Wakulima tushauriane kampuni zinazouza mbegu bora

X_INTELLIGENCE

JF-Expert Member
Mar 25, 2014
9,667
12,238
Ndugu, jamaa na marafiki zangu habari zenu. Nikiwa mdau na mkeleketwa wa kilimo huwa napata uchungu sana pale mkulima anaponunua mbegu ambayo inamletea mavuno duni, wakulima wanashindwa kuendelea na hii yote ni kutokana na baadhi ya makampuni yanayouza mbegu kutokuwa na uhakika na mbegu zao...makampuni haya husifu mbegu zao na kuzipa ubora ambao haistahiri...utakuta mbegu inasifiwa na kampuni kuwa inahimiri na kutokudhuriwa na magonjwa kumbe ni kinyume...pindi mkulima anaponunua mbegu inaenda kumuangusha na kumrudisha nyuma kwani mazao huwa duni na yenye kushambuliwa kiurahisi na magonjwa...wakulima wengi ni masikini wanazidi kuwa masikini kutokana na ujanja wa haya makampuni yanayouza mbegu feki...
ba6b1ff48506bc29e8481f9b68fc4d74.jpg

Naomba tushauriane juu ya wauzaji wa uhakika wa mbegu....

1.je nini mkulima azingatie pindi anunuapo mbegu...
2.je ni kampuni zipi zenye kuuza mbegu zenye ubora wa hali ya juu?
3.nini mkulima afanye pindi anapouziwa mbegu ambayo haijakizi vigezo¿
4.ni dawa zipi mkulima atumie kabla na baada ya kulima...kutibu ardhi na kuua wadudu hatari wa mazao
39a5110db1642ec740de70c056be3ac9.jpg
 
Watu hawapend jambo zuri wala kuishughulisha akil kwa kitu kinachoweza kuwapa faida,ila ingekua ni uzi wa Wema kaondoka chadema ungekuta replies zaid ya 2k ila jambo la msingi kama hili wanaona wanapoteza muda,,watakuja tu wajuz wa mambo
 
Imekosa wakuchangia
Hahahahahaaa..hili la mbegu aisee ni Tatizo..mi niliingizwa mkenge na consultation ya the so called afisa kilimo akaniambia ninunue mbegu HYBRID ya Kenya... yaani mahindi yalianza kuchanua yakiwa hayajafika hata urefu wa magotini....

Kuna kila haja hawa wataalam waji update maana wanachangia kutuangusha......

Wajuzi mje jamani tunawahitaji mnooooi
 
nadhani balton wako good, ila kufanya kazi na wabongo walio wengi ni changamoto sana bora uwe na pesa ya kutosha upate mbegu zisizo na mfungamano na wabongo
Kama Mbegu zipi mkuu, maana wakati mwingine mbegu huendana na eneo husika..mfano mbegu ya mahindi kuna za nyanda za juu, sijui pwani..

Mfano za mahindi na vitunguu zipi unarecommend?
 
Kama Mbegu zipi mkuu, maana wakati mwingine mbegu huendana na eneo husika..mfano mbegu ya mahindi kuna za nyanda za juu, sijui pwani..

Mfano za mahindi na vitunguu zipi unarecommend?
mkuu Tatiana mie nilikua na horticulture hasa kwenye matikikiti zilifanya vizuri sana ukanda wa pwani ila kwenye mahindi kwa ushauri wangu nenda tanganyika farmers association maana hapo enzi nipo home tulikua tunanunua na hamna ujanja ujanja
 
mkuu Tatiana mie nilikua na horticulture hasa kwenye matikikiti zilifanya vizuri sana ukanda wa pwani ila kwenye mahindi kwa ushauri wangu nenda tanganyika farmers association maana hapo enzi nipo home tulikua tunanunua na hamna ujanja ujanja
Asantee sana,nitawatafuta hawa aisee... maana kuna mbegu zingine sio rafiki hata ukizihudumia vipi hazileti matokeo mazuri
 
Asantee sana,nitawatafuta hawa aisee... maana kuna mbegu zingine sio rafiki hata ukizihudumia vipi hazileti matokeo mazuri
kabisa mkuu, yaani mjini ujanja ujanja tu mpk hasira nadhani wapo mwenge kama sikosei ila pia wapo arusha(i mean balton) ila TFA wapo nadhani nchi nzima
upo kwenye horticulture field mkuu?
 
Kibo seed, tanganyika farmers association, harsho wapo moshi!

Kwa kifupi ukiharibu kwenye mbegu basi jua umeliwa!
 
kabisa mkuu, yaani mjini ujanja ujanja tu mpk hasira nadhani wapo mwenge kama sikosei ila pia wapo arusha(i mean balton) ila TFA wapo nadhani nchi nzima
upo kwenye horticulture field mkuu?
Asantee sana.....msimu ujao nitafanya mabadiliko ya mbegu...

mimi nipo kwenye uzalishaji wa mahindi, karanga,chorizo na vitunguu na ufugaji kuku ndio nimeanza

But nilikuwa nataka pia nilime bamia kidogo
 
Asantee sana.....msimu ujao nitafanya mabadiliko ya mbegu...

mimi nipo kwenye uzalishaji wa mahindi, karanga,chorizo na vitunguu na ufugaji kuku ndio nimeanza

But nilikuwa nataka pia nilime bamia kidogo
hongera mkuu, naomba mwaliko shambani kwako nije kujifunza kilimo cha karanga
 
Back
Top Bottom