Naongea haya kwa uchungu mkubwa ,kuhusu wanaume na wakazi wa dar kwa ujumla .
Mnamo mwaka 2013 nilikuja dar kwa mara ya kwanza nikijiunga chuo kikuu UDSM ,
Siku moja majira ya saa 9 mchana nikiwa narudi hosteli za mabibo nilipita maeneo ya SONGAS kwenye mitambo ya umeme, hakika ilikuwa saa 9 kweupe nilikwapuliwa wallet na kunyang'anywa Pesa zangu kiasi cha 50000, nilipiga kelele kuhitaji msaada , lakini wakazi hasa Wanaume wa darisalama waliniangalia tu huku wakinipita na kumuacha yule kibaka akitamba ,..
Iliniuma sana kwani sikuwahi kudhani kwamba Wanaume na wakazi wa dar wapo hivo, nilijiuliza ni uoga au ndio kila mtu na maisha yake, kwamba kila mtu kaja kutafuta.
Niliondoka na kwenda polis kutoa taarifa waje wawakamate wale vibaka . Nilienda kituo cha polis ubungo ndani ya stendi , cha ajabu nao walinipiga dana dana wakitaka hela ndio wakamkamate..
Nikaondoka nikaenda kituo cha polis urafiki
Sikupata msaada.
Nikarudi ubungo mataa nikiwa nimechoka nisielewe tabia za wakazi wa dar.
Bahati nzuri nikakutana na mwanajeshi nikamueleza tukio zima, tukafunga safari hadi kwa hao vibaka , akakamatwa na kunirudishia pesa yangu.
SASA kuna tukio limetokea huko buguruni , kijana mmoja ansjiita Scorpion anachoma watu visu na kupora , mchana kweupe lakini ...wanaume wa dar wanakuacha hawatoi msaada .
Ni juzi amemtoboa mfanyabiashara mmoja macho na kumchoma visu lakini watu walishuhudia na hawakutoa msaada wowote.
Polis wapo siku zote wanajua kuhusu huyu kibaka...
Mpaka vyombo vya habar vimepiga kelele ndio katiwa nguvuni
NINACHOSHANGAA MBONA MIKOANI KUNA USHIRIKIANO TOFAUTI NA HUKU DAR?
HEBU WANAUME NA WAKAZI WA DAR MBADILIKE SOTE NI WATANZANIA