Jan-uary
JF-Expert Member
- Dec 7, 2017
- 967
- 1,015
Nimetoka kwenye kikao cha usuluhishi usiku huu, wanandoa wanagombana kisa simu anazopigiwa mwanamke na mzazi mwenzake. Mwanamke kila akijaribu kujitetea Jamaa haelewi, anasema haiwezekani lazima mtakuwa na mahusiano.
Sasa kuna kauli tata imetolewa na bibie ndiyo iliyonisukuma nifungue uzi huu.
Hii hapa - "Shemeji mimi nimechoka, naipenda sana ndoa yangu lakini mume wangu hana imani kabisa na mimi, sina raha kwasababu ya mzazi mwenzangu, naomba Mungu huyu mzazi mwenzangu afe tu ili ndoa yangu iwe na amani, mbona mzazi mwenza wa fulani alishakufa na ndoa yao ina amani.
Nimemwambia Shemeji ukisema hivyo unakosea sana, hiyo hatua uliyofikia kumuombea kifo binadamu mwenzako sio sawa kabisa, kama mumeo hataki upigiwe simu basi mwambie huyo baba nanii asiwe anakupigia,.,.." kabla sijamaliza kanikatisha ,"Hooo hapana Shemeji yaani hata ningekuwa na uwezo wa kumuua ningemuua tu ili nipate amani ya moyo wangu, sina raha.
Nikaona nije kwenu nyinyi mnaojisifia kupasha viporo na wazazi wenzenu, kuna mwenzenu anaplaniwa kuuawa ili kunusuru ndoa, kuweni makini.
Sasa kuna kauli tata imetolewa na bibie ndiyo iliyonisukuma nifungue uzi huu.
Hii hapa - "Shemeji mimi nimechoka, naipenda sana ndoa yangu lakini mume wangu hana imani kabisa na mimi, sina raha kwasababu ya mzazi mwenzangu, naomba Mungu huyu mzazi mwenzangu afe tu ili ndoa yangu iwe na amani, mbona mzazi mwenza wa fulani alishakufa na ndoa yao ina amani.
Nimemwambia Shemeji ukisema hivyo unakosea sana, hiyo hatua uliyofikia kumuombea kifo binadamu mwenzako sio sawa kabisa, kama mumeo hataki upigiwe simu basi mwambie huyo baba nanii asiwe anakupigia,.,.." kabla sijamaliza kanikatisha ,"Hooo hapana Shemeji yaani hata ningekuwa na uwezo wa kumuua ningemuua tu ili nipate amani ya moyo wangu, sina raha.
Nikaona nije kwenu nyinyi mnaojisifia kupasha viporo na wazazi wenzenu, kuna mwenzenu anaplaniwa kuuawa ili kunusuru ndoa, kuweni makini.