Wakala wa Shetani

Wakala wa Shetani

Mkuu MziziMkavu jumamosi hiyo iko mbioni tunakusubiri utupie mambo!

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Wakala wa Shetani - 13.....




"Turudini, muda huu ni mbaya mvua inaweza kushuka si mnakumbuka kuna wingu lilitoweka kiajabu huenda likatuulia mbali. Kwanza sehemu hii haina maeneo ya kujificha na kama mvua itashuka kama ya juzi basi sote tutakufa tunajiona."
SASA ENDELEA...

"Basi turudini, maana tumekwenda sana bado kidogo tutaingia kijiji cha jirani, mnakumbuka wale ni mahasimu wetu wakubwa?"
"Haya jamani turudini, lakini bado nina uhakika tumewaacha nyuma."
"Lazima tutawapata kwani hawana sehemu ya kukimbilia."
Walikubaliana kwa pamoja kugeuza, ilikuwa ni ajabu ya Mungu kushindwa kuuvuka ule mti ambao ndipo alipokuwa wamejilaza Ngw'ana Bupilipili na mwanaye.
Wakati wakijadiliana, Ngw'ana Bupilipili huku akitetemeka, alifumba macho na kumuomba Mungu amuokoe na kikombe kile akiwa amemkumbatia mtoto wake na kuomba asilie. Kwani kama angelia angeharibu kila kitu, wakati akiomba huku amemkumbatia mwanaye alijisaidia haja ndogo.
Aliamini kwa kujisaidia kule lazima mikojo ingemuwasha na kumfanya alie na kutoa sauti na kuharibu kila kitu. Aliuweka mkono mdomoni kwa mtoto wake ili akitaka kutoa sauti basi amzibe.
Aliendelea kumlilia Mungu huku akijikabidhi mikononi mwake. Baada ya maombi yaliyochukua zaidi nusu saa alipofumbua macho hakukuta mtu yeyote. Aliamini kwa mara nyingine tena Mungu amemtendea muujiza.
Siku zote aliamini Mungu hutenda muujiza kwa kila amtegemeaye, watu wale kuishia nyuma ya mti aliokuwa amejilaza ulikuwa muujiza mwingine. Alinyanyuka alipokuwa amejilaza na kumbadili nguo mtoto.
Ajabu kubwa baada ya hali ya utulivu mtoto alianza kulia, kila kitu kilichomtokea kilikuwa kikimuonesha maajabu mengine. Mungu alizidi kudhihirisha uwezo wake kwa kumziba kauli mtoto wakati wa matatizo na kumuachia wakati wa hali ilipokuwa shwari.
Alimnyonyesha mtoto wake mpaka akashiba, baada ya kumaliza kumnyonyesha, naye alifungua mzigo wake na kutoa kipande cha muhogo wa kuchemsha kutokana na njaa kali iliyokuwa ikimuuma.
Baada ya kudanganya tumbo, alijikuta akiwa njia panda asijue aende wapi. Alisimama kwa muda akiwa hajui hatima ya maisha yake ya mbele.
Aliamini kilichokuwa kikifuata mbele yake kilikuwa mtihani mzito kuliko uliokuwa umekwisha muda mfupi wa kuokoka katika kinywa cha mauti. Alijiuliza ataishi wapi, atakula nini na nini hatima ya maisha ya mwanaye?
Kichwa kilikuwa kizito kupata jibu na kujikuta akitokwa na machozi huku akizungumza na Mungu wake amuoneshe njia.
Muda ulizidi kukatika asijue nini hatima yake katika mbuga ile ambayo kila muda ilizidi kutisha.
***
Usiku ulipoingia Ngw'ana Bupilipili na mwanaye walijilaza pembeni ya mti ule mkubwa huku akiendelea kumuomba Mungu asishushe mvua kwa vile hawakuwa na sehemu ya kujikinga, pia awalinde na wanyama wakali wapitao usiku.
Mungu aliwalinda na kulala bila tatizo mpaka asubuhi. Siku ya pili Ngw'ana Bupilipili alijinyanyua toka alipokuwa amelala na kumchukua mwanaye aliyekuwa bado yupo kwenye usingizi. Ilibidi waamke alfajiri kutokana na baridi kali na hali ya hewa bado ilikuwa haijapambazuka vizuri kwa wingu kuwa jeusi.
Alimfunga vizuri mwanaye na kuanza safari ya kuelekea kusikojulikana, alivuka mpaka wa kijiji na kuingia kijiji cha jirani. Aliamini huenda jamaa waliokuwa wakimtafuta wakadamka alfajiri kuanza msako upya na kumkuta, kwa hasira ya kupoteza ndugu zao, lazima wangewaua wote.
Baada ya kuamini mwanaye amekaa vizuri kifuani alianza safari ya kuelekea kusikojulikana. Moyoni aliapa kurudi kijijini alipokimbia kwa ajili ya kulipa kisasi. Alitembea mwendo wa saa saba bila kupumzika huku akikwepana na wanyama wakali kama simba, chui na baadhi ya wanyama waliokuwa katika pori lile la kutisha.
Baada ya mwendo mrefu huku akisumbuliwa na njaa na kiu kikali, alijikuta akiishiwa na nguvu na kuamua kujipumzisha chini ya mti mkubwa. Mtoto wake alianza kulia akionesha njaa inamsumbua. Alitoa titi nje na kumuwekea mtoto mdomoni na yeye kujilaza pembeni yake.
Kila mtoto alivyokuwa akiyavuta maziwa ya mama yake kwa nguvu kutokana na njaa ndivyo naye nguvu zilivyokuwa zikimuishia na kumfanya ahisi kizunguzungu kizito. Kiza kinene kilitanda mbele yake, hakujua chochote kilichoendelea.
***
Ngw'ana Bupilipili aliposhtuka alijikuta amelala kwenye kitanda cha chuma kilichokuwa kimetandikwa vizuri. Mkononi kulikuwa na mrija wa kuingizia maji mwilini mwake. Alitulia na kutafakari kwa muda huku akipepesa macho. Baada ya akili yake kutulia aligundua pale ni hospitali.

Itaendelea jumamosi ijayo.....



 
shukran mzizi mkavu nasubilia utapoiendeleza, ubarikiwe sana kwa hichi ulo tuwekea kinaburudisha sana
 
Mzizi, ucfanye masihara bhana: wengine vocha za manati ss wakitia timu humu wakaitaraji uhondo kisha wakakosa utakuwa umewalostisha!
 
daaah MziziMkavu please dont do this to me ooooo...............................
 
Last edited by a moderator:
Eti leo naingia kwa mara ya tano ndo nagundua kuwa Mzizi mbichi alisema mwisho wa episode 13,eti itaendelea jumamosi ijayo....daaaaaaah pouwa ntakuja that day bt pls MZIZI tufikirie hapa katikat ya wk pleaaaaasee.....
 
MziziMkavu jumamosi imeshapita,tunakusubiri huku mkuu.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
kwa staili yako hii ya kusubiri subiri hata utamu unaisha
jms imeshapita mkuu
 
[h=1]Wakala wa Shetani - 14.....[/h]
Ngw'ana Bupilipili aliposhtuka alijikuta amelala kwenye kitanda cha chuma kilichokuwa kimetandikwa vizuri. Mkononi kulikuwa na mrija wa kuingizia maji mwilini mwake. Alitulia na kutafakari kwa muda huku akipepesa macho. Baada ya akili yake kutulia, aligundua pale ni hospitalini.
SASA ENDELEA...

Alishtuka na kuamini mtoto wake anaweza kuwa ameuawa na yeye yupo pale anasubiri kupona ili wanakijiji wakamfungulie mashitaka ya mauaji ya wanakijiji ambao waliuawa na marehemu mumewe.
Aliamini hata kama atajitetea vipi kuwa hakuhusika na mauaji ya wale wanakijiji waliomuua mume wake, bado wasingemwelewa kwa kuamini alishirikiana na mumewe kufanya mauaji.
Alitamani kunyanyuka, ikiwezekana atoroke japo hakujua pale yupo wapi. Alijaribu kujinyanyua alipokuwa amelala lakini mwili nao haukuwa na nguvu, alijirudisha chini na kujilaza. Moyoni hakukubali kushikwa kirahisi namna ile. Lakini bado alikuwa katika kitendawili kizito mwanaye alikuwa wapi.
Alijitahidi kunyanyuka huku moyoni akiapa kupambana na yeyote atakayejitokeza mbele yake. Alijitahidi kujinyanyua na kukaa kitako kisikilizia hali yake.
Wazo lake kubwa ni kutafuta upenyo atoroke hospitalini ili kuikimbia kesi nzito ya mauaji iliyokuwa ikimkabili marehemu mume wake. Kuhusu mwanaye alikuwa amekata tamaa kwa kuamini lazima atakuwa amekwishakufa. Alikaa kitandani mawazo yakiwa mengi huku akivuta pumzi kwa ajili ya kupata nguvu zitakazomfanya atembee peke yake.
Wakati akitaka kuteremka kitandani, alisikia mlango wa chumba alicholala ukifunguliwa. Alirudi kitandani kwa haraka na kujifanya bado hajarudiwa fahamu. Akiwa amefumba macho na kupumua taratibu ili mtu asijue kama ameshaamka, alisikia nyayo za viatu zikisogea alipokuwa amejilaza.
Hakujitikisa, woga ulimjaa na kuanza kutetemeka kwa kuamini wamekuja kumwangalia kama karudiwa na fahamu ili wamkamate. Akiwa bado amefumba macho, alisikia wakizungumza:
"Dokta ina maana hadi sasa atakuwa bado hajarudiwa na fahamu?" Sauti ya kike iliuliza.
"Noo, lazima atakuwa amerudiwa na fahamu, hakuwa na tatizo kubwa, ni njaa na uchovu ndivyo vilivyomfanya awe vile," ilikuwa sauti ya dokta mwenye lafudhi ya kizungu.
"Mbona bado yupo vilevile?"
"Inawezekana kalala, dawa tulizomchanganyia kwenye dripu zina nguvu sana lazima atajisikia vizuri tu, huenda kulala huku ni usingizi na si kupoteza fahamu."
"Sasa dokta kama atapata fahamu ataweza kumnyonyesha mwanaye, maana mtoto yule kila tulichompa amekataa."
Kauli ile ilimshtua Ngw'ana Bupilipili na kuamini kumbe mwanaye bado yupo hai lakini bado alijawa na maswali pale ni wapi na watu wale ni akina nani. Na nini shida yao kwake, lakini kusikia kuwa mwanaye mzima na anahitaji ziwa la mama, aliamini sehemu ile ni salama na kuwa tayari kwa lolote.
Alijipindua na kujifanya kama mtu anayetoka usingizini, kabla hajafumbua macho, alisikia sauti ya kike ikisema.
"Dokta kweli ameamka."
"Hakuwa na tatizo kubwa sana."
"Kwa hiyo dokta?"
"Mpaka sasa hatujajua anatoka wapi na anaelekea wapi, ngoja apate nguvu tutaweza kumuhoji."
Ngw'ana Bupilipili alizidi kutoka mashaka kwa kuamini sehemu ile ni salama ambayo ilimuhifadhi baada ya kumuokota porini. Alifumbua macho na kumuona daktari mzungu aliyekuwa amevaa shati la rangi ya bluu bahari shingoni, alikuwa na kipimo cha mwenendo wa mzunguko wa damu.
Pembeni yake alikuwepo binti mmoja mrembo aliyekuwa ameshikilia faili na kalamu mkononi. Walipomuona amefumbua macho, wote walisogea mpaka kitandani. Daktari alimshika kichwani na kumwambia kwa sauti ya upole.
"Unajisikiaje sasa?"
"Sijambo," alijibu kwa sauti ya chini.
"Pole."
"Asante."
"Unaitwa nani?"
"Salome," alidanganya jina.
"Andika jina hilo," daktari mzungu alimgeukia msaidizi wake na kumweleza aandike jina la mgonjwa.
"Hali ya mwili unaisikiaje?"
"Mmh, uchovu tu na mwili kuishiwa nguvu."
"Okay, nafikiri ukipata chakula utapona kabisa."
"Nitashukuru, mwanangu yupo wapi?"
"Yupo, utaweza kumnyonyesha?" walimuuliza.
"Ndiyo."
"Okay, kamleteni mwanaye."
Baada ya kusema vile, msaidizi alitoka kumfuata mtoto na kubakia daktari mzungu ambaye aliendeleza kumdodosa mgonjwa.
"Eti mama umetokea sehemu gani?"
"Kabla sijakujibu naomba unieleze hapa ni wapi na nimefikaje?"
"Ooh vizuri mama, hapa ni kituo cha watumishi wa kiroho, tupo kwa ajili ya kutoa misaada kwa watu wa maeneo ya karibu kielimu na kiafya.

Itaendelea jumamosi ijayo.
 
Back
Top Bottom