka, alichokiona hakutegemea, alilichukua briefcase lile mpaka nyumbani kwake na kukaa kimya.
Waziri mkuu aliporudi aliuliza kama kuna wageni waliomfuata na kumkosa, alipewa habari yote lakini alipomuuliza msaidizi alikana, biashara yote ni ya mazabae, waziri mkuu hakuweza kulipeleka swala hili kokote.
Huu ndiyo mwanzo wa utajiri wa msaidizi na uhasama aliojijengea na watu wa chama.