Waitara ampandia Rais Magufuli

Waitara ampandia Rais Magufuli

makufuri na mfaninasha na mtu aliye ingia kwenye ulingo wa ngumi na baada kuona ameshindwa anaanza kuruka salakasi ili aendele kujitafutia mashabiki ingawaje ameshindwa.

ni sawa na makufuli inshu ya viwanda imemshinda ameaumua kuanza kuipindisha sheria ili aendelee kujitafutia washabiki.

na kama kweli yeye makufuli ni dikteta huo udikteta wake auweke kwenye viwanda tuone udikteta wake.
Ha ha mfalme badala ya kujenga viwanda anawakamata wote wanaomwambia kakosea. Aisee najutia kura yangu kwa huyu msukuma sikujua kwa kweli.
 
Rais anawagwaya UKAWA, lakini kwa sababu ya rais huyo huyo UKAWA wameanza kuwagwaya Wananchi , 2020 Magufuli hapigi kampeni.
Kwani vipi? Umeona kuna dalili za kujiuzulu kabla ya muda kwa kuona mambo yanamshinda?
 
Kama kunakitu wanataka kutueleza watumie vyombo vya habari na wabandike matangazo!
 
Witara size yake mi Jerry Slaa, kwa magufuli ni mwendelezo ule ile wa kutaka umaarufu pasipo kuwa maarufu.
Ajaribu kwenye jimbo lake kwanza tuone kama atapata watu wa kumsikiliza, yeye alikutana na upepo wa mabadiliko, asije akajidangannya kuwa ana nguvu za kisiasa Ukonga
 
Tangu wanadamu waishi pamoja kumekuwa na mpishano ambao haukomi. Yaani wewe unaenda mm ninarudi., unalala mimi naamuka. unamaliza mimi naanza. kwa hiyo dunia ni mpishano na hivo hakuna utawala utaodumu milele na kwa kuwa vyama ni vingi kuna siku kutakuwa na mpishano tu! kutokubali ukweli huu ni fujo lakini mpishano uko pale pale.
Kwa sababu hiyo hakuna haja ya hii reaction bali tujiandae kupishana kwa amani!
 
mtakubaliana na yale tuliosema sisi kina gogo la shamba kwamba kama ccm wanaona ni vyema kufanya siasa 2020 wao wakae wasubiri lakini wanaoona waendelee na siasa kuanzia sasa waachwe wafanye maana wote katiba inawaruhusu
 
MWITA Waitara, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Dar es Salaam amesema, marufuku ya vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara nchini inatokana na kukosekana kwa fikra pevu miongoni mwa viongozi, anaandika Regina Mkonde.

Waitara ambaye pia ni Mwenyekiti wa Uongozi Maalum wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Dar es Salaam amesema hayo leo katika kipindi cha ‘Tuongee Asubuhi’ kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha Star TV.

“Anachofanya Rais Magufuli ni kuzuia siasa za CHADEMA ili tusijiimarishe huku yeye akisuka mipango ya CCM kusikika peke yake pia anadhibiti vyombo vya habari vinavyoandika ukweli, hii ni siasa ya kitoto,” amesema na kuongeza;

“Maamuzi yaliyofanyika si ya haki, Magufuli amezuia mikutano ya CHADEMA anaruhusu ya CCM tu, mwanzo alikataza mikutano ya hadhara lakini alipoona chama chake kitahitaji kufanya mikutano akaruhusu wabunge kufanya kwenye maeneo yao, jambo hili si sawa.”

Waitara amesema kuwa inashangaza kuona hata tamko la kuwataka wabunge na madiwani peke yao kufanya siasa katika Kata na Majimbo yao likikiukwa kwa kuwaruhusu viongozi wakuu wa CCM kufanya mikutano lakini viongozi wa upinzani wakizuiliwa.

“Christopher Ole Sendeka ni msemaji wa CCM na siyo Mbunge, amefanya mkutano mkoani Arusha na polisi walimlinda wala hawakumzuia, lakini ukiacha hilo vyama visivyo na wabunge au madiwani vitajijenga vipi na kupata wabunge wapya bila mikutano?” Amehoji.

Katika hatua nyingine, Waitara amesisitiza adhima ya CHADEMA kufanya mikutano na maandamano nchi nzima kuanzia Septemba Mosi mwaka huu ili kupinga viashiria vya udikteta ambavyo vimeanza kuonekana katika serikali ya awamu ya tano.

“Kufanya mikutano ya hadhara ni haki ya kikatiba na kisheria kwa vyama vyote vya siasa, na UKUTA upo pale pale kwasababu hii ni nchi ya vyama vingi, kama CHADEMA hatufanyi mikutano ya maendeleo watuache, waitishe ya kwao na watushitaki kwa wananchi,” amesema.
Hii hata kama ni kweli ni mhimu kuzingatia nidhamu ya namna ya kuiwasilisha kwa mkuu wa kaya.
Enzi za Mtemi(Onyama) kule kwetu kulikuwa na utaratibu ambao ulikuwa hauruhusu mtu ambaye si msaidizi wa Mtemi (Ng'wanangwa) kumkosoa au hata kumjibu moja kwa moja Mtemi bila kupitia kwa msaidizi wake.
Kwa mfano hata kama mtakuwa kwenye msongamano ikatokea Mtemi akakukanyaga kwenye unyayo na akawa hajaondoa mguu wake,hata kama anakuumiza namna gani ni lazing umwambie Msaidizi wa Mtemi kuwa amwambie Mtemi kuwa amekukanyaga ili aondoe mguu wake.(Ng'wanangwa, ng'wilage u onyama onipandaga )
Tofauti ya hapo ukimweleza Mtemi moja kwa moja,japo ni kweli,basi utakiona cha mtemakuni.
Nadhani ndo tunatakiwa kuiga nidhamu hii ya kwetu.
 
Hakuna ukweli wowote nilioambiwa hapo, ukweli tutaujua 2019 na 2020.Waitara akirudi mnikate kidole mimi mkurya mwenzake lakini dalili za kumng'oa zimeshaonekana.

Vipi mmeshaitia hofu tume ya uchaguzi na saa hizi mko mahali mnapanga matokeo yawe vipi ama?
 
Mhe Waitara kaongea hoja za msingi.
Lakini sitashangaa kusikia leo hii au kesho Waitara kama ilivyokuwa kwa Mhe. Lissu na yeye anatafutwa na Kamanda Ciro kwa uchochezi! Nashindwa kupata lugha ya kuzungumzia huu utawala wa John Pombe Magufuli na PM wake Majaliwa Majaliwa! Ni timu mbovu kabisa ambayo haijawahi tokea hapa Tz!

Nasikia hawa jamaa wote ni Waalimu na Waalimu huwa wana sifa moja ya kwamba ni WAELEWA. Lakini hii pair naona ni kinyume chake! Yawezekana ni wale Waalimu walioingia enzi zile kwa utaratibu wa UPE(Ualimu Pasipo Elimu)! Hawa walikuwa ni waalimu waliotokana na kufeli Darasa la 7 kuingizwa kwenye Ualimu.
Pengine kuna haja ya kuchunguza vyeti vyao!
Mkuu Masters na uDr wa mawaziri wa CCM zinaandikwa na watumishi wa serikali pamoja na mimi nimeandika za mawaziri na wakurugenzi si chini ya watano.

Vyuo vinavyowatunuku si wa kweli kwa sababu kama walikuwa kazini walipata wapi muda wa kuhangaikia hizo shahada zao. Nakumbusha Masters za wateuliwa wa Jamaa yake Lisu wengi wao walikuwa watumishi wa CCM jiulize huko CCM kuna vyuo vikuu vinatunuku shahada. Kama kawaida wanatunukiwa tu bila kuwa na merit zo zote ndiyo elimu yetu hiyo.

Naamini Jamaa yake Lissu ni mmoja waliotunukiwa shahada zao wakiwa mezani kwa kulingana na ujinga unaoonyeshwa (Hata kujua katiba ni issue).
 
MWITA Waitara, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Dar es Salaam amesema, marufuku ya vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara nchini inatokana na kukosekana kwa fikra pevu miongoni mwa viongozi, anaandika Regina Mkonde.

Waitara ambaye pia ni Mwenyekiti wa Uongozi Maalum wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Dar es Salaam amesema hayo leo katika kipindi cha ‘Tuongee Asubuhi’ kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha Star TV.

“Anachofanya Rais Magufuli ni kuzuia siasa za CHADEMA ili tusijiimarishe huku yeye akisuka mipango ya CCM kusikika peke yake pia anadhibiti vyombo vya habari vinavyoandika ukweli, hii ni siasa ya kitoto,” amesema na kuongeza;

“Maamuzi yaliyofanyika si ya haki, Magufuli amezuia mikutano ya CHADEMA anaruhusu ya CCM tu, mwanzo alikataza mikutano ya hadhara lakini alipoona chama chake kitahitaji kufanya mikutano akaruhusu wabunge kufanya kwenye maeneo yao, jambo hili si sawa.”

Waitara amesema kuwa inashangaza kuona hata tamko la kuwataka wabunge na madiwani peke yao kufanya siasa katika Kata na Majimbo yao likikiukwa kwa kuwaruhusu viongozi wakuu wa CCM kufanya mikutano lakini viongozi wa upinzani wakizuiliwa.

“Christopher Ole Sendeka ni msemaji wa CCM na siyo Mbunge, amefanya mkutano mkoani Arusha na polisi walimlinda wala hawakumzuia, lakini ukiacha hilo vyama visivyo na wabunge au madiwani vitajijenga vipi na kupata wabunge wapya bila mikutano?” Amehoji.

Katika hatua nyingine, Waitara amesisitiza adhima ya CHADEMA kufanya mikutano na maandamano nchi nzima kuanzia Septemba Mosi mwaka huu ili kupinga viashiria vya udikteta ambavyo vimeanza kuonekana katika serikali ya awamu ya tano.

“Kufanya mikutano ya hadhara ni haki ya kikatiba na kisheria kwa vyama vyote vya siasa, na UKUTA upo pale pale kwasababu hii ni nchi ya vyama vingi, kama CHADEMA hatufanyi mikutano ya maendeleo watuache, waitishe ya kwao na watushitaki kwa wananchi,” amesema.
Kama umeamua kuandika alichokisema Waitara leo mbona hujasema kuhusu kusifia baadhi ya mambo mazuri ya uongozi wa Rais Magufuli?
 
Naona imekuwa wakati muafaka kwa kila kila mbunge wa chadema kupata kick kwa kutumia jina la magufuli.

Hili neno "kiki" au "kick" naona sasa linazidi kutumika hata out of context!!

Sasa sina hakika utazungumziaje mambo ya nchi hii ya Tanzania ambayo mimi naifananisha na mwili wa binadamu bila kukigusa kichwa (Rais) ambaye kwa sasa ni Magufuli??

Kila media iwe gazeti, TV au Radio na mitandao karibu yote ya kijamii hutaweza kukosa post/habari ambayo inamzungumzia Magufuli John Pombe iwe kwa ubaya au kwa uzuri; kumsifu au kumponda!!

Unafikiri ni kwanini asiwe Jakaya Kikwete tena kama ilivyokuwa hapo kabla ya miezi kumi iliyopita??......hebu nipe jibu Rodney

Au kauli ya "anatafuta 'kiki' huyu kwa......" kwenu nyie mnakuwa mnamaanisha nini hasa??
 
Naona imekuwa wakati muafaka kwa kila kila mbunge wa chadema kupata kick kwa kutumia jina la magufuli.

mim nimefura tu wanavyotisha eti 1.9.2016 ukuta uko pale pale , wao wawe wakwanza kulianzisha
 
Back
Top Bottom