Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 372,753
- 863,651
Siku moja mmasai mmoja ambaye hakuwahi kuvaa chupi, alinunua moja na kuvaa huko huko mnadani alikoenda kufanya biashara yake ya kuuza ng'ombe. Baada ya hapo akala na kunywa kwa furaha na rafiki zake.
Ni wakati wa kurudi nyumbani akashikwa na haja kubwa hivyo akatafuta kichaka cha karibu na kushusha mzigo..kumaliza akaangalia mzigo wake alioshusha hauoni akatimua mbio kali sana mpaka kijijini na kusimulia watu.
Kila mtu aliongea lake kuanzia uchawi mpaka mizimu kuwa ndio walichukua kinyesi chake. Taharuki ilipomwisha akagundua kinyesi chake anacho makalioni kimemganda ndani ya chupi..kumbe wakati anajisaidia hakuvua chupi kwakuwa hayakuwa mazoea yake.
Taifa lolote linapopata taharuki ama sintofahamu yoyote ile basi kitengo huingilia kati tukio zima zima na kulichakachua ili kutoa nafasi taharuki ana sintofahamu husika kufanyiwa kazi bila bugudha.
Hapa kitengo lazima kipotoshe uhalisia, kichepushe mada, kitengeneze hadithi mpya, kitengeneze taharuki ama sintofahamu bandia ili wao wabaki njia kuu huku hadhira ikichepushwa machakani.
Hili si la kulaumu hata kidogo kwakuwa unapotokea mshindo sauti yake huenda mbali na taharuki huwa juu. Kinachoonekana ni vumbi nene na watu kukimbia huko na huko, hapo kila mtu huwaza lwake. Tathmini na kujua nini kilitokea hufanyika baada ya hali kutulia.
Ni katika kipindi hicho cha kukwepeshwa hadhira mambo huwekwa sawa
Ni katika kipindi hicho cha taharuki na sintofahamu, kitengo huwaza na kupanga kabla ya wengine hakuna kulala ni mwendo wa kubadilishiwa santuri tu halafu tufani ikikoma wakiwa tayari wameshadhibiti mshindo. Kifuatacho ni KIMYA KIKUU SANA na sometimes cha KUOGOFYA!
Ni wakati hadhira inapozoea mshtuko wa kishindo ndio huja tangazo lililotazamiwa na wengi BABA FULANI NDIO KAZAA NA BINTI YAKE
Ni wakati wa kurudi nyumbani akashikwa na haja kubwa hivyo akatafuta kichaka cha karibu na kushusha mzigo..kumaliza akaangalia mzigo wake alioshusha hauoni akatimua mbio kali sana mpaka kijijini na kusimulia watu.
Kila mtu aliongea lake kuanzia uchawi mpaka mizimu kuwa ndio walichukua kinyesi chake. Taharuki ilipomwisha akagundua kinyesi chake anacho makalioni kimemganda ndani ya chupi..kumbe wakati anajisaidia hakuvua chupi kwakuwa hayakuwa mazoea yake.
Taifa lolote linapopata taharuki ama sintofahamu yoyote ile basi kitengo huingilia kati tukio zima zima na kulichakachua ili kutoa nafasi taharuki ana sintofahamu husika kufanyiwa kazi bila bugudha.
Hapa kitengo lazima kipotoshe uhalisia, kichepushe mada, kitengeneze hadithi mpya, kitengeneze taharuki ama sintofahamu bandia ili wao wabaki njia kuu huku hadhira ikichepushwa machakani.
Hili si la kulaumu hata kidogo kwakuwa unapotokea mshindo sauti yake huenda mbali na taharuki huwa juu. Kinachoonekana ni vumbi nene na watu kukimbia huko na huko, hapo kila mtu huwaza lwake. Tathmini na kujua nini kilitokea hufanyika baada ya hali kutulia.
Ni katika kipindi hicho cha kukwepeshwa hadhira mambo huwekwa sawa
- Magendo yaliyofanyika
- Miamala ambayo haikupita njia kuu
- Nyeti zilizofutikwa chini
- Chenchi na salio kwenye kibubu
- Wafaidikaji
- Wapigaji
- Wahuni
- Madudu yaliyofanyika
Ni katika kipindi hicho cha taharuki na sintofahamu, kitengo huwaza na kupanga kabla ya wengine hakuna kulala ni mwendo wa kubadilishiwa santuri tu halafu tufani ikikoma wakiwa tayari wameshadhibiti mshindo. Kifuatacho ni KIMYA KIKUU SANA na sometimes cha KUOGOFYA!
Ni wakati hadhira inapozoea mshtuko wa kishindo ndio huja tangazo lililotazamiwa na wengi BABA FULANI NDIO KAZAA NA BINTI YAKE