Wakuu, hii mnaionaje?

Wakuu, hii mnaionaje?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
37,154
Reaction score
55,648
Bosi akiwa mwanamke, wafanyakazi wakiume na wengineo wanakuwa wanamuita mama, badala ya kumpa heshima yake kwa kumuita bosi; ila bosi akiwa wakiume, ataitwa bosi na si kuitwa baba.

Kwa mtazamo wangu, mi naona hawa wanaoleta mahusiano ya kuitana mama katika maeneo ya kazi, huku wamama zao wazazi wakiwa huko kwingineko inakuwa haina tija, zaidi ya kutafuta huruma katika utendaji wa kazi; au inawezekana wakawa ni 'incompetent' wakitegemea kuishi kazini kwa huruma ya bosi wao.

Wakuu, hii mnaionaje?
 
Kwanza ni dharau na kumshusha bosi husika kimamlaka yaani ni dairekti meseji kwamba yeye ni mama na sio boss,Mama ni nyumbani kwake kwa wanae akiwa ofisini ni kiongozi aka madam boss 🙏
 
Bosi akiwa mwanamke, wafanyakazi wakiume na wengineo wanakuwa wanamuita mama, badala ya kumpa heshima yake kwa kumuita bosi; ila bosi akiwa wakiume, ataitwa bosi na si kuitwa baba.

Kwa mtazamo wangu, mi naona hawa wanaoleta mahusiano ya kuitana mama katika maeneo ya kazi, huku wamama zao wazazi wakiwa huko kwingineko inakuwa haina tija, zaidi ya kutafuta huruma katika utendaji wa kazi; au inawezekana wakawa ni 'incompetent' wakitegemea kuishi kazini kwa huruma ya bosi wao.

Wakuu, hii mnaionaje?
Mama yupo kazini...mi nachekaga tu🥸
 
Nyieee
Kumuita mtu boss sio kazi nyepesi..

Yan ED pekee ndio namuita Mkurugenzi.
Waliobaki ni mama, dada, na kuna mama boss mmoja namuita madam/ mama

Wa size tumezoea kuitana dear/ jina lake

Kuna baba mtu mzima namuita mkwe/ docta sbb ni dokta.
 
Sababu hata Mungu alivowaza kuumba mwanadam alimuumba mwanaume peke yake badae akabadili mawazo na kumuongezea mtu sababu aliona ana upweke akamfanyia msaidizi
Dunia ni ya wanaume
No women no cry
 
Mama ni cheo kikubwa sana lakini pia ni mlezi wa familia nzima hana mipaka.

Uboss unamipaka yake.sijui umenielewa mkuu
 
Bos kwa kizungu anaitwa " Mom' au "Madam". Kiswahili chake ni "Mama" Acha kuwaza sana

Wamarekan sometimes wanaita "maam" au "mam". Simple haimanishi mama wa nyumbani. .
 
Nyieee
Kumuita mtu boss sio kazi nyepesi..

Yan ED pekee ndio namuita Mkurugenzi.
Waliobaki ni mama, dada, na kuna mama boss mmoja namuita madam/ mama

Wa size tumezoea kuitana dear/ jina lake

Kuna baba mtu mzima namuita mkwe/ docta sbb ni dokta.
Kwetu ni mwendo wa majina tu muda hautoshi.

Hii idara inakuwa na utaratibu wa kimataifa snaa😃😃hatari tupu
 
Kwakweli Kwa upande wangu ni hapana.
Sir,Ma’am na majina husika.
Na hiyo Sir sijui makitu gani huko ni ya kutafuta kwa tochi sana
Kwetu sisi kawaida labda sabab ya setting pia kuitwa chief kuita mtu chief ni rahisi na vizuri zaid tunatumia prefix za professional basi haina shida
 
Bos kwa kizungu anaitwa " Mom' au "Madam". Kiswahili chake ni "Mama" Acha kuwaza sana

Wamarekan sometimes wanaita "maam" au "mam". Simple haimanishi mama wa nyumbani. .
Kuna kitu nilitaka kuandika 😃😃

📌📌📌📌🤸‍♀️🤸‍♀️🤸‍♀️
 
Hamuitani da flani kwa aliyekuzidi sana af ana cheo?
Dada hiyo vipi shooo…hakunaga hiyo kitu.

Walionizidi vyeo na umri ni wengi mno lakini ni mwendo wa majina.

Labda Director nitaiweka Sir au Ma’am

Huku tunakuwaga na ulimwengu wetu🤓🤓
 
Kuna Mama mmoja ana Kampuni yake lakini hupendelea wafanyakazi wake kumwita Mama na siyo Bosi.
 
Bosi akiwa mwanamke, wafanyakazi wakiume na wengineo wanakuwa wanamuita mama, badala ya kumpa heshima yake kwa kumuita bosi; ila bosi akiwa wakiume, ataitwa bosi na si kuitwa baba.

Kwa mtazamo wangu, mi naona hawa wanaoleta mahusiano ya kuitana mama katika maeneo ya kazi, huku wamama zao wazazi wakiwa huko kwingineko inakuwa haina tija, zaidi ya kutafuta huruma katika utendaji wa kazi; au inawezekana wakawa ni 'incompetent' wakitegemea kuishi kazini kwa huruma ya bosi wao.

Wakuu, hii mnaionaje?
Mtu akiitwa mama , wewe inakuuma nini au na wewe unataka kuitwa mama ?
 
Back
Top Bottom