Wake zetu na Ma Housegirl

Wake zetu na Ma Housegirl

Chum Chang hiyo avatar nimeiweka tu sababu ilinipendeza. Niliiona mtandaoni! Nitafurahi kama ukichangia kunipa ushauri ya haya yanayonisibu


Kuna vijimabo alivyjisahau mkeo kuvitekeleza hapo nyumbani sasa woga umemshika anapoona msaidizi wa nyumbani anafanya kazi yake inapotakiwa
Ushauri
Kama mfanyakazi wewe piga mzigo kazini ikiwezekana usipende kurudi mara kwa mara na jaribu kufata ushauri mzuri wa wenzangu waliotanguria pia ikiwa haitosaidia chagua mfanyakazi au mke na usilazimishe kujenga nyumba na tofari la udongo kwenye mapolomoko ya maji
 
Suala la handling ya wadada ni tete na kila mara limekuwa linajitokeza katika sura anuwai.
Kuna familia naifahamu dada na watumishi wengine hawatumii chakula sawa na wana familia. Sijui kwanini wanadamu tunapenda kujisahau hivi!

Muumba huyu huyu angeweza kubadili kibao na ukajikuta wewe mwajiri wa leo ndio mdada ( mwajiriwa).
Mimi naamini ukijiweka katika nafasi ya mdada au mtumishi, utajikuta unakuwa fair . Sio mbaya kugombeza lakini tuwe na kiasi na iwe justified na isigeuke kuwa nagging , eti kisa kwa vile ni mtumishi.
Huwa nasikitika saana kwa kweli maana hawa ni binadamu kama sisi.

Sasa kufungua friji kama mtu hajawahi kuona friji nayo igeuke nongwa? Je mkeo akipelekwa ofisi za NASA huko mambele, naye akaambiwa kufungua mitambo ili mtambo upae sayari ya Mars naye ataweza bila kugombwa? Kila kitu ukijuacho ni relative ujue na sio kuwa kuwa mjini ni nongwa!

Jirani yangu mwingine kwa mwaka hukaa na wasichana 6 hadi 8 ; wastani wa mwezi mmoja na nusu per msichana!

Sielewi asilani. Nilitangulia kusema katika thread fulani kuwa namshukuru Mungu, wangu nimeishi naye mwaka wa 7 huu nikiwa sina watoto na hata sasa nikiwa nimejaliwa watoto. Kwakweli namshukuru Mungu tu kwa yote maana nikisema mengine itakuwa kama kukosa hekima, shukrani na kujisifia.
Mungu atubariki sote na atupe moyo wa mapendo kwa kila mwanadamu kadri tujaliwavyo!
 
Back
Top Bottom