Wakazi wa Ludewa - Njombe wadai wanagongwa mihuri mgongoni kimiujiza

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
IMG-20240101-WA0019.jpg

Wakazi wilaya ya Ludewa mkoani Njombe wamelalamikia kugongwa mihuri kimiujiza katika maeneo ya mgongoni, huku wakielekeza tuhuma hizo kwa baadhi ya wazee wa kijiji cha Kilima hewa.

Wakazi hao wamelazimika kuitisha mkutano maalumu ili kujadili suala hilo ambapo wamesema, awali tatizo hilo liliripotiwa na wakazi wa kata jirani ya Lupingu wilayani humo na baada ya kupigiwa kelele, tatizo hilo lilikoma, lakini hivi sasa limehamia katika kijiji cha Kilima hewa, huku wakiwataka wazee wanaotuhumiwa kurudisha mhuri huo walipoutoa.

Bado wahusika wa matukio ya kugonga watu mihuri kimiujiza, hawajatajwa moja kwa moja, licha ya kwamba wanaohusishwa ni baadhi ya wazee waliosamehewa kufanya shughuli za maendeleo na serikali kutoka na umri wao.

Kiongozi wa wakazi wa kitongoji cha Kilima hewa, Isaya Mwailamula amemwambia Mwandishi wa Habari wa Star TV kuwa mkutano huo umeitishwa maalum kujadili malalamiko ya uwepo wa mihuri ya kimiujiza kwa wakazi wa eneo hilo, baada ya kupokea malalamiko ya mara kwa mara kutoka kwa watu



Chanzo: Star TV
 
Huo muhuri ni ile chapa ya mnyama ant christ 666 au ni kitu kingine? Au ni tatoo tu wanachorwa?
 
View attachment 2859741
Wakazi wilaya ya Ludewa mkoani Njombe wamelalamikia kugongwa mihuri kimiujiza katika maeneo ya mgongoni, huku wakielekeza tuhuma hizo kwa baadhi ya wazee wa kijiji cha Kilima hewa.

Wakazi hao wamelazimika kuitisha mkutano maalumu ili kujadili suala hilo ambapo wamesema, awali tatizo hilo liliripotiwa na wakazi wa kata jirani ya Lupingu wilayani humo na baada ya kupigiwa kelele, tatizo hilo lilikoma, lakini hivi sasa limehamia katika kijiji cha Kilima hewa, huku wakiwataka wazee wanaotuhumiwa kurudisha mhuri huo walipoutoa.

Bado wahusika wa matukio ya kugonga watu mihuri kimiujiza, hawajatajwa moja kwa moja, licha ya kwamba wanaohusishwa ni baadhi ya wazee waliosamehewa kufanya shughuli za maendeleo na serikali kutoka na umri wao.

Kiongozi wa wakazi wa kitongoji cha Kilima hewa, Isaya Mwailamula amemwambia Mwandishi wa Habari wa Star TV kuwa mkutano huo umeitishwa maalum kujadili malalamiko ya uwepo wa mihuri ya kimiujiza kwa wakazi wa eneo hilo, baada ya kupokea malalamiko ya mara kwa mara kutoka kwa watu



Chanzo: Star TV
Mwaka mpya, same struggle. No time to relax.....mchaka mchaka mpaka usingizini
 
Chapa ya mnyama sio ya kuviziana umelala asubuhi unakuta tayari.Wanasema ya mnyama unaenda mwenyewe Kwa utashi wako na akili zako timamu.
Kitabu cha Ufunuo ni Kitabu cha Unabii ujulikanao km Apokalyptiko,Hivyo kinahitaji sana kuelewa nyakati za uandishi,mazingira yake wakati huo na tabia ya mwandishi,otherwise utaingia chaka.Namba 666 imewaingiza chaka watu wengi sana.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom