Wale tuliosoma Kibasila secondary.

Mimi nilisoma advance ila niliipenda sana ile shule kwa sababu nyingi kama;
1.Hakukuwa na matabaka sana.
2.Mkuu alikuwa peace kipindi hiko ni Mwl Urasa msaidizi Mwl Anania.
3.Ufundishaji ni mzuri mfano Sir Mathias alikuwa mtata ila anajua kufundisha.
4.Kiwanda cha Serengeti kilikuwa kinatoa harufu nzuri yani naimis sana.
5.Shule ilikuwa karibu na ofisi ya Mzee kwaiyo nilikuwa nashushwa na gari la mzee getini(mana mimi ni wakishua) wanafunzi wananishangaa.
6.Kubwa kuliko ni, watoto wa kike wa o-level walikuwa wanatukubali advance yani ukikaa kwenye vimbweta lazima wakuletee swali, mimi nilipata kama wanne hivi mmoja nipo nae hadi leo tumeshakuwa.
Vitu vilivyokuwa vinanikera.
1.Ajali kwenye high way(machinjoni)pale pamepoteza maisha ya wanafunzi wengi.
2.Bifu kati ya boys wa o-level yani wavaa kaki na boys wa advance.
3.Advance kupewa madarasa ya kawaida wakati o-level wanakaa ghorofani.
Dah Kibasila high school naikumbuka sana, nilipomaliza nilisikitika.

Kuhusu Advance kupewa madarasa ya chini na olevel kupewa ghorofa hilo ni sawa. O'level ipo mpaka mingi na tulikua tunasomea jengo la ghorofa wakati huo pale kwenye majengo ya advance kulikua na mti mkubwa tulikua tunakaa tunapaita Kibasila Beach. Ni Mwl. Kivugo tu ndio alikua anaweza kufika kibasila beach kuvunja kijiwe.

Harufu ya kimea pale Serengeti aisee inapendeza.

Ila mlikua washamba kuweka bifu na madogo.

Hahahaa... wa Kishua kuachwa getini wakati kuna wanafunzi walikua wanakuja na ndinga zao wanapaki chini ya Mkungu.
 
Nakumbuka nlipata additional math 13 nikiwa form one ....nikahamie French napo sikudumu nikasema haya ma~option basi ...
 
Pamoja sana mimi nimeondoka pale 2001 form 4 baada ya miaka michache nje ya tz niliporudi nikapitia pale nikamkuta mwl kivugo na wengine bado wapo hapo,ilikua ukumbusho mzuri.
Daah Safi Sana kivugo alikuwepo ?mi nilimwacha , wengine ngadala, mama mabruki, marehemu babu raja kwenye mihogo, mwakalinga Mzee wa French etc
 
Hao
Mimi nilisoma advance ila niliipenda sana ile shule kwa sababu nyingi kama;
1.Hakukuwa na matabaka sana.
2.Mkuu alikuwa peace kipindi hiko ni Mwl Urasa msaidizi Mwl Anania.
3.Ufundishaji ni mzuri mfano Sir Mathias alikuwa mtata ila anajua kufundisha.
4.Kiwanda cha Serengeti kilikuwa kinatoa harufu nzuri yani naimis sana.
5.Shule ilikuwa karibu na ofisi ya Mzee kwaiyo nilikuwa nashushwa na gari la mzee getini(mana mimi ni wakishua) wanafunzi wananishangaa.
6.Kubwa kuliko ni, watoto wa kike wa o-level walikuwa wanatukubali advance yani ukikaa kwenye vimbweta lazima wakuletee swali, mimi nilipata kama wanne hivi mmoja nipo nae hadi leo tumeshakuwa.
Vitu vilivyokuwa vinanikera.
1.Ajali kwenye high way(machinjoni)pale pamepoteza maisha ya wanafunzi wengi.
2.Bifu kati ya boys wa o-level yani wavaa kaki na boys wa advance.
3.Advance kupewa madarasa ya kawaida wakati o-level wanakaa ghorofani.
Dah Kibasila high school naikumbuka sana, nilipomaliza nilisikitika.
a level walikuwa wapuuzi Tu , Kibasila original Ni shule ya o level , sasa wanalalamika nn ?
 
Sijasoma Kibasila lakini nilikuwa natimba sana pale kwenda kula mihogo ya Mzee Rajabu ya shilingi tano tano! Kudadadeki, miaka ya 90 hiyo, watu tunatoka Kurasini hadi Kibasila kw ajili ya mihogo huku tukiipita mihogo ya Willy pale Jitegemee na mihogo ya kishua pale jirani Kanisa la Anglican Kurasini!
Daah Safi Sana mkuu, babu raja chachandu na mihogo yake ilikuwa bomba
 
Back
Top Bottom