Wala bata wa JF

Wala bata wa JF

1775647738384.jpg
 
Bata batani, wana wa stress free zone

Don't take it personal... Wala usichukulie wahusika wa mada hii ni watu wa nyodo wenye nazo na wanaopenda show off... La hasha... Hata wewe ni sehemu ya mada hii.. Hata kama uko kibanda umiza kwa mama muuza na jero yako ukila ngumu kumeza na cheni bloku.. Bado unakula bata...

Ama la uko na mkoko wa mwana kakuazima uoshee.. Bado ni moment ya kula bata.. Weee tupia tuu... Lakini ficha plate number

Hata kama mmealikwa kwenye karamu ya ofisi, jirani, ndugu, harusi.... Hafla za kichama na serikali wee tupia tuu... Hiyo ni moment yako ya kula bata...

Hata kama uko zako bush umeamua kujitenga ukafurahi na kima mijusi na ngedere.. Tupia kwa raha zako

Usiache kutupia hata kama si tukio lako ni la mwana ama mchuchu

Maisha yetu yamejaa CHANGAMOTO na setbacks kibao.... Ukizishikia stress bango... Zitakumaliza utuache tukichill na vilimbwende vya mzee baba... Kuwa sehemu ya wala bata wa JF.... Onesha wapi upo au ulipokuwa ukichill na pengine hata kula tundi kimaskhara

Jisikie huru kujiachia... Usiendekeze stress na majungu... Vitakumaliza... [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Jr[emoji769]
Niko hapa napata mbege kwanza
 

Attachments

  • FB_IMG_1779124429071.jpg
    FB_IMG_1779124429071.jpg
    103.9 KB · Views: 10
Hivi kula bata ni kula na kunywa mabia tu? Haya kama ni hivyo hilo bata linaliwa kwa msuguri, temboni, tegeta, katoro, nkuhungu, R chuga, na kwingineko tu? Yaani hata kufika hapo Ngorongoro Crater, Dubai, Bahamas, na kwingineko ni shida?
 
Hivi kula bata ni kula na kunywa mabia tu? Haya kama ni hivyo hilo bata linaliwa kwa msuguri, temboni, tegeta, katoro, nkuhungu, R chuga, na kwingineko tu? Yaani hata kufika hapo Ngorongoro Crater, Dubai, Bahamas, na kwingineko ni shida?
Matumizi ni mipango.. Bata ni zaidi ya hivyo .. Ila kuna mikasi nk
Ruksa kuweka ziada sisi tumeweka tuliyoweza na mengine ni ya wengine tumenakili tuu
 
Back
Top Bottom