Wake zetu na Ma Housegirl

Wake zetu na Ma Housegirl

Hakika hili ni tatizo kwa wanawake walio wengi kwa wasichana wa kazi, hakika hawatendi haki na wengine utakuta hata huyo anayeitwa ni msichana wa wakazi ni mtoto kweli let say under 13, lakini bado unakuta treatment ni very poor, hawajali kuwa hawa wadada wa kazi wanatunza nyumba na watoto wetu hata kidogo.

Pole, ongea naye mkiwa wawili, mwelimishe atakuelewa.
 
Ni conclusion yenye maneno makali kidogo, jamaa kasema ni mjamzito huenda mimba ina mchango hapo. Walikuwa wanaishi na mama mtu mzima, sijui kwanini walimtoa au ni matatizo ya huyo bidada?

Alikuwa na majukumu mengine zaidi na alikuwa ametoa taarifa muda mrefu tu
 
Nawasalim,

Ninadhani hii topic ilishakuja mara kadhaa lakini nashare nanyi hii kitu inayonifanya nikose raha sana nyumbani.

Tuna wiki sasa amekuja msichana mdogo wa kazi kwa ajili ya kusaidia pale nyumbani. Mke wangu anamkosoa huyu dada kwa kila jambo tena kwa ukali. Mara nyingine naona kabisa anamuonea lakini kuingialia hapo ni ugomvi usioisha.

Pia nimegundua mke wangu kama ana pressure hivi kuhusu huyo dada. By the way ni dada mdogo 18yrs ametoka kijijini Iringa, hata kufungua mlango wa fridge alikuwa hajui, amefundishwa siku mbili tatu.

Tatizo hasa kwa akina mama ni nini? Mfano nimemshauri mke wangu amuandalie ratiba ya siku na kazi za kufanya zile fixed. Sababu tunaishi watatu tu kwa sasa, kazi si nyingi. Yeye atamuamsha saa kumi na moja asubuhi na usiku mpaka asubirie tule atoe vyombo ndio akalale!!

Amani imepotea kiasi ndani nyumba. Kwa wenye experience naomba tushirikishane, je ni approach gani nzuri niitumie ili kila mtu awe na amani nyumbani. Amani namaanisha dada wa kazi ajisikie kama mtu anayethaminiwa na mke wangu asione kama mimi nina mawazo mabaya(ngono etc) kwa dada au asione kama nampendelea dada**.

Pole sana,mimi ni mama pia ongea na mkeo vizuri kwa upole,tena kama baba,mwambie huyo binti ameshikilia maisha yenu mkononi,akihamua anawawapoison wote mnakufa!!yani dada ni mtu wa kumheshimu sana sana,mimi huwa wananisema naendekeza wadada wa kazi,lakini jamani msichana anaweza kuwawekea mavi,mikojo, bleed yake au simu kwenye chakula,yeye akala kiporo,si ndio huwa wadada wanaambiwa pika kingi na kesho mchana usipike! mwelimishe mwambie dada akikarisika anaweza kutuua kwa sumu au akatulisha uchafu!!Halafu mko wawili tu dada wa nini sasa,msiponde honeymoon yenu wenyewe!!!Ok kuwa makini tu unapoongea nae asije kumind maana sisi wa mama kwa kumind ndio wenyewe,ila wewe ndio baba,simamia hilo kama kichwa cha familia.
 
huyo mke ana tabia mbaya tu.inaonyesha na wewe hauna sauti kiivyo.kama ulivyosema mkeo ni mama wa nyumbani,nina uhakika kama ukiwa haupo anamtreat vibaya tu.muwe makini maana ma house girl wengine ukiwa treat vibaya,hasira wanazimalizia kwa mtoto.huyo ni binaadamu
 
Duh kanitumia message sasa hivi kuwa dada kavunja glass kadhaa!!!!! Amemwambia atamkata kwenye mshahara!! Dah narudi tena home kukiwa na drama,,,,,,,,,,,,,
 
Kama hamna mtoto msichana ni wanini?mke wako ni mvivu anamwachia msichana majukumu yake km mke ndo maana anamtreat vibaya akihofia kuchukuliwa nafas yake.we ukimtetea uyo mdada mkeo anajifeel unsecure na ndo atazdi kumchukia muondoe uyo msichana nyumba itakua na aman
 
Ukimaliza kujibu maswali ya FP na HorsePower nami nitaweza kuchangia vizuri.

Ila kwa sasa labda nikusaidie hapo kwenye kuondoa viombo.
Sidhani kama mnafanya vyema kwani hiyo inampasa hata mkeo kuondoa viombo mmalizapo kula sio mpaka House Girl aache kulala eti anasubiria mmalize kula aondoe viombo.
Hebu jaribuni kumfanya kama mwanenu, msimchukulie kama mtu baki, muonyesheni upendo na kumthamini.
Sio kitu kidogo tu, mnagomba wakati ni maswala ya kuelezana taratibu.
Hapo nilipopigia mstari, ndiyo huwa ni feeling zangu siku zote. Yaani housegirl akishafika nyumbani kwangu huwa ni sehemu ya familia na anapewa privilages zote ambazo member wengine wa familia wanapata. Na huwa napenda kama ni kazi kila mmoja ndani ya nyumba afanye sawasawa na wenzake bila kujali ni housegirl au ni ndugu au mtoto.

Kama ilivyo kwa mleta maada, siku za mwanzo wife alikuwa anaonyesha hali ya kutaka kumtreat housegirl kama mtu baki, lakini hivi sasa amebadilika sana na hivi sasa amempeleka housegirl wetu shule na anamlipia ada, and it feels like our own daughter.

Wake zetu siku zote huwa wana wivu wa kipuuzi. The best way, kama baba unatakiwa kuonyesha msimamo usioyumba. Hawezi, kumtreat kama mtoto wake, mrudisheni kwao, umasikini wake usiwe kigezo cha kunyanyaswa.
 
Mke mama Kijacho na kuwa na msaidizi wa kazi si jambo baya au kuonesha uvivu. Kinachonikwaza mimi ni namna mke wangu anavyomtreat huyu dada,,,,,,,
Leo ukirudi home mkiwa chumbani kwenu mwambie mkeo hivi,
Akumbuke yy ni mama kijacho
pia huyo kijacho anakuja kulelewa na huyo dada hapo home, so anatakiwa aishi naye vizuri ili na yeye aje aishi na mtoto wenu vizuri
akiwa anamkaripia , na kumgombeza kila mara, huyo mtoto akija atakuwa anamtesa. tumeshasoma na kuona jinsi hawa wasidizi wanavyowafanya watoto wetu.
Pia mueleweshe kuwa house girl wenu kashika roho zenu akiamua kuwauwa anawauwa wote, maana yeye ndiye anayetayarisha chukula na kila kitu , so anaweza akaweka sumu mkafa wote.
mwambie hupendi huyo dada awepo wakati nyinyi mnakula,mwambie kuna muda unataka kumkiss, au kula tunda na yeye hapo sitting room so msichana anakuzuia awe amelala, kama ni vyombo wewe utatoa, utaona atashtuka na kuanza kutoa yeye hivyo vyombo na kijirekebisha na atakuwa anaongea vizuri na huyo msichana.ONGEA NAYE CHUMBANI NA KWA UTARATIBU SANA, TENA MKIWA KATIKA ROMANTIC .
 
Kama hamna mtoto msichana ni wanini?mke wako ni mvivu anamwachia msichana majukumu yake km mke ndo maana anamtreat vibaya akihofia kuchukuliwa nafas yake.we ukimtetea uyo mdada mkeo anajifeel unsecure na ndo atazdi kumchukia muondoe uyo msichana nyumba itakua na aman

Ni mjamzito ndugu! Ninaona kabisa anastahili kuwa na msaidizi
 
Duh kanitumia message sasa hivi kuwa dada kavunja glass kadhaa!!!!! Amemwambia atamkata kwenye mshahara!! Dah narudi tena home kukiwa na drama,,,,,,,,,,,,,
Uwiiiiiiiiiiiiiiiiii! mwambie asifanye hivyo, ni vibaya huyo pia ni mtoto akifika kwao, asimfanye akaja akatesa huyo mtoto, mwambie anamtengenezea chuki ambayo atakuja ilipizia kwa mtoto.
 
Duh kanitumia message sasa hivi kuwa dada kavunja glass kadhaa!!!!! Amemwambia atamkata kwenye mshahara!! Dah narudi tena home kukiwa na drama,,,,,,,,,,,,,

Mhhhh......Talk to her personally! si vizuri kumtreat lyk that, glass hata yeye anaweza kuvunja au mwanao. can she do that 4 herself?
 
aaaah acha nipite tu mie


experience yangu hg ukimlea kama malaika viroja atakavyokufanyia utajuta kuzaliwa...ila wale wanaotumikishwa kijeshiojeshi ndo wanaodumu.....anyway inawezekana mkeo hajazoea hali ya kuishi 3 ndani ya nyumba in time atazoea... by the way mna watoto? kama hamna hg wa nini? ushauri wa bure usiingilie sekta hiyo la sivyo mkeo anaweza kuhisi anayoyajua mwenyewe halafu ikawa nogwa....
 
Nawasalim,

Ninadhani hii topic ilishakuja mara kadhaa lakini nashare nanyi hii kitu inayonifanya nikose raha sana nyumbani.

Tuna wiki sasa amekuja msichana mdogo wa kazi kwa ajili ya kusaidia pale nyumbani. Mke wangu anamkosoa huyu dada kwa kila jambo tena kwa ukali. Mara nyingine naona kabisa anamuonea lakini kuingialia hapo ni ugomvi usioisha.

Pia nimegundua mke wangu kama ana pressure hivi kuhusu huyo dada. By the way ni dada mdogo 18yrs ametoka kijijini Iringa, hata kufungua mlango wa fridge alikuwa hajui, amefundishwa siku mbili tatu.

Tatizo hasa kwa akina mama ni nini? Mfano nimemshauri mke wangu amuandalie ratiba ya siku na kazi za kufanya zile fixed. Sababu tunaishi watatu tu kwa sasa, kazi si nyingi. Yeye atamuamsha saa kumi na moja asubuhi na usiku mpaka asubirie tule atoe vyombo ndio akalale!!

Amani imepotea kiasi ndani nyumba. Kwa wenye experience naomba tushirikishane, je ni approach gani nzuri niitumie ili kila mtu awe na amani nyumbani. Amani namaanisha dada wa kazi ajisikie kama mtu anayethaminiwa na mke wangu asione kama mimi nina mawazo mabaya(ngono etc) kwa dada au asione kama nampendelea dada**.
Mkuu Tigga Mumba,chukua hatua stahiki haraka. Zungumza kama baba wa familia.Ukichelewa,huyo dada naye ataonesha 'ubinaadamu' wake kwa kufanya kisichotarajiwa. Hii ni kwasababu yeye kama binaadamu ameumbwa na hasira,chuki na visasi.Itafikia wakati,atalipa kisasi cha hata kumdhuru mmoja wenu au wote au mali. Wafanyakazi wa ndani wengi hufanya yasiyovutia baada ya kunyanyaswa na kuteswa kama hivyo.Take care!
 
Last edited by a moderator:
am sorry Kaunga ila mimba sio sababu, blv me kuna wanawake wana jeuri sana kama wanakipato na wana ndoa.
nimeshuhudia wengi sana wa aina hii ndio mana nikamwambia ni limbukeni tu. but anisamehe sana kwa maneno yangu.

sjui ni hasira za da sophy yaani ata sijielewi.

You are right mimba ni sababu tu...............mbona hawafanyi vituko na kiburi kwa mabosi/ waajiri wao???

Ulimbukeni tuu na kujiona maisha wameyapatia...........ukichunguza waeza kuta na background ni pangu pakavu!!!!!!!!
 
Niko home hali ya hewa si nzuri. Nitaongea na mke wangu kwa taratibu..... kweli challenges hizi......
 
Back
Top Bottom