Wako wapi hawa makamanda wa CHADEMA?

Wako wapi hawa makamanda wa CHADEMA?

Mbona kimya sana. hawa Makamanda wako wapi?
1. Mabere Nyaucho Marando
2. Tundu Antipas Mgaiwa Lissu
3. Babu Juma duni Haji
4. Kingunge Ngombale Mwiru
5. Mch. Josephat Gwajima(Mshenga).
6. Lucy Philemon Owenya

mmh kwan siku zote ulikuwa ukiwasikia wapi? Gwajima njoo kanisan jumapili utamsikia.....
 
Lissu pamoja na heshima kubwa aliyojijengea lakini kwa sasa anaonekana kama kanjanja fulani hivi wa siasa.

Toka alivyomkashifu Nyerere na kumtusi Dr.Slaa sina hamu nae!
 
Mbona kimya sana. hawa Makamanda wako wapi?
1. Mabere Nyaucho Marando
2. Tundu Antipas Mgaiwa Lissu
3. Babu Juma duni Haji
4. Kingunge Ngombale Mwiru
5. Mch. Josephat Gwajima(Mshenga).
6. Lucy Philemon Owenya

1. Huyu masikini ni mgonjwa na chama kimetelekeza.
2. Alikuwa akimuonea the Democratic and polite leader Mh Kikwete. Hivi sasa kain fiat msituni, Subutu acheze na Magufuli.
3. Kigeugeu anagoja malipo kutoka kwa Mh. Lowasa.
4. Anatafuta namna ya KUTIMIZA ile ahadi aliyommpa yule Nabii wa kinaigeria, lakini makanisa yoteeee yamemkataa
5. Kavikwa ushungi na anaona album kwani power zake za kufufua maiti zimekosa nguvu.
6??????????? Haijulikani
 
Jecha yuko wapiii..siku hizi simusikii
 
Nadhani Wanapeana Zamu Ya Kuchunga Mifugo Ya Mdhamini wao ndio maana hatuwaoni wala kuwasikia...
 
Mshenga kawabadilishia gia angani juu kwa juu, nanukuu,"Reli ni ile ile, mabehewa ni yale yale lakini kichwa ni tofauti, huyu ndiye rais tuliyekuwa tunamtafuta watz anayesimamia maslahi ya wananchi. ..magufuli piga kazi sisi tunakuombea" mwisho wa kunukuu

Ama kweli kubadili gear angani ni kama kula nyama ya mtu,ukianza huachi.
 
Huyo uliyemtaja Mwishoni usichanganye maigizo yake na mabadiliko. Kwanza taka alizohamasisha Dec 9 hazijazolewa bado

Wew ndo ulikaidi agizo la rais la kufanya usafi. Ungezoa taka zako nchi ingekuwa safi . Shame on u
 
Hao wengine sijui...ila kuhusu Lisu yupo njia panda, amechanganyikiwa....yule aliyejitahidi kumuhubiri na mapovu kuwa ni fisadi amekuja sebuleni kwake.

Kila akibadilisha miwani white hair amejaa tele...anatamani miujiza iliyotekelezwa na Gwajima itekelezwe na kwake ili kila white hair akimuangalia adhanie tu ni Peter Msechu.
 
Back
Top Bottom