Mpwayungu Village
JF-Expert Member
- Jul 21, 2021
- 14,591
- 31,128
#HABARI Msajili wa vyama vya wafanyakazi na waajiri amebatilisha uamuzi wa wajumbe 18 wa kamati ya utendaji wa taifa wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wa kushinikiza kumsimamisha Katibu wao mkuu Japhet Maganga kuendesha shughuli za taasisi hiyo.
Kufuatia uamuzi huo Rais wa CWT Leah Ulaya amelaani kitendo kilichofanywa na wajumbe hao kwa kukiuka katiba na misingi ya chama na kusema watachukuliwa hatua za kinidhamu.
“Kikao kilichofanyika hakikuwa halali na kilifanya maamuzi batili ambayo hayakuzingatia katiba na kanuni za CWT”. Amesema Ulaya.
#EastAfricaTV
Kufuatia uamuzi huo Rais wa CWT Leah Ulaya amelaani kitendo kilichofanywa na wajumbe hao kwa kukiuka katiba na misingi ya chama na kusema watachukuliwa hatua za kinidhamu.
“Kikao kilichofanyika hakikuwa halali na kilifanya maamuzi batili ambayo hayakuzingatia katiba na kanuni za CWT”. Amesema Ulaya.
#EastAfricaTV