Wake zetu na Ma Housegirl

Wake zetu na Ma Housegirl

Watoto bado, tunatarajia(mama kijacho)
bahati yako hayo mabano....
maana nilitaka kuuliza kama hamna watoto hg wa nini?
hongereni na maandalizi mema.
kwa nini anamwamsha dada saa 11 wakati hakuna watoto?
kwani akiamka 12 na nusu hataweza kufanya usafi wa nyumba na kazi nyingine?
Ongea na mkeo, akianza hivi na hivi ni mama kijacho ajiandae kubadilisha hg kila mwezi, na sijui atawapata wapi na siku hizi walivyo mapepe!
 
Ukimaliza kujibu maswali ya FP na HorsePower nami nitaweza kuchangia vizuri.

Ila kwa sasa labda nikusaidie hapo kwenye kuondoa viombo.
Sidhani kama mnafanya vyema kwani hiyo inampasa hata mkeo kuondoa viombo mmalizapo kula sio mpaka House Girl aache kulala eti anasubiria mmalize kula aondoe viombo.
Hebu jaribuni kumfanya kama mwanenu, msimchukulie kama mtu baki, muonyesheni upendo na kumthamini.
Sio kitu kidogo tu, mnagomba wakati ni maswala ya kuelezana taratibu.

Vitendo ni mwalimu mzuri, kuliko kumwambia ajaribu kuwa anakusanya hizo plate na pot anapeleka jikoni mwenyewe. Halafu mnakula saa ngapi? Kanuni za afya na good figure inashauri ulale masaa 4 baada ya kula. So kama mnakula saa 1 jioni na kulala saa 5 bado ni mapema kwa binti ku-clear the table.

Halafu jinsi ya kuongea na mkeo; kama una ndugu wa kike mtumie huyo amshauri na kumuonesha jinsi gani binti anaweza kuondoka kwa maltreatment.
 
Mke mama Kijacho na kuwa na msaidizi wa kazi si jambo baya au kuonesha uvivu. Kinachonikwaza mimi ni namna mke wangu anavyomtreat huyu dada,,,,,,,

Wanawake wakiwa na hali hiyo huwa na hasira sana, yaani kitu kidigo tu kinamkwaza.
Hivyo unapaswa kuizoea hiyo hali.
 
Nina maswali naomba unijibu,
1.Mmeishi bila housegirl kwa muda gani?
2.Mkeo kabla ya kuja housegirl alikuwa akipika na kutoa vyombo au ndio mtu mzima ulikuwa ukifanya kazi hizo?
3.Mkeo anafanya kazi au ni mama wa nyumbani?
Ningeuliza maswali mengi lakini naona yatakuja baadae baada ya kunijibu haya,ila mkuu huwezi achilia hili la mkeo kula na wewe halafu aje kutoa vyombo housegirl maana halina tofauti na kula chakula cha usiku na mkeo halafu shuka aje kufua housegirl,kuwa makini na simama kama mume ndani ya nyumba.

Tumeishi nae sasa ni wiki moja
Mke wangu alikuwa anafanya hizo kazi lakini pia kulikuwa na dada msaidizi aliyekuwa anakuja na kuondoka
Mke wangu ni mama wa nyumbani kwa sasa
 
Labda haujasoma vyema;;

MKE WANGU mambo anayoyafanya kwa dada wa nyumbani yananifanya nisifurahi. Hamtreat vizuri,,,,, Sasa matatizo yangu hapo na mke wangu kunichoka vimetokea wapi??

Endelea kuchunguza utakuja gundua tu, saikolojia ya Wanawake ngumu wakati mwingine kuielewa!
 
Huyu msichana alitafutwa na mama yake mdogo na mke wangu. Huyu ni msichana wa kwanza kuanza kuishi nae ndani ya nyumba, msaidizi wa kwanza alikuwa anakuja na kuondoka na alikuwa na familia(mume na mtoto)

kaka wala usipate shida kabisa kwasasa fanya hivi, kuwa baba mwambie mkeo pembeni kwamba anatakiwa amwone huyo binti kama mwanae na kama inakuwa ngumu basi ni heri aondoke mmbaki wenyewe na kazi ziwe mgongoni kwa mkeo.

hii tabia ya mkeo ni ya baadhi ya akina mama na sipendi niiongelee sana as nitakuwa namsema mkeo kitu ambacho sipendi kabisa ila tu jua kwamba mkeo ni limbukeni wa maisha kwa lugha nyepesi na utapata shida sana usipo jitahd kumrekebisha
 
Vitendo ni mwalimu mzuri, kuliko kumwambia ajaribu kuwa anakusanya hizo plate na pot anapeleka jikoni mwenyewe. Halafu mnakula saa ngapi? Kanuni za afya na good figure inashauri ulale masaa 4 baada ya kula. So kama mnakula saa 1 jioni na kulala saa 5 bado ni mapema kwa binti ku-clear the table.

Halafu jinsi ya kuongea na mkeo; kama una ndugu wa kike mtumie huyo amshauri na kumuonesha jinsi gani binti anaweza kuondoka kwa maltreatment.

Hebu jaribu kuwa na huruma kwa mwana wa mwenzio, huwa sipendelei kabisa kumuona HG anabaki macho mang'amng'am eti kisa Boss wake hajamaliza kula ili yeye aondoe vyombo.

Huwa najiuliza kwani huyo anayekula hawezi kujiondolea vyombo mwenyewe?
Hata kama unamlipa mtu sio kumfanyia hivyo, vitu vingine ni kusaidiana tu.
 
Hebu jaribu kuwa na huruma kwa mwana wa mwenzio, huwa sipendelei kabisa kumuona HG anabaki macho mang'amng'am eti kisa Boss wake hajamaliza kula ili yeye aondoe vyombo.

Huwa najiuliza kwani huyo anayekula hawezi kujiondolea vyombo mwenyewe?
Hata kama unamlipa mtu sio kumfanyia hivyo, vitu vingine ni kusaidiana tu.

I know, ndio maana nikasema kama wanakula mapema sio tu HG ataweza toa vyombo bila kuathiri sleep timetable inayofaa; bali ataweza hata kuviosha na kwenda kulala jiko likiwa safi na kutolazimika kuamka mapema next day.

I do that mimi mwenyewe baada ya kuanza kuishi mwenyewe. Msosi 6:30, vyombo kabla ya saa mbili vimeoshwa, nacheck news nikinywa maji tu kiasi kwamba kesho naamka saa 7:30 na kuwahi job 9:00.
 
Kwanza usijaribu kuchangia au kukosoa jambo lolote kuhusu mfanyakazi mbele yake. Mimi pia niliwahi kupata misukusuko kama hii na wapo walionishauri na tatizo likakoma. Kaa na mkeo umpe uhakika wa namna gani unampenda yeye ili apunguze wivu, pia mweleze kuhusu malezi ya mfanyakazi kwamba awe kama mwanenu kwani bila kufanya hivyo mtabadilisha hadi mataleta na majini ndani. Mfanyakazi wa familia yangu pia katoka IR yaani uwe makini saaaaaaaaaaaaaaaana hawa ndg wana kiburi kilichoambatana na hasira na Visasi, kamwe msidhubutu kumwonya jambo kisha mkaenda kazini, mshauri mkeo awe na timing ya kumwonya yaani ahakikishe yupo full day ili hasira iishe la sivyo hawa watu ni danger sana. Kwa upande mwingine ni Wachapa kazi saaaaaaaaaaaana kama utawalea kama wanao wa kuwazaa.....Hawana tabia ya kujitongozesha kwa waajiri wao ila ukiwatongoza hawajui kukataa pia. Kama baba wa familia hakikisha unaondoa mianya ya kutia laana familia epuka mazoea na maHG
 
kaka wala usipate shida kabisa kwasasa fanya hivi, kuwa baba mwambie mkeo pembeni kwamba anatakiwa amwone huyo binti kama mwanae na kama inakuwa ngumu basi ni heri aondoke mmbaki wenyewe na kazi ziwe mgongoni kwa mkeo.

hii tabia ya mkeo ni ya baadhi ya akina mama na sipendi niiongelee sana as nitakuwa namsema mkeo kitu ambacho sipendi kabisa ila tu jua kwamba mkeo ni limbukeni wa maisha kwa lugha nyepesi na utapata shida sana usipo jitahd kumrekebisha

Ni conclusion yenye maneno makali kidogo, jamaa kasema ni mjamzito huenda mimba ina mchango hapo. Walikuwa wanaishi na mama mtu mzima, sijui kwanini walimtoa au ni matatizo ya huyo bidada?
 
Kwanza usijaribu kuchangia au kukosoa jambo lolote kuhusu mfanyakazi mbele yake. Mimi pia niliwahi kupata misukusuko kama hii na wapo walionishauri na tatizo likakoma. Kaa na mkeo umpe uhakika wa namna gani unampenda yeye ili apunguze wivu, pia mwelezi kuhusu malezi ya mfanyakazi kwamba awe kama mwanenu kwani bila kufanya hivyo mtabadilisha hadi mataleta na majini ndani. Mfanyakazi wa familia yangu pia katoka IR yaani uwe makini saaaaaaaaaaaaaaaana hawa ndg wana kiburi kilichoambatana na hasira na Visasi, kamwe msisubutu kumwonya jambo kisha mkaenda kazini, mshauri mkeo awe na timing ya kumwona yaani ahakikishe yupo full day ili hasira iishe la sivyo hawa watu ni danger sana. Kwa upande mwingine ni Wachapa kazi saaaaaaaaaaaana kama utawalea kama wanao wa kuwazaa.....Hawana tabia ya kujitongozesha kwa waajiri wao ila ukiwatongoza hawajui kukataa pia. Kama baba wa familia hakikisha unaondoa mianya ya kutia laana familia epuka mazoea na maHG

Ushauri mzuri kutoka kwa mhanga.
 
Nawasalim,

Ninadhani hii topic ilishakuja mara kadhaa lakini nashare nanyi hii kitu inayonifanya nikose raha sana nyumbani.

Tuna wiki sasa amekuja msichana mdogo wa kazi kwa ajili ya kusaidia pale nyumbani. Mke wangu anamkosoa huyu dada kwa kila jambo tena kwa ukali. Mara nyingine naona kabisa anamuonea lakini kuingialia hapo ni ugomvi usioisha.

Pia nimegundua mke wangu kama ana pressure hivi kuhusu huyo dada. By the way ni dada mdogo 18yrs ametoka kijijini Iringa, hata kufungua mlango wa fridge alikuwa hajui, amefundishwa siku mbili tatu.

Tatizo hasa kwa akina mama ni nini? Mfano nimemshauri mke wangu amuandalie ratiba ya siku na kazi za kufanya zile fixed. Sababu tunaishi watatu tu kwa sasa, kazi si nyingi. Yeye atamuamsha saa kumi na moja asubuhi na usiku mpaka asubirie tule atoe vyombo ndio akalale!!

Amani imepotea kiasi ndani nyumba. Kwa wenye experience naomba tushirikishane, je ni approach gani nzuri niitumie ili kila mtu awe na amani nyumbani. Amani namaanisha dada wa kazi ajisikie kama mtu anayethaminiwa na mke wangu asione kama mimi nina mawazo mabaya(ngono etc) kwa dada au asione kama nampendelea dada**.


kama mke wako anaweza kufanya kazi zote yeye basi amuondoe tu huyo binti na siyo kumnyanyasa eti anahisi wewe unaweza kufungua mahusiano nae. wewe huna unachoweza kufanya haswa ikizingatiwa kwako unaona mfanyakazi hastahiri manyanyaso. kingine ni kuwa huenda tatizo si kuwa mkeo hakuamini bali amelelewa na kukulia ktk mazingira ambayo mfanya kazi wa ndani ni wa kunyanywaswa. lakini tahadhari kubwa ni kwa kwenu kama mna watoto/ mtoto angalieni kwani manyanyaso yanapozidi hawa wafanya kazi hufanyia kisasi kwa watoto wenu...

ushauri huu mpelekee mke wako:
mwambie aongeze kukupenda akupe mapenzi makali sana, mapenzi ya maji ya moto, nk.. ila yasikuunguze .. ili huyo binti asipate tafsiri nyingine machoni/moyoni pako. sisi tuliokuwa tukiteka maji visimani kwa ndoo za aluminium, ndoo ikitoboka tunatumia udongo kuzima,... tunaziba ndani ya ndoo na siyo nje. mke wako anaziba nje... aahh ndoo inaweza endelea kuvuja
 
Ni conclusion yenye maneno makali kidogo, jamaa kasema ni mjamzito huenda mimba ina mchango hapo. Walikuwa wanaishi na mama mtu mzima, sijui kwanini walimtoa au ni matatizo ya huyo bidada?
am sorry Kaunga ila mimba sio sababu, blv me kuna wanawake wana jeuri sana kama wanakipato na wana ndoa.
nimeshuhudia wengi sana wa aina hii ndio mana nikamwambia ni limbukeni tu. but anisamehe sana kwa maneno yangu.

sjui ni hasira za da sophy yaani ata sijielewi.
 
Last edited by a moderator:
I know, ndio maana nikasema kama wanakula mapema sio tu HG ataweza toa vyombo bila kuathiri sleep timetable inayofaa; bali ataweza hata kuviosha na kwenda kulala jiko likiwa safi na kutolazimika kuamka mapema next day.

I do that mimi mwenyewe baada ya kuanza kuishi mwenyewe. Msosi 6:30, vyombo kabla ya saa mbili vimeoshwa, nacheck news nikinywa maji tu kiasi kwamba kesho naamka saa 7:30 na kuwahi job 9:00.

Labda hapo kidogo umenishawishi.

Ila isiwe ni lazima HG akae kuwasubiria, kama amechoka na anaona hawezi kukaa mpaka mwisho aruhusiwe kupumzika.
Na kama imetokea HG amelala aachwe alale na sio kumuamsha ili aondoe vyombo.
 
njia rahisi kuliko zote muambie mkeo akuachie umfundishe na kumsimamia kazi hgal manake una ufanisi mkubwa zaidi. hapo utauona mtiti wake. mahausigelo ni headache, mie nasaka form 6 failure saahizi manake hata form 4 kanishinda. how on earth does someone fail to remember taka zinawekwa kwe ye dustbin na sio kurusha mlangoni!
 
Mke mama Kijacho na kuwa na msaidizi wa kazi si jambo baya au kuonesha uvivu. Kinachonikwaza mimi ni namna mke wangu anavyomtreat huyu dada,,,,,,,

Kaka tukikuuliza maswali mengi nahisi tunakukosea, cha kufanya kama mwanaume. Ebu angalia ni jinsi gani unaweza ongea na mke wako ili aache tabia ya kufoka. Kwa lugha nyingine mkeo ni mjamzito sishangai sana akibehave hivyo, ila asidishe manjonjo yatamtoka puani. Tell her politely!!
 
Mood swings sa zingine zinawasumbua baadhi ya wadada/wanawake wanapokuwa wajawazito. Nenda taratibu kabla HG hajavuruga hiyo ndoa!
 
Back
Top Bottom