Wakala wa Vipimo mko wapi? Mabucha ya nyama Chanika yanawapunja wateja

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,765
36,354
Habari!

Siku moja kwa makusudi kabisa nikaamua kuwa mkaksi, nikasema nitanunua nyama kwenye duka(bucha) lenye mizani iliyo kamili kabisa.

Nikaanza duka la kwanza nikakuta upande wa kuwekea mawe kuna jiwe la nusu kg. Nikamuuliza muuzaji, "Hili jiwe la nini ilhali mizani iko free haina nyama" akasema kaweka tu. Nikalitoa hapohapo mzani ukaangukia upande wenye sahani ya kuwekea nyama. Hapa maana yake mzani hauko sawia. Sikununua nyama.

Nikaenda duka la pili, nikakuta kuna jiwe limewekwa upande wa kuwekea mawe huku mzani hauko kwenye upimaji. Nikamuuliza muuzaji hili jiwe la nini ilhali mizani iko free haina nyama akasema kaweka tu kutunza mizani. Nikalitoa hapohapo mzani ukaangukia upande wenye sahani ya kuwekea nyama wakati wa kupima kabla hata hakijawekwa kitu. Nikamwambia huniuzii Mimi nikaenda sehemu nyingine ya tatu.

Nikakutana na mauzauza mengine kidogo, sahani ya kuwekea nyama wakati wa kupima imewekwa mifupa. Na hii sahani mara nyingi wanaiseti upande ambao mnunuzi hasimami ili wakikutilia nyama mifupa iongeze uzito kidogo.

Nikaenda duka la nne nikakutana na mauzauza kama yale ya duka la kwanza na la pili. Nikaenda maduka kadhaa vivyohivyo.

Serikali ipige marufuku hizi mizani za kizamani, pia serikali (Wakala wa Vipimo) wasiishie kukusanya pesa tu kupitia kupiga muhuri mizani bali wafanye kazi yao kuu ya kumlinda mlaji asipunjwe.

Binafsi naona ni heri kununua nyama kwenye mabucha ya kisasa na supermarket ambako hakuna kupunjana. Hawa wauzaji wa mitaani hawana utu, washazoea unyonyaji.
 
Tafuta hela ili uache kulalamika vitu vidogo na usipate maumivu buchaman anapotafuta namna ya kulea wanae kwa kuchukua gram chache tu toka kwako
 
Sasa si wakaiibie serikali yenye mabilioni, iweje waniibie Mimi mteja wao.
Niliwahi kumwambia mmoja wa wauza nyama buchani ni heri waongeze bei kuliko kuuza kilo sh. elfu 7 huku kiuhalisia wanakukupa nyama ya elfu 5
Tafuta hela ili uache kulalamika vitu vidogo na usipate maumivu buchaman anapotafuta namna ya kulea wanae kwa kuchukua gram chache tu toka kwako
 
Sasa hivi wana mbinu nyingine wanafunga celling fan hizi ndogo halafu wanalenga sahani ilipo upepo unasaidia kusukuma sahani chini ukiangalia tayari wamekupiga gram kadhaa
Kumbe hivi vifeni ni kwaajili ya kufanyia ujambazi.
Lol
 
Sio chanika tu ndg,nenda mbagala,tandika na kwny masoko yote ni shida tupu,pia ujanja mwingine wanatumia sumaku,anaweka nyama ukishangaa kidogo tu anapachika sumaku upande wa sahani mzani unalalia upande huo.
 
Dhulma tupu
Sio chanika tu ndg,nenda mbagala,tandika na kwny masoko yote ni shida tupu,pia ujanja mwingine wanatumia sumaku,anaweka nyama ukishangaa kidogo tu anapachika sumaku upande wa sahani mzani unalalia upande huo.
 
Sio chanika tu ndg,nenda mbagala,tandika na kwny masoko yote ni shida tupu,pia ujanja mwingine wanatumia sumaku,anaweka nyama ukishangaa kidogo tu anapachika sumaku upande wa sahani mzani unalalia upande huo.
Ndio maana hayaendelei yanaishi kwa umaskini wa kutupa. Walau wangekuwa wanapunja na kudhulumu hivo wangekuwa na maendeleo.
 
Back
Top Bottom