Frumence M Kyauke
JF-Expert Member
- Aug 30, 2021
- 630
- 1,245
Ndugu zangu tunakumbuka kuwa Branch na Tala walikua wakichuana sana na kutupa mikopo ya papo kwa hapo kupitia simu yako ya mkononi. Wapo watu wengi walionufaika sana mikopo hiyo kwa namna tofauti. Ilifikia pahala Tala wakatuondokea bila taarifa yeyote ya kueleweka kitendo kilichotuumiza sana tuliokuwa wateja wao. Branch nao mpaka sasa hawaeleweki kuwa wanaotoa mikopo ama lah. Hii ni kwasababu wateja wa Branch waliokuwa wamekopa awali, wanadai kuwa kila wanaporejesha mikopo yao basi hawapewi tena wanapojaribu kuomba. Mpaka sasa hatujafahamu nini changamoto kubwa inayo kwamisha kampuni hizi mbili.