Wakulima wagomea bei ya Korosho

Wakulima wagomea bei ya Korosho

Bwana yule alitengeneza kizazai Cha kusifu nakupongeza kuliko empire yoyote hapa Duniani.

Aliwaaminisha wafuasi wake , kua yeye ndie masihi wa kuokoa kizazi Chao. wale watakao fuatia baada yake watakua Manabii wa uongo hivyo wapingwe kwa jina la lake.

Wale wote watakao kanisha uongo hao watakua wameuza utu wao kwa ma beberu.

Vumilia ,wanafunzi walimpenda Mwalim wao na wameanua kuyaishi Yale yote alio wafundisha, Huku wakitegemea kuungana nae kuongoza Taifa la Maraika.
Hapo ulipo nsonyo wote upo wazi, wageni wanapita tu
 
Wakulima wa Korosho watendewe HAKI.
Nani awatende haki.???

Waziri kaja na pdf ndefu ya bei kwa nchi zingine zinazozalisha korosho afrika zikiwa low price compare na tz ili kuwaaminisha kuwa wanakataa bei nzuri.

Naona wamewageuza wakulima matoy.

#MaendeleoHayanaChama
 
1
IMG-20221025-WA0045.jpg
 
Mshtuko umewakuta wakulima baada ya Kuletewa bei ya Tsh 1680 kabla ya makato ambapo baada ya makato huenda mkulima ikamfikia 1380, Zoezi hilo la mauzo ya Korosho liliendeshwa wilayani Tandahimba katika kijiji cha Mitondi.

Wakulima wamegomea bei hiyo hivyo korosho hazijauzwa leo.
Mama anaupiga mwingi hadi unamwagika
 
Mbona mkulima wa mahindi naye anauza gunia 70,000 wakati kipindi cha Magufuli aliuza hadi 10,000

Bei za mazao zinaamuliwa na soko sio Rais, acheni uzezeta
Kijana kuna siku utakuja jua huna akili na hujui nini kinaendelea dunia bii, wakati wa. Mheshimiwa mahindi yalizuiliwa kutoka nje ili yatumike hapa ndani ndio maana yalikuwa hayapandi bei na sababu ni mazao ya chakula na hii ilikuwa faida kwa taifa fara wewe
 
kijana kuna siku utakuja jua huna akili na hujui nn kinaendelea dunia bii, wakati wa. Mheshimiwa mahindi yalizuiliwa kutoka nje ili yatumuke hapa ndani nndio maan yalikuw hayapand bei na sabb ni mazai ya chakul na hii ilikuw faida kwa taifa fara wewe
Wewe ni bumunda, hujui lolote, kama huwezi kununua kalime
 
Sijui haya maelezo yako unayatoa kama sarcasm au unamaanisha kweli

Magufuli alisema waziri mkuu atafute wanunuzi watakaonunua kwa bei isiyopungua 3000, waziri mkuu akapata makampuni kadhaa ambayo yangetoa bei hiyo ya juu ya 3000 kidogo, yakatoa bei zao kama vile 3080, 3,100 n.k

Magufuli akakataa akasema bei hizo ni za chini mno akafoka vibaya, akasema serikali ndio utanunua hizo korosho na jeshi ndio litabangua hata kwa mabomu, mwisho wa siku naye akaja kutoa ofa ya 3000 kwa wakulima na zaidi ya nusu ya watu hawakulipwa sababu waliambiwa ni walanguzi (kangomba) na hata hao waliolipwa ni wachache sana walilipwa kwa bei ya 3000, wengi walilipwa kwa bei ya 2600

Mwisho wa siku jeshi halikuweza kubangua zile korosho kwa mabomu na zilikosa wanunuzi na tetesi ni kuwa zilitupwa baharini
 

8 October 2022​

Dodoma, Tanzania

BODI YA KOROSHO TANZANIA YATOA MWONGOZO WA USIMAMIZI WA MASOKO NA MAUZO​


BODI ya Korosho Tanzania ikishirikiana na Bodi ya Usimamizi wa stakabadhi za ghala na Tume ya Maendeleo ya Ushirika zimeandaa na kutoa Mwongozo wa Pamoja wa Usimamizi wa Masoko na Mauzo ya korosho ghafi kwa msimu 2022/2023.

Hayo yalisemwa leo jijini Dodoma na Kaimu Mkurugenzi wa bodi ya korosho Tanzania Francis Alfred Wakati qkitoa taarifa ya utekekezaji wa Shughuli za bodi hiyo kwa mwaka 2021/2022.

Alisema Bodi ya Korosho imetoa miongozo mingine ambayo ni mwongozo wa usimamizi na udhibiti ubora wa korosho pamoja na Mwongozo wa upatikanaji wa korosho ghafi kwa wabanguaji wa ndani kupitia soko la awali kwa msimu 2022/2023.

" Miongozo yote mitatu tayari imesambazwa kwa Sekretarieti za Mikoa, Vyama vikuu vya Ushirika, Waendesha ghala, wanunuzi na wadau wengine katika mnyororo wa zao la korosho. Aidha miongozo hii inapatikana katika tovuti ya Bodi ya korosho ambayo ni www.cashew.go.tz,"alisema

Na kuongeza "Bodi tayari imeanza kusajili na kutoa leseni kwa wanunuzi wa korosho ghafi kwa ajili ya kusafirisha nje ya nchi na kubangua nchini ambapo hadi kufikia tarehe 07 Oktoba, 2022, jumla ya kampuni 48 zimejisajili na kati yake, kampuni 18 tayari zimepata leseni na zilizosalia zipo katika hatua mbalimbali za kukamilisha upataji wa leseni," Alisema Mkurugenzi huyo.

Alibainisha kwa Upande wa minada ya mauzo ya korosho inatarajia kuanza tarehe 14 Oktoba, 2022 kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani.

Aidha bodi inatoa rai kwa Vyama Vikuu vya Ushirika kuhakikisha maghala ya vyama vya msingi yanaanza kupokea korosho za wakulima na ghala za minada ambazo tayari zimepata leseni kufungua ghala kwa ajili ya kuhifadhi korosho hizo, tayari kwa mauzo.

Alisema bodi itaendelea kushirikiana na wadau wote katika mnyororo wa zao la korosho kuhakikisha mkulima anazalisha na kuuza korosho zake kwa tija kwa maendeleo ya tasnia ya korosho nchin

Hata hivyo Bodi ya Korosho Tanzania imekasimiwa jukumu la kusimamia maendeleo ya zao la korosho katika ngazi zote za uzalishaji, ubanguaji/usindikaji, masoko na utafiti ili kuhakikisha kuwa zao la korosho linatoa mchango wake katika kuinua pato la mwananchi na Taifa kwa ujumla.
hotuba zenu za hovyo hatuzitaki na hazisaidii
 
"...Nyinyi hamjajua tu mambo yamebadilika.." JPM kikao na wafanya biashara wa Korosho juu ya bodi 2018
 
12 November 2022



Wakulima wa korosho mkoani Mtwara wamekubali kuuza korosho zilizokusanywa wiki hii zaidi ya tani 10,000 kupitia minada ya korosho iliyofanyika wilayani Newala na Mtwara kwa bei ya juu ya shilingi 2,012 na bei ya chini shilingi 1,850 huku tani 900 zikisalia ghalani baada ya baadhi ya wakulima kukataa kuuza kwa bei hizo

Source : Azam TV
 
Wakulima wakorosho sasa wapambane na hali zao..hakuna wakuwatetea..viongozi wao ndio madalali wa korosho.

#MaendeleoHayanaChama
 
US$ 14.78 kwa gramu 850gms ya korosho katika supermarket za America ya Kaskazini. Sawa na shilingi 33,994 za Tanzania (US $1 = Tshs 2,330) kwa gramu 850. Kilo moja ni gramu 1,000. Mkulima anauza korosho ghafi gramu 1,000 kwa shilingi?

View attachment 2394175

Tujiulize kwanini korosho iliyosindikwa na unauzwa ktk supermarkets na maduka ya walaji bei huwa haishuki ipo palepale lakini bei ya korosho ghafi huwa inaporomoka na kupanda.

Nini kifanyike ili Bodi ya Korosho Tanzania iweze kuhakikisha wakulima bei wanayoipata 'haiporomoki' kama ilivyo kwa walaji wa korosho zilizosindikwa na kutiwa ktk vifungashio bei huwa juu kila siku ktk soko la ndani na nje ya Tanzania.

Korosho za Tanzania hatimaye zapigiwa chapuo Marekani,



More info :
The eight-tonne cargo of processed cashew nuts was dispatched to New Orleans, Louisiana USA

WHT President Godfrey Simbeye described the occasion as a “historic moment of cashew nuts grown, harvested, and consumer-packaged in Tanzania being exported directly for the first time from farmers in Tanzania to the US marketplace”.
 
Wakulima wakorosho sasa wapambane na hali zao..hakuna wakuwatetea..viongozi wao ndio madalali wa korosho.

#MaendeleoHayanaChama
Aliyaharibu hilo zao ni MAGUFULI, wanunuzi wameopt kwenda nchi kama Togo, Msumbiji nk TZ wanasema hakuna uhakika wa biashara maana serikali inaingilia na hiwa na sera ambazo hazieleweki na hubadirika kutokana na Rais aliyepo madarakani
 
Back
Top Bottom