Jephta2003
JF-Expert Member
- Feb 27, 2008
- 6,501
- 6,200
Mama ni mama tu.Hapa kila mtu namwona anamapenzi na mamake hongereni. Ila mi na mamangu tumechokana kila kukicha ni stress tupu. Malezi yake yamefanya Sina bond na yeye hata kidogo, moyo wangu hauwezi sema kwamba nampenda, na wala simchukii ila huwa ananitia hasira na negative energy, sidhani kama siku akifa ntaumia au ntamkumbuka.
Kwa sababu yuko haiHapa kila mtu namwona anamapenzi na mamake hongereni. Ila mi na mamangu tumechokana kila kukicha ni stress tupu. Malezi yake yamefanya Sina bond na yeye hata kidogo, moyo wangu hauwezi sema kwamba nampenda, na wala simchukii ila huwa ananitia hasira na negative energy, sidhani kama siku akifa ntaumia au ntamkumbuka.
Daah!!so sorry, R.i.p mamaNikikumbuka siku nakuchukua hospitali, madaktari wakisema urudi tu nyumbani hamna namna...ugonjwa(cancer) umeenea mwili mzima, ukibaki hospitali gharama zitaongezeka...Nililia sana, nawe ulilia sana....ukiniambia, "mwanangu God Heals, madokta wameshajua hali ni mbaya...sina mda wa kuendelea kuishi. Umenipambania tangu siku ya kwanza miaka 5 iliyopita....leo imefikia." Uliongea kwa uchungu sana...tukarudi nyumbani....ukanisihi mengi sana, ukanikumbusha mengi sana, na ukaniomba niendelee kuwapenda wadogo zangu.
Ukanitania....ukilazimisha furaha, "mwanangu God Heals naondoka bila kumwona mjukuu wangu...ningependa sana kumbeba mme au mke mwenzangu, ila naondoka bila kumwona mjukuu..." Tukacheka huku mioyo ikiuma sana. Lilikuwa tabasamu la mwisho....
Nakumbuka kesho ukaomba nimpigie dada aje nyumbani, aje na mjukuu wako....kweli nilifanya hivyo...nao wakafika.... Tukaongea tukiwa na hudhuni sana... ukawa unajitahidi kutabasamu huku ukilalamika moyo unakuuma, mara mbavu, mara miguu, mara kichwa, mara mikono.... Ukatuangalia wote, kila mmoja kwa wakati wake... Ukiwa mbele ya mumeo kipenzi, watoto wako watatu, mjukuu wako mmoja, ukaanguka chini... ukajilaza... na hukufumbua macho tena.
Ni miaka 6 sasa imepita, Pumzika kwa amani mama, pumzika salama...katika siku hii sina pa kushika kila nikikumbuka maneno yako, na wakati ule mgumu, wa mwisho pale hospitali. Tutakumbuka kwa nasaha zako. Hakika ulikuwa mwema kwetu.
Lala salama mama yetu kipenzi.
Pole sana mkuu.R.i.p momR.I.P japo sikukuona uliniacha mikononi mwa Docter
I wish ungekuwepo sizani ningekuwa hv
Pole mkuuPumzika kwa amani mama, uliniacha nikiwa na miaka 20, sasa hivi nina watoto, natamani ungekuwepo walau wakuite bibi, natamani ungekuwepo unione vile nafuata uliyonifunza katika maisha....
Ulikuwa rafiki yangu, nakumbuka nilipokuwa nasoma O-level shule ya day, mimi ndio nilikuwa nakaa na pesa zako za biashara, weekend unanituma nikafunge mzigo.
Nilipokuwa A level, nikirudi home unaniambia biashara imekuingizia kiasi gani kwa kipindi nilipokuwa shule. Baada ya kumaliza form 6 ukanikabidhi biashara niwe msimamizi, Tulifanya kazi kwa bidii mpaka naenda chuo nilikuwa na pesa nyingi kwenye account. Sasa hivi ndio nimegundua kumbe ulikuwa unanifundisha kuwa independent...malezi yako yamenifanya kuwa strong! I will be a good mom to my kids also, i loove youuu ...
Uwiiii machozi yananitoka.
Mmmmh!! Humjui mamangu wala familia yangu. Huijui abuse wewe wala huijui traumatic experience, hujakulia kwenye toxic family inayoleta matatizo ya kisaiklojia. Huijui Post traumatic disorder wala depression wewe. Huwezi kuelewa.Mama ni mama tu.
Katika mabaya kumi sidhani Kama hakuna jema hata moja alilowahi kukufanyia.
Jifunze kumthamini mama yako..kuna watu wanatamani wangekuwa naye Hata huyo unayemuona hafai.
Siku ukimpoteza hutaongea haya unayoyaongea.
Thamani ya kitu huonekana kikitoweka.
Jifunze kuona thamani ya kitu kingali kipo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Samahani Kama nitakuwa nimekukwaza.Mmmmh!! Humjui mamangu wala familia yangu. Huijui abuse wewe wala huijui traumatic experience, hujakulia kwenye toxic family inayoleta matatizo ya kisaiklojia. Huijui Post traumatic disorder wala depression wewe. Huwezi kuelewa.
Thanks bro! I hope so, always she is with I.POLE SANA NDUGU...SHE IS WATCHING YOU OVER wherever she is