Wakulima msipotajirika Awamu ya Rais Samia mjue hamtakuja kutengeneza pesa tena

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,115
49,833

Wakulima mna bahati sana awamu hii ya Rais Samia maana anawapeti peti Kwa Kila Hali Ili mnyanyuke.Rais Samia ndio Malkia wa Sheba wa Kizazi hiki.


1. Ruzuku ya mbolea na pembejeo zingine
2. Kilimo ni biashara na uhakika wa soko
3. Visima vya umwagiliaji Kwa wakulima wadogo
4. Riba nafuu kwenye mabenki isiyozidi Asilimia 9%
5.Kafuta ushuru/import duty kwenye zana za Kilimo kama matrekta
6.Uhakika wa Masoko
7.Anajenga Scheme za Umwagiliaji
8. Anawajengea Cold facilities
9. Anagawa vifaa vya umwagiliaji Kwa njia ya matone
10. Mradi wa BBT Kwa Vijana
11. Amerejesha 8/8 na kuifanya ya Kimataifa ambapo Vitalu vya mafunzo vitajengwa kwenye Viwanja vilovyoteuliwa.
12. Ameanzisha mnada wa Chai Tanzania,hakuna Kupeleka Mombasa.
13. Ameongeza Bajeti ya Kilimo Hadi kufikia Bilioni 970 ,hii ni Historia Kwa Tanzania.


Hayo ni Baadhi tuu kati ya mengi ambayo yamefanyika na yanaendelea kufanyika kwenye sekta ya Kilimo.
---
1691522028258.png

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Kilimo Hussein Bashe, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Gerald Mweli pamoja na Dkt. Hussein Mohammed Omar Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo wakati akikata utepe kuashiria uzinduzi wa ugawaji wa vifaa vya maafisa ugani, trekta kwa wakulima, vifaa vya kutengeneza Vihenge vya chuma kwa Vijana, bei elekezi za mbolea ya ruzuku, mradi wa uchimbaji wa visima pamoja na ugawaji wa vifaa vya mfumo wa umwagiliaji kwa matone katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

My Take
Kiufupi Mama amenishawishi nimeingia kwenye Kilimo baada ya kuki damp awamu ya 5,Sasa hivi Kila zao utakalolima ni hela.
 
Wakulima kukopeshwa zana za Kilimo

Benki ya NMB na Kampuni ya Agricom Africa, wamewahakikishia wakulima nchini, ushirikiano baina ya taasisi hizo ndio mkombozi wa Sekta ya Kilimo, hivyo kuwataka kuchangamkia fursa za mikopo nafuu ya pesa, zana za kilimo hususani matrekta, 'power tillers' na pembejeo ili kufanya kilimo chenye tija.

Hayo yamesemwa katika viwanja vya maonesho ya Kitaifa ya Kilimo ya Nanenane jijini Mbeya na Mkuu wa Kitengo cha Kilimo Biashara wa NMB - Nsolo Mlozi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Agricom Africa, Alex Duffar.

Akizungumza,Mlozi alisema NMB na Agricom wanafahamu kwamba Kilimo cha Tanzania kinahitaji miundombinu, pembejeo na zana bora na za kisasa, eneo ambalo wamejipanga vya kutosha kuwafikia wakulima wote - Bara na Zanzibar, hasa vijana na kinamama ambao ndio nguvu ya Taifa katika kilimo.

Alifafanua zaidi kuwa NMB wana bajeti ya mabilioni ya mikopo na mtandao mpana unaojumuisha matawi 229 kote Tanzania, huku washirika wao Agricom nao wakiwa na matawi zaidi ya 12 kwenye Kanda mbalimbali, hivyo, wana uhakika kuwa wateja wao wanakuwa na Kilimo chenye tija na biashara ya sekta hii kwa ujumla wake itaenda vizuri.
 
RAIS Samia Suluhu amewataka vijana wanaoshiriki programu ya Jenga kesho iliyo Bora (BBT),kuongeza kasi ya unenepeshaji wa ng’ombe kutokana na kuwepo kwa soko kubwa la nyama ndani na nje ya nchi.
-
Rais Samia ametoa wito huo leo Agosti 8,2023 alipotembelea banda la unenepeshaji wa ng’ombe kupitia programu hiyo lililopo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi,kwenye maonesho ya Nanenane viwanja vya John Mwakangale mkoani Mbeya.
-
“Wanangu soko la nyama ni kubwa mno hata wanyama hai kuna kipindi nchi za wenzetu huko wanataka, sasa wanyama wakuja kuwachukua ni hawa walioko kwenye mabanda yetu, lakini pia tuna soko ambalo hatuwezi kulisha mpaka nilizungumza na Waziri wa Zambia nikamwambia tuletee tuchanganye tupeleke kwa pamoja, ili Tanzania isikose hilo soko,”amesema Rais Samia.
-
Amesema wapo vijana wengi wakiwemo waliohitimu mafunzo ya JKT hawana kazi, hivyo programu hiyo ikihamasishwa itawezesha vijana wengi kujiajiri na kuongeza kipato chao na Taifa kwa ujumla na kuwataka vijana wanaoshiriki programu hiyo kutokata tamaa kutokana na changamoto wanazokabiliana nazo wanapotekeleza programu hiyo.
-
Isome zaidi:‘Ongezeni kasi unenepeshaji ng’ombe kuna soko kubwa’ - HabariLeo
-
Imeandaliwa na Shukuru Mgoba, Mbeya
 
Akutukanae hakuchagulii tusi.....

Case Study; Wakulima wa Vanilla Bkb (among others)
 
Akutukanae hakuchagulii tusi.....

Case Study; Wakulima wa Vanilla Bkb (among others)
Hilo zao hakiko kwenye ratiba za serikali,nendeni Kwa Mnkondya.

Mwisho iwaje Uganda na Madagascar bei Iko poa harafu nyie bei ni mbovu?
 
Hilo zao hakiko kwenye ratiba za serikali,nendeni Kwa Mnkondya.
Serikali inapanga ndio mkulime alime au serikali ipange kulingana na nini mkulima amelima au nini kipo sokoni ? Nani yupo kumu-assist nani ?
Mwisho iwaje Uganda na Madagascar bei Iko poa harafu nyie bei ni mbovu?
Nini kazi ya Wizara ?, Kama inajua huko bei ipo juu kwanini isichukue hapa ipeleke huko ?

Haya ya kuwaachia peasants wajitafutie soko ndio kunasababisha watu wakimbizane na soko, Mara mnaawaambia alizeti (eti vita Ukraine) mara Parachichi, mara katani mara Michikichi ilimradi tu mnapiga Siasa na maisha ya watu..., Kwanini msiwasaidie hawa watu wapate soko constant ? Hata kama mtu analima sungwi anendelee kulima Sungwi, sio leo Sungwi kesho zambarau.....
 
Write your reply...BADO SANA
Kazi nzuri
===
Rais Samia Suluhu Hassan amezindua programu ya uchimbaji wa visima kwa ajili ya wakulima wadogo 67,850 kwa nchi nzima vitakavyowezesha hekari 2,7014,000 kufikiwa na mfumo wa umwagiliaji.

Akitoa maelezo kwa Rais Samia katika kilele cha maadhimisho ya sherehe ya wakulima nane nane kwenye viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya, leo Jumanne, Agosti 8, 2023, Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema kila kisima kitakuwa na uwezo wa kuhudumia wakulima 16.

Amesema kisima hicho kitakuwa na tenki la lita 5,000 litakalokuwa limefungwa mfumo wa umeme jua kwa ajili ya ku-pump.
"Pia mkulima atapewa eneo la umwagiliaji la heka 2.5 na mkulima wa kwanza katika program hii anatoka wilayani Mbarali mkoani Mbeya," amesema.

Akizungumzia mradi huo, Rais Samia amempongeza Waziri Bashe kwenye eneo hilo la umwagiliaji maji kwa kufanikiwa kutumia vyanzo mbalimbali ikiwamo skimu za umwagiliaji.

Amesema upo uwezekano wa kutumia maziwa ambayo Mungu ameibariki Tanzania yakatumika pia katika kilimo cha umwagiliaji.
"Tunalo Ziwa Vicktoria, Tanganyika na Nyasa maji yako pale. Tukivuta maji machache kufanyia kilimo haitadhuru samaki waliokuwepo pale wala haitapunguza kina cha maji cha meli kuelea, ni maziwa makubwa Mungu katubariki.

"Angalieni uwezekano wa kutoa maji kumwagilia kwenye mashamba wakulima wavune mara mbili kwa mwaka," amesema.

Ametoa mfano nchi kama Misri inatumia maji ya Mto Nile kuzalisha ngano ambayo imeifanya nchi hiyo kuwa kinara wa uzalishaji wa zao hilo duniani.

"Kuwepo mikataba sijui ya kikanda wenzetu wamefumba macho na masikio. Sisi Mungu katupa maziwa matatu halafu tunatafuta vyanzo vya kumwagilia kilimo! vitumiwe watalaamu wakae ili kilimo chetu kikue zaidi," amesema.
 
Serikali inapanga ndio mkulime alime au serikali ipange kulingana na nini mkulima amelima au nini kipo sokoni ? Nani yupo kumu-assist nani ?

Nini kazi ya Wizara ?, Kama inajua huko bei ipo juu kwanini isichukue hapa ipeleke huko ?

Haya ya kuwaachia peasants wajitafutie soko ndio kunasababisha watu wakimbizane na soko, Mara mnaawaambia alizeti (eti vita Ukraine) mara Parachichi, mara katani mara Michikichi ilimradi tu mnapiga Siasa na maisha ya watu..., Kwanini msiwasaidie hawa watu wapate soko constant ? Hata kama mtu analima sungwi anendelee kulima Sungwi, sio leo Sungwi kesho zambarau.....
Kwa Sasa Serikali ndio inawatafutia masoko na yenyewe pia inanunua.
 
Kilimo cha kwenye karatasini kizuri lakini ukiingia filied ni tofauti.hakuna kipindi kigumu kilimo kama awamu ya sita.mbolea bei juukati ya 70-85kg50wakati hapo kabla miaka miwili iliyopita tulinunua kwa 45-50.Matrkta bei juu kuliko ilivyokuwa hapa awali mfano hp50-70 massey au new holland ambayo ndiyo nzuri inauzwa kuanzia 70milioni hadi 100milioni na vifaa vyake.mkulima mdogo ataweza?Soko la mazao limekufa kwa maagizo ya wanasiasa mara waseme hakuna kuuza nje ya nchi.Serikali imeshindwa kabisa kuwasaidia wananchi kujikwamua na kilimo
 
Wakulima mna bahati sana awamu hii ya Rais Samia maana anawapeti peti Kwa Kila Hali Ili mnyanyuke

1. Ruzuku ya mbolea na pembejeo zingine
2. Kilimo ni biashara na uhakika wa soko
3. Visima vya umwagiliaji Kwa wakulima wadogo
4. Riba nafuu kwenye mabenki isiyozidi Asilimia 9%
5.Kafuta ushuru/import duty kwenye zana za Kilimo kama matrekta
6.Uhakika wa Masoko
7.Anajenga Scheme za Umwagiliaji
8. Anawajengea Cold facilities
9. Anagawa vifaa vya umwagiliaji Kwa njia ya matone
10. Mradi wa BBT Kwa Vijana
11. Amerejesha 8/8 na kuifanya ya Kimataifa ambapo Vitalu vya mafunzo vitajengwa kwenye Viwanja vilovyoteuliwa.
12. Ameanzisha mnada wa Chai Tanzania,hakuna Kupeleka Mombasa.
13. Ameongeza Bajeti ya Kilimo Hadi kufikia Bilioni 970 ,hii ni Historia Kwa Tanzania.

Hayo ni Baadhi tuu kati ya mengi ambayo yamefanyika na yanaendelea kufanyika kwenye sekta ya Kilimo.
---

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Kilimo Hussein Bashe, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Gerald Mweli pamoja na Dkt. Hussein Mohammed Omar Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo wakati akikata utepe kuashiria uzinduzi wa ugawaji wa vifaa vya maafisa ugani, trekta kwa wakulima, vifaa vya kutengeneza Vihenge vya chuma kwa Vijana, bei elekezi za mbolea ya ruzuku, mradi wa uchimbaji wa visima pamoja na ugawaji wa vifaa vya mfumo wa umwagiliaji kwa matone katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

My Take
Kiufupi Mama amenishawishi nimeingia kwenye Kilimo baada ya kuki damp awamu ya 5,Sasa hivi Kila zao utakalolima ni hela.
Asante kwa kutufahamisha
 
Kilimo cha kwenye karatasini kizuri lakini ukiingia filied ni tofauti.hakuna kipindi kigumu kilimo kama awamu ya sita.mbolea bei juukati ya 70-85kg50wakati hapo kabla miaka miwili iliyopita tulinunua kwa 45-50.Matrkta bei juu kuliko ilivyokuwa hapa awali mfano hp50-70 massey au new holland ambayo ndiyo nzuri inauzwa kuanzia 70milioni hadi 100milioni na vifaa vyake.mkulima mdogo ataweza?Soko la mazao limekufa kwa maagizo ya wanasiasa mara waseme hakuna kuuza nje ya nchi.Serikali imeshindwa kabisa kuwasaidia wananchi kujikwamua na kilimo
Wakati mnanunua hizo bei vipi mlikuwa la soko na Mazao? Kilimo kitakuwa Kwa kuwa na guarantee ya soko tuu na sio vinginevyo na hii ndio msisitizo wa Serikali.
 
Vema! Lakini siyo Rais wa kwanza kutoa matumaini mfano wa hayo kwa Watanzani!
Sijui kama yule mzee wa Msoga amemkumbusha, KILIMO KWANZA! Maisha bora kwa kila mtanzania wakati kila kukicha tunaona maisha magumu kwa kila mtanzani.
Pamoja na yote hayo ambayo mheshimiwa Rais ana nia njema kwa Wakulima, asitusahalishe Bandari zetu!
 
Kusema kweli kwenye kilimo SSH, anajitahidi sana, kawapa furaha sana wakulima ila kazi kubwa sana bado inahitajika ili kuboresha kilimo kwenye nchi hii
 
Vema! Lakini siyo Rais wa kwanza kutoa matumaini mfano wa hayo kwa Watanzani!
Sijui kama yule mzee wa Msoga amemkumbusha, KILIMO KWANZA! Maisha bora kwa kila mtanzania wakati kila kukicha tunaona maisha magumu kwa kila mtanzani.
Pamoja na yote hayo ambayo mheshimiwa Rais ana nia njema kwa Wakulima, asitusahalishe Bandari zetu!
Samia sio tuu anawapa matumaini Bali anataka Kilimo kiwatoe watu kwenye umaskini.

Hata JK alikuwa anataka kutumia Kilimo Kwa upana wake kuondoa watu kwenye umaskini kabla ya kuja yule Rais wenu wa Wanyonge ambaye alita muendelee kuwa maskini Ili awatawale vizuri.

Matokeo Yake alivuruga Kilimo na masoko ya mazao.Huwezi India umaskini wa watu bila kuweka Nguvu kwenye sekta ya Kilimo,mifugo na uvuvi ambayo tuna advantage zaidi.
 
Kusema kweli kwenye kilimo SSH, anajitahidi sana, kawapa furaha sana wakulima ila kazi kubwa sana bado inahitajika ili kuboresha kilimo kwenye nchi hii
Samia hana tamaa za madaraka za kijinga kijinga kwamba umuomdoe Waziri ambae anafanya vizuri kwenye sekta husika Kwa vile eti atapata umaarufu zaidi,huu ni utoto na ndio maana hapendi kupanguo hovyo Mawaziri anawapa mda watumie vyema vipawa vyao na kwenye Hili Bashe kajitajidi sana na ashukuru anapata Rais mwelewa na mwezeshaji ilimradi ukenge hoja na mkubaliane matokeo ndicho Rais anataka.
 
Back
Top Bottom