Wakulima wagomea bei ya Korosho

Wakulima wagomea bei ya Korosho

Korosho ndio inaenda kudidimia..nchi ya walamba asali hii sasahivi wamejipanga kumnyonya mkulima..ukute bei ni kubwa tu huko kwenye masoko ta nje.

Ila wao wanawapanga wafanyabiashara kisha wanaenda kuuza kwa faida kubwa.

#MaendeleoHayanaChama
Duh we acha tu ndugu
 
Jinsi nilivyo na hasira Leo haielezeki.
Hivi wanajua vurumai la kulima korosho lilivyo!?.
Huku vijijini watu wanajua Rais ndo mwenye kosa, na katika hili Rais Ana kazi nzito kwa hii mikoa ya kusini.
Watu hawamuelewi
 
Safi kabisa Mwanauchumi mbobezi.... Haya ungekuja huku Nanyamba au Nanyanga au Mahuta utuhubirie tukuelewe.

Tunachojua wauzao nchi yetu ni ninyi mjionao kuwa wasomi.

Hope unajua vema sasa kwamba ground haukuwa peke yako, na ni sisi kwenye vijiwe vyetu vya kahawa na bao tukumbukao enzi zile.

Kila la heri katika Kulambishwa kwako Asali, tuliao tunatosha hatuhitaji msaada wenu.
Hivi kwa nini mnasema kila anayemkosoa Magufuli analamba asali? Kwa hiyo hakuna mkosoaji wa Magufuli ambaye hakuridhiswa na sera zake bali wote ni maslahi binafsi?
 
Hivi kwa nini mnasema kila anayemkosoa Magufuli analamba asali? Kwa hiyo hakuna mkosoaji wa Magufuli ambaye hakuridhiswa na sera zake bali wote ni maslahi binafsi?
Ukishabikia hoja za walamba Asali nawe tunakuweka kundi moja nao, hata kama nawe uko unapigika na korosho tangu mwezi wa 5, kupogolea, kupiga magugu, kupuliza, kulimia mpaka kuvuna.

Bei ya sasa ukilinganisha na Gharama za Uzalishaji, NI UNYANG'ANYI WA MCHANA KWEUPE. Ajabu wewe mkulima sawa nami unahalalisha kwa hoja za walamba Asali, ETI UCHUMI UMEYUMBA. Mbona bia haipungui bei?

Elimu yetu ni Janga LA Taifa.
 
Upo sahihi kabisa, wachangiaji wengi wanazungumzia swala hili kisiasa na sio katika hali ya uhalisia. Ingewezekana wakulima wangezikataa hizo dawa msimu ujao.
Wanakera Sana haswa Hawa Chawa wa wanasiasa...ulagahai wa kisiasa Ni tatizo kubwa Sana ...Sasa Bei ya 1600 ukitoa matozo yao mkulima atanufaika Nini...
 
Wale watetezi wa wakulima wa korosho akina Nauye..Maembe..Kasimu..Aliyekua mwenyekiti wa bodi Annae wako wapi.

Au ndio zama za walamba asali hizi wanakula kwa urefu wa kamba zao.

#MaendeleoHayanaChama
 
Bei ya sasa ukilinganisha na Gharama za Uzalishaji, NI UNYANG'ANYI WA MCHANA KWEUPE. Ajabu wewe mkulima sawa nami unahalalisha kwa hoja za walamba Asali, ETI UCHUMI UMEYUMBA. Mbona bia haipungui bei?
Mgomo wa Bei inabidi uwe mkubwa.....

Rais na Makamu wake wamekwenda ukanda wa kaskazini Mara Saba Mwanza ,Arusha,Kilimanjaro nk ...

Huku Lindi na Mtwara hakuna alitekanyaga hata Mara moja kutusalimia....

It's unfair....tusilaumiane 2025...
 
Sijui haya maelezo yako unayatoa kama sarcasm au unamaanisha kweli

Magufuli alisema waziri mkuu atafute wanunuzi watakaonunua kwa bei isiyopungua 3000, waziri mkuu akapata makampuni kadhaa ambayo yangetoa bei hiyo ya juu ya 3000 kidogo, yakatoa bei zao kama vile 3080, 3,100 n.k

Magufuli akakataa akasema bei hizo ni za chini mno akafoka vibaya, akasema serikali ndio utanunua hizo korosho na jeshi ndio litabangua hata kwa mabomu, mwisho wa siku naye akaja kutoa ofa ya 3000 kwa wakulima na zaidi ya nusu ya watu hawakulipwa sababu waliambiwa ni walanguzi (kangomba) na hata hao waliolipwa ni wachache sana walilipwa kwa bei ya 3000, wengi walilipwa kwa bei ya 2600

Mwisho wa siku jeshi halikuweza kubangua zile korosho kwa mabomu na zilikosa wanunuzi na tetesi ni kuwa zilitupwa baharini
 
hovyo kabisa... nimekuuliza ulishawahi uza hiyo bei au ulimuona nani kalipwa bei hiyo
Acha upumbavu wa kubisha kila kitu niliuza ndio. Mtu uko mikoa ya kati huko unaleta harakati za kubishia usichokijua
 
Wale watetezi wa wakulima wa korosho akina Nauye..Maembe..Kasimu..Aliyekua mwenyekiti wa bodi Annae wako wapi.

Au ndio zama za walamba asali hizi wanakula kwa urefu wa kamba zao.

#MaendeleoHayanaChama
Hao wote ukimtoa membe ni wahuni na wamemwaga pesa sana kwa vijana ili wawanunulie kangomba hili linajulikana kabisa kwasisi wakazi wa huku kusini hakika apumzike kwa amani JPM
 
Unaniudhi sana kwa kujifanya mtu wa kusini yaani sisi tumechanganyikiwa serikali ipo kimya haitoi kauli yeyote juu ya utata huu halafu wewe unaleta siasa zako za kijuha
We akili huna, Mimi nafanya biashara na pia nna mashamba ya mikorosho huko kusini pamoja na mihogo, huyo jiwe kawafirisi watu wengi kipindi kile
 
Back
Top Bottom