Wakuu, nimekuja rasmi sasa!

Wakuu, nimekuja rasmi sasa!

Dr sai nini kinasababisha mtu fulani akivaa chochote iwe nguo au viatu, wenzie humwonea wivu na kumteta na wengine huamua kushindananaye kwa wao pia kununua vitu hivyo hata kama haikuwa ktk bajeti zao?
 
Mkuu mtaalam wa afya ya mahusiano
Kwanza nimefurahia uwepo wako mahali hapa
Swali langu je ni nini hupelekea mtu ke kuwavutia zaidi jinsi me walio na umri chini yake, hii imekuwa ikitokea toka shule ya msingi.
 
Dr sai nini kinasababisha mtu fulani akivaa chochote iwe nguo au viatu, wenzie humwonea wivu na kumteta na wengine huamua kushindananaye kwa wao pia kununua vitu hivyo hata kama haikuwa ktk bajeti zao?
Asante mkuu Freed Freed.
Naomba nikujibu swali lako kwa kifupi, kama ifuatavyo:-

1: MWANAMKE.

Kwa upande wa mwanamke, tabia ya WIVU tunaihesabu kuwa ni moja ya nature point yake. Na wivu ndio sababu kubwa ya kujitokeza kwa dhana inayoitwa "kuteta". Sasa usimshangae, kwanini anamuonea mtu fulani wivu kiasi kwamba, anafikia hatua hata ya kumteta!

Na mwisho ifahamike wazi ya kwamba, kila mwanamke ana hisia za asili. Hisia zinazomsukuma kutaka (psychologically) kuwa yeye ndio mwanamke number one kwa UZURI NA MVUTO! Na hisia hizo, ndizo zilizozaa tabia ya kupenda KUSIFIWA NA KUBEMBELEZWA.

Sasa tatizo linakuja, pale anapoona kuna uwezekano wa mtu fulani hasa mwanamke mwenzake, kusifiwa au kukubarika kwa sababu ya kitu fulani......hapo yeye ujiona kama anaibiwa nafasi yake psychologically, hivyo ujikuta akitawaliwa na wivu na hata kufikia hatua ya kuteta au/na kushindana.

2: MWANAUME.

Kwa mwanaume, suala la wivu na kuteta katika muktadha wa mavazi, hiko ni kipimo cha uwepo wa gap katika sehemu ya fikra katika ubongo wake. Na ndio maana hii utaikuta sana kwa wanaume, ambao hawana majukumu yaani muda mwingi wapo idle.

Kwa kweli, tabia ya wivu au/na kuteta katika muktadha huo, sio kitu kizuri hata kidogo kwa mwanaume. Kwa sababu ni sababu moja wapo ya mabadiliko ya hisia fulani mwilini.

Freed Freed, karibu tena mkuu.
 
Dr
Mimi hapa nipo harakaharaka Sana kwenye mambo yangu
Mfano
Kufanya kazi, kutembea, kutongoza mwanamke napenda nimtongoze na anikubalia hapokwa hapo akikataa sihangaiki nae tena
Naweza nikakaa mwezi halafu tena nikamsemesha ikitokea amenikataa nanyuti inakuwa Kama vile cycle

How?
 
Mkuu mtaalam wa afya ya mahusiano
Kwanza nimefurahia uwepo wako mahali hapa
Swali langu je ni nini hupelekea mtu ke kuwavutia zaidi jinsi me walio na umri chini yake, hii imekuwa ikitokea toka shule ya msingi.
Asante mkuu client3,
Swali lako limebeba mada pana takribani 3, ila naomba niende nikakujibu kwa kifupi zaidi. In case hutonielewa au utahitaji msaada zaidi, unaweza kuniona hata private...

Awali ya yote naomba niweke wazi kwamba, sio kitu kibaya kwa mwanamke KUTAMANIWA na mwanaume wa aina yoyote hile. Regardless ni mwa/wanaume wa aina gani. Wawe wakubwa au wadogo kiumri, yote ni sawa. Maana kwa wanaume, hali hiyo ya kutamani mwa/wanawake, ndio msingi mkubwa wa udhihirisho wa uzima wa jinsia yake ya kiume, katika mawanda mapana ya kisaikolojia.

Ila sio kitu kizuri kwa mwanamke, kuwa na tendency ya kutamaniwa zaidi na wanaume, aliowazidi umri. Bad enough, if wanaume hao WAKAWEZA hata kufikia point ya kumtongoza au/na kutoka kabisa na mwanamke huyo, katika uwanja wa mahusiano ya kimapenzi. Maana scenario hiyo, uleta definitions za psychology, ambazo zote uhitimishwa kwa kusema kwamba, "MWANAMKE HUYO, ANA TATIZO".

Moja ya definitions hizo, inapambanua wazi kwamba "Mwanamke aliyopo kwenye scenario hiyo, ni ameshindwa kutumia lugha sahihi ya ulinzi wa jinsia yake".

-Kushindwa kutumia lugha sahihi ya ulinzi wa jinsia yake, ndio kitu gani?.

-Maana yake ni kwamba, inawezekana:-

1: Mwanamke huyo akawa ni mtu wa kujichanganya sana, katika kundi/makundi ya wanaume wa sampuli hiyo.

2: Vilevile, mwanamke huyo amepoteza hali ya KUHESHIMIKA, mbele ya watu hao. Hii huwa inatokana na mambo mengi, ikiwemo mtu husika kuwa na kawaida ya kuongea hasichanya nyingi, mbele ya watu fulani. Au kuyavaa mavazi fulani yasio rafiki wa ustahivu, mbele ya watu hao.

3: Pia, endapo hali hiyo itajitokeza katika mazingira ya kazi. Hilo pia linasimama, kama matokea ya kipimo cha kukosekana kwa udhatiti wa mwanamke huyo, katika mahali pake pa kazi.

Kwa maneno mengine, masuala hayo matatu hapo juu, ndio vyanzo vikuu vya kwanini? Mwanamke anakumbwa na hali ya kutamaniwa au/na kutoka kimapenzi na wanaume, aliowazidi umri.

Karibu client3
 
Asante mkuu MLEVi Mmoja,

Hakika suala la kuwa ant social, lina negative impacts nyingi kuliko positives. Lakini kwa kuwa umesisitiza, ya kuwa unataka kuzijua positive tu......nami, naenda kukuelezea baadhi ya hizo positive kama ifuatavyo:-

Kwanza, ukiwa mtu wa kujitenga sana na watu....unakuwa na uwezekano mkubwa sana wa kuheshimiwa au/na kuogopwa na watu hao. Na hii inatokana na watu kushindwa, kukujua/kukuelewa haswa MLEVi Mmoja ni mtu wa aina gani????

Pili, kutokana na kuwa na hali hiyo ya kuogopwa au/na kuheshimiwa na watu wanaokuzunguka. Itapelekea kuwa na SAUTI YENYE NGUVU, yaani utakuwa unapata usikivu au/na muitikio wa watu wengi, pindi utakapohitaji kuongea au kufanya kitu fulani katika jamii hiyo!

Tatu, unapokuwa ant social zaidi. Kuna uwezekano mkubwa zaidi wa kupunguza asilimia 8% za chronic stress (mawazo tatizo), ambayo binadamu anaweza kuyapata kupitia watu wanaomzunguka. Hapa ni kwamba, hakutakuwa na uwezekana wa kusikia au/na kuwa affected na "nani kakusema hivi au vile"/ " sijui nani kafanya nini...." etc

Mkuu MLEVi Mmoja, naomba kwa leo niishie hapo. Ila nitakuja na uzi murua, utakaodadavua hii mada vizuri, naamini kupitia uzi huo.....dhana ya ant social, itafahamika katika mawanda mapana zaidi. Naomba uendelee kuwa nami, katika nyuzi zijazo.....

KARIBU SANA.
Depal
 
Dr
Mimi hapa nipo harakaharaka Sana kwenye mambo yangu
Mfano
Kufanya kazi, kutembea, kutongoza mwanamke napenda nimtongoze na anikubalia hapokwa hapo akikataa sihangaiki nae tena
Naweza nikakaa mwezi halafu tena nikamsemesha ikitokea amenikataa nanyuti inakuwa Kama vile cycle

How?
Asante mkuu Rhz4567

Hiko ulichonacho, ni matokeo ya kukua kwa FIKRA PAMBAMUZI kwenye ubongo wako. Na kwa kawaida hali hiyo, mara nyingi uwatokea watu wa kuanzia age ya 37's na kuendelea. Ila pia kuna posibility ya case hiyo kujitokeza hata kwa watu, walio chini ya age hiyo....yote itatokana na mazingira aliyokulia huyo mtu.

Hakika, hiko sio kitu kibaya kabisa. Maana kina faida kadha wa kadha. Katika mawanda ya saikolojia, tunakihesabu kuwa ni moja ya mechanism defense ya mwanadamu.

Ni imani yangu, nimelijibu swali lako mkuu Rhz4567. Nakutakia siku njema...

Asante.
 
Mkuu nashukuru sana
Majibu yako murua kabisa hata mimi ningeletewa swali hili ningefikiri kwa namna yako na kujibu hivyohivyo hivyo lakini bahati mbaya sana vigezo hivi havi apply kabisa kwenye hii case na ndio sababu nikalileta kwako nione kama kuna sababu nyingine za kisaikolojia
Asante mkuu client3,
Swali lako limebeba mada pana takribani 3, ila naomba niende nikakujibu kwa kifupi zaidi. In case hutonielewa au utahitaji msaada zaidi, unaweza kuniona hata private...

Awali ya yote naomba niweke wazi kwamba, sio kitu kibaya kwa mwanamke KUTAMANIWA na mwanaume wa aina yoyote hile. Regardless ni mwa/wanaume wa aina gani. Wawe wakubwa au wadogo kiumri, yote ni sawa. Maana kwa wanaume, hali hiyo ya kutamani mwa/wanawake, ndio msingi mkubwa wa udhihirisho wa uzima wa jinsia yake ya kiume, katika mawanda mapana ya kisaikolojia.

Ila sio kitu kizuri kwa mwanamke, kuwa na tendency ya kutamaniwa zaidi na wanaume, aliowazidi umri. Bad enough, if wanaume hao WAKAWEZA hata kufikia point ya kumtongoza au/na kutoka kabisa na mwanamke huyo, katika uwanja wa mahusiano ya kimapenzi. Maana scenario hiyo, uleta definitions za psychology, ambazo zote uhitimishwa kwa kusema kwamba, "MWANAMKE HUYO, ANA TATIZO".

Moja ya definitions hizo, inasema "Mwanamke wa aina hiyo, ni ameshindwa kutumia lugha sahihi ya ulinzi wa jinsia yake".

-Kushindwa kutumia lugha sahihi ya ulinzi wa jinsia yake, ndio kitu gani?.

-Maana yake ni kwamba, inawezekana:-

1: Mwanamke huyo akawa ni mtu wa kujichanganya sana, katika kundi/makundi ya wanaume wa sampuli hiyo.

2: Vilevile, mwanamke huyo amepoteza hali ya KUHESHIMIKA, mbele ya watu hao. Hii huwa inatokana na mtu husika, kuwa na kawaida ya kuongea hasichanya nyingi, mbele ya watu fulani. Au kuyavaa mavazi fulani yasio rafiki na ustahivu, mbele ya watu hao.

3: Pia, endapo hali hiyo itajitokeza katika mazingira ya kazi. Hilo pia linasimama, kama matokea ya kipimo cha kukosekana kwa udhatiti wa mwanamke huyo, katika mahali pake pa kazi.

Kwa maneno mengine, masuala hayo matatu hapo juu, ndio vyanzo vikuu vya kwanini? Mwanamke anakumbwa na hali ya kutamaniwa au/na kutoka kimapenzi na wanaume, aliowazidi umri.

Karibu client3
 
Mkuu nashukuru sana
Majibu yako murua kabisa hata mimi ningeletewa swali hili ningefikiri kwa namna yako na kujibu hivyohivyo hivyo lakini bahati mbaya sana vigezo hivi havi apply kabisa kwenye hii case na ndio sababu nikalileta kwako nione kama kuna sababu nyingine za kisaikolojia
Asante kwa kushukuru mkuu client3.

Ila sijakuelewa kidogo, kuanzia hapa "...lakini bahati mbaya sana vigezo hivi havi apply...."

Tafadhali naomba ufafanuzi wa hapo, kama hautojari.
 
Dr..inakuwaje mdada umri kati ya miaka20- 25 kutongozwa sana na wanaume watu wazima sana sana waliooa wenye familia huku vijana wanamuogopa hawamtongozi .
 
Asante Mkuu Blue G.
Naomba nikujibu kwa kifupi sana maswali yako yote matatu, kama ifuatavyo:-

Kwa kifupi yote hayo yanatokea, kwa sababu ya kukosekana kwa uelewa wa haswa, ni vitu gani mtu anatakiwa avizingatie......kabla ajafanya maamuzi ya kuwa na mtu kimahusiano ya kimapenzi.

Hakika vipo vitu vya msingi, ambavyo mtu anatakiwa avifahamu vizuri....ili viweze kumsaidia kutoka katika scenarios za namna hiyo.

Mkuu Blue G, naomba kwa leo niishie hapo. Ila naomba ufatilie nyuzi zangu zinazofuata.....hakika nitawaletea uzi, utakaoeleza kwa kina vitu hivyo ni vipi?.

Asante.
oh asante sana mkuu ukifungua uzi wowote ule wa kisaikolojia kuhusiana na mahusiaano kwa ujumla naomba usiache kunitag tafadhali.
 
Dr
Mimi hapa nipo harakaharaka Sana kwenye mambo yangu
Mfano
Kufanya kazi, kutembea, kutongoza mwanamke napenda nimtongoze na anikubalia hapokwa hapo akikataa sihangaiki nae tena
Naweza nikakaa mwezi halafu tena nikamsemesha ikitokea amenikataa nanyuti inakuwa Kama vile cycle

How?
Najiona mimi
 
Dr Sai, kwanini ktk jamii yetu mtu akipata anguko ktk nyanja yoyote watu hufurahia sana na kumsema kisirisiri? Mfano kushindwa biashara, kutumbuliwa, kufungwa gerezani, kupata kesi, kutapeliwa nk
 
Dr..inakuwaje mdada umri kati ya miaka20- 25 kutongozwa sana na wanaume watu wazima sana sana waliooa wenye familia huku vijana wanamuogopa hawamtongozi .
Asante mkuu madam cute.
Very sorry kwa kuchelewa kukujibu.....nilikuwa busy kidogo!
Ila naomba nianze sasa kulijibu swali lako, sema nitaomba uniwie radhi kidogo, maana naenda kukujibu kwa kifupi, kama ifuatavyo:-

Awali ya yote naomba niweke bayana, kuwa scenario hiyo haimpati mwanamke pekee. Bali hata kwa upande wa kiume pia scenario hiyo inajitokeza, ingawa sio mara kadha wa kadha.

Kwa mwanamke, scenario hiyo inaanza kujitokeza kuanzia age ya 20 up to 26. Kwa upande wa mwanamke hii scenario, huwa na characteristic ya kuanza kwa kasi, then inaanza kunyong'onyea kadili siku zinavyokatika. Yaani pale inapoanza hapo kwenye age ya 20, huwa inakuwa na kasi sana. Ila kila muda unavyozidi kwenda, ndipo na scenario hiyo inavyozidi kupunguza kasi.....hatimahe upotea kabisa.

Ila kwa upande wa mwanaume, mara nyingi scenario hiyo inaanza kuonekana kuanzia age ya 23 up to 35. Na ina sifa kubwa ya kuanza kwa utaratibu sana, pale inapoanza kwenye hiyo 23. Ila kila muda unavyozidi kwenda, ndipo na scenario hiyo huzidi kukua mara dufu!

Hakika kwa pande zote mbili (mwanamke na mwanaume), scenario hiyo inasababishwa na muunganiko wa matokeo ya masuala mawili makubwa. Masuala hayo ni haya yafuatavyo:-

A. Asili ya kijinsia (biological & intellectual factors).

B. Mfumo wa maisha (personality)

Haya sasa, tuanze kuangalia udadavuliwaji wa masuala hayo sababishi.

A. ASILI YA KIJINSIA.

Hakika hiki ndio kisababishi cha kwanza, kinachopelekea kutokea kwa hiyo scenario. Lakini sababu hii, inatupa hasa jibu la kwanini scenario hiyo ujitokeza zaidi, kwa watu wenye range ya ages hizo tu. Kwa maneno mengine, kisababishi hiki kimejikita zaidi kuonyesha ni kwanini, hiyo scenario inawakumba wanawake wa age 20-26. While wanaume inawakumba, katika age ya 23-35.

-Sasa tukianza na upande wa wanawake, tunaona scenario hiyo inajitokeza kwa sababu ya uwepo wa matokeo chanya ya msingi mkubwa wa kijinsia, ambao tunasema ni BIOLOGICAL ISSUES. Hapa tunaangalia biological factors, zinazomfanya mtu wa jinsia ya kike, kutoka kwenye stage ya utoto na kuingia kwenye room ya kuwa mwanamke kamili. Hakika hapa ndipo mwanamke, anaanza kuwa na mng'ao, ambao unakuwa ni kivutio kikubwa kwa mwanaume yoyote yule. Hivyo ujikuta akiwavutia sana kimapenzi wanaume wengi, wenye sifa tofauti tofauti.

Ila ubaya au uzuri wa biological factors hizo, huwa zina asili ya kunyong'onyea, kila muda unavyoongezeka! Na hii tunaweza hata kuipima, kupitia maumbile ya mwili wa mwanamke. Kwa kawaida maumbile ya mwanamke wa kuanzia age 20's, ni tofauti na ya mwanamke wa age 40's.... Na ndio maana hapo juu tumeona, hata hiyo scenario pia ina sifa ya kupunguza kasi kwa mwanamke, kadili muda unavyozidi kwenda.

-Tukirudi upande wa mwanaume, tunaona scenario hiyo inasababishwa hasa na uwepo wa matokeo chanya ya msingi wa asili ya kijinsia katika INTELLECTUAL ISSUES. Hapa tunaongelea intellectual factors, zinazotuwezesha kupima uwezo wa mtu fulani, katika uwanja wa ufikiriaji na upambanuzi wa masuala mbalimbali. Hakika intellectual factors, ni moja ya factors pia zinazomfanya mtu wa jinsia ya kiume, kutoka kwenye room ya utoto na kuanza kuingia kwenye chapter ya kuwa mwanaume kamili.

-Pia tunaona uzuri au ubaya wa factors hizo, nyingi huwa zina tendency ya kukuza uwezo wa kifikiri wa binadamu. Sasa kwenye upande wa mwanaume pindi tu afikapo age ya kuanzia 23, tunaona uwezo wake wa kufikiri kama mwanaume unaanza kubadilika kitaratibu taratibu kwa kukua. Na hakika kila muda wa siku zinavyozidi kwenda, ndio na yeye anazidi kuimalika zaidi kifikra. Sasa tukiangalia hiki kwa makini, ndipo tunapata hoja ya swali la kwanini, mwanaume anazidi kuwa kivutio kikubwa cha wanawake wengi hasa waliomzidi umri, kadili ya jinsi ya yeye anavyozidi kukuwa kiumri!

B. MFUMO WA MAISHA.

Hapa katika mfumo wa maisha, tunaangali zaidi suala zima la personality. Personality inaweza kupimwa katika mambo kadha wa kadha, ikiwemo mamna mtu anavyoongea, anavyovaa, anavyo show his/her feelings etc. Hakika vipimo hivyo vya personality, ndivyo vinafanya tunasema "fulani anafaa kuwa kiongozi" au "fulani yupo kama kibaka" au "Mtu fulani anajisikia/anaringa" etc. Kwa kifupi, personality ndio kitu kinacho hamua mtu fulani awe na taswira ipi, katika jamii inayomzunguka.

Kwa msingi huo tunaona suala la personality, linaweza kupelekea pia mtu akajikuta anakumbwa na scenario hiyo ya kuogopwa na watu wa rika lake, katika muktadha mzima wa mahusiano ya kimapenzi.

Okay basi twende tukaone, how personality inaweza kuzalisha hiyo scenario. Na hapa nitaenda zaidi kuongea kwa upande wa mwanamke zaidi, kama swali lako mkuu madam cute ulivyouliza.

Kwa kawaida mwanamke akifikwa na shida hiyo, ya kujikuta anaogopwa na wanaume wa rika lake, katika muktadha mzima wa mahusiano ya kimapenzi. Ni wazi mwanamke huyo ana personality kubwa, yaani ana muonekano wa matawi ya juu! Na taswira hiyo ya matawi ya juu, haiishii tu kwenye uzuri alionao. Bali pia inabeba hata namna anavyojiweka, kuanzia kukaa, kutembea, kuongea mpaka kuvaa kwake.

Hivyo vijana wenzake wa jinsia ya kiume au watu wanaolingana naye rika, wanakuwa ni watu wanaovutiwa sana kimapenzi na mwanamke huyo. Na akili mwao wanakiri wazi kwamba, hakika mwanamke huyo ni mzuri. Lakini shida inakuja pale, wanapoangalia personality nzima nzima ya mwanamke huyo husika. Hapo ujikuta psychologically, mwanaume anajivua wadhifa wa kuweza kumpata na kumfanya mlimbwende huyo kuwa mwenza wake, katika ulimwengu mzima wa mahusiano ya kimapenzi. Na hiyo yote inatokana na yale anayo yaona kwa mwanamke huyo. Na mbaya zaidi, endapo mwanaume huyo atakuwa tayari kasha kuwa affected kisaikolojia, juu ya hali yake duni ya kipato aliyo nayo!

Ila tukirudi kuona why watu wazima, ndio wanakuwa na courage ya kumtongoza mwanamke huyo. Hapa tunaona kuna vitu vingi sana, vinavyo build hiyo courage kwa wanaume wa age hizo. Awali ya yote tunaona inachangiwa na experience walizo nazo katika muktadha huo. Vilevile wengi wao wanakuwa na hali ya kujikubali psychologically, kwamba i can.....na hii ni matokeo ya uwezo wa kifedha au kitu fulani alichonacho etc. Hakika ndipo hapo, ile personality ya mwanamke iliyowatia hofu vijana au wanaume wa rika lake, inaposhindwa kutake place kwenye mind za watu hao wazima....

Kwa leo naomba niishie hapo madam cute, in case una swali lolote.....you're welcome!

Asante.
 
oh asante sana mkuu ukifungua uzi wowote ule wa kisaikolojia kuhusiana na mahusiaano kwa ujumla naomba usiache kunitag tafadhali.
Okay, out worry mkuu.

You're welcome...
 
Dr Sai, kwanini ktk jamii yetu mtu akipata anguko ktk nyanja yoyote watu hufurahia sana na kumsema kisirisiri? Mfano kushindwa biashara, kutumbuliwa, kufungwa gerezani, kupata kesi, kutapeliwa nk
Asante mkuu Freed Freed.
Awali ya yote naomba niwie radhi sana, kwa kuchelewa kukujibu. Ila now naenda kukujibu kwa kifupi, kama ifuatavyo:-

Hakika hiko ukionacho ni matokeo ya mambo mengi, baadhi ya mambo hayo ni kama yafuatavyo:-

1: Ni wazi mtu huyo aliyepata matatizo, alikuwa kwenye USHINDANI. Hakika mtu huyo alikuwa kwenye ushindani wa masuala fulani na watu hao, wanaofurahia anguko lake. Inawezekana alikuwa anajua au akuwa anajuwa, uwepo wa ushindani huo.

Na kimsingi, ubongo wa mwanadamu unaporuhusu hali ya ushindani....ni wazi umeruhusu pia na amabatano lake, ambalo ni wivu. Sasa kawaida ya matokeo ya wivu wa kiushindana, ni furahio la anguko la upande wa mshindani.

2: Pia scenario hiyo, usimama kama matokeo ya MATENDO HASI YA MUATHIRIKA MWENYEWE. Hakika mtu anayekumbwa na hilo tatizo la kuchekwa au/na kusemwa, pindi apatapo anguko. Inawezekana yeye mwenyewe kuwa sababu ya kutokea kwa hayo au scenario hiyo.

Pengine alifanya jambo/mambo karahishi kwa wanaomzunguka, either kwa kujua au kutokulijua hilo. Then aliowafanyia hivyo walishindwa kuonyesha hisia zao za kukarahishwa (maumivu). May be walikosa muda sahihi wa kuonyesha hilo, au walishindwa tu kufanya hivyo kutokana na nafasi ya mtu huyo aliyetoa karaishi, kuwa ya muhimu na heshima katika maisha yao. Sasa inapotokea anguko kwa mtu wa aina hiyo, direct watu hao ndipo wanapopatia pakutolea zile sumu zao za kukalarahishwa. Sasa, sumu hizo zinatolewa vipi?. Jibu ni kwamba, zinatolewa kwa kumsema na kuchekelea hilo anguko!

3: Pia suala hilo linatokana na matokeo ya watu kuwa na MUDA MWINGI WA ZIADA (relaxation), katika maisha yao mazima ya kila siku.

Kwa kawaida, ubongo wa mwanadamu unapokuwa una kaa bila mshughurisho wa ile hali ya waza wazua.....huwa unakuwa na sifa kubwa ya kumfanya mwanadamu huyo, kuwa ni kiumbe aliye kosa utulivu. Maana shughuri za kiubongo ndio kitu pekee, chenye asilimia kubwa ya kuzalisha hali ya utulivu kwa mwanadamu. Na kipimo kikubwa cha uwepo wa utulivu huo, ni mtu huyo kutokuwa mtu wa kuongea ongea.....yaani atalazimika kuongea pale tu inapobidi. Sasa endapo mtu atakosa utulivu huo, direct inaenda kuwa vice vesa. Normally atakuwa ni mtu wa kuongea lolote lile, linalopita kwenye mboni za macho yake.....regardless yanamuhusu au lah!

Note:
Makundi yote matatu ya hoja hapo juu, yanawahusisha tu wale watu walio karibu nawe, inawezekana wakawa ni ndugu/jamaa/marafiki. Na huu ndio msingi wa kwanini, wanakusema na kukucheka KISIRISIRI, pindi upatapo anguko.

Kwa maneno mengine ni kwamba, still wanakukubali na hawataki kukupoteza katika maisha yao, ndio maana hawakucheki na kukusema PUBLICLY.

Mkuu Freed Freed, naomba niishie hapo kwa leo.

You're welcome....
 
Back
Top Bottom