Waitara ampandia Rais Magufuli

Waitara ampandia Rais Magufuli

HATUTAKI LONGOLONGO NCHI INAENDESHWA KWA RASIMU YA CCM.
KAULI MBIU NI HAPA KAZI TUU
 
Sizani kama kauli zinazo onenaka ni maamuzi binafsi ya mtu mmoja ni vizuri kuyafumbia mdomo ikiwa ni athari kwa wengine na faida zao
ni bora tuache nchi iende kwa misingi ile ile tuliyolelewa na wakuu waliopita.kama walikua wanakosea basi wawajibishe kwa uongozi wao mbovu uliotulea..
 
HATUTAKI LONGOLONGO NCHI INAENDESHWA KWA RASIMU YA CCM.
KAULI MBIU NI HAPA KAZI TUU
Kwa kazi gani inayofanywa...?kazi kubwa ingeanza na kutumbua lile jipu la Richmond na wote walio husika hapo tungeona iyo kazi..kazi imekua ya usafi kila jumamosi
 
Witara size yake mi Jerry Slaa, kwa magufuli ni mwendelezo ule ile wa kutaka umaarufu pasipo kuwa maarufu.
umaarufu wa magufuri unatojana na ujinga wa baadhi ya watanzania, mtu asiyetumia akili kamwe umaarufu wake Ni wa mda mfupi. Hitler naye alianza hivi pia idi Amin dadaa
 
Rais anawagwaya UKAWA, lakini kwa sababu ya rais huyo huyo UKAWA wameanza kuwagwaya Wananchi , 2020 Magufuli hapigi kampeni.
Namshangaa huyu mbunge Waitara anang'ang'ania kutaka azungumze na watanzania waliopo Mbeya na kuacha watu wake wanataabika kwa kutokuwa na umeme. Mfano wakazi waliopo maeneo ya Bomba mbili hawana umeme,maji, barabara mbovu, hakuna zahanati na shule ipo moja tu haina hata madawati. Badala ya kutatua kero zilizomzunguka kwenye jimbo lake anataka kwenda mbeya na kwingineko. Namtahadharisha kuwa awe makini maana 2020 sio mbali na tumeshadhamiria kumbwaga hana maana huyu mbunge. Ameshauriwa na Raisi kuwa awe karibu na sisi wananchi tuliomchagua sasa hataki kufanya hivyo badala yake anakimbilia kwenye vyombo vya habari na kuzungumuza mambo amabyo sisi wananchi wa eneo hili tunayaona hayatufai.
haa haa wenzetu mna kura zaidi ya moja nini wakuu...
 
Magu ni sikio la kufa.Yeye anatwanganya anavuruga kila kitu.Huyu sijui anavuta shisha au bange maana katiba na sheria kaweka mfukoni.
 
MWITA Waitara, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Dar es Salaam amesema, marufuku ya vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara nchini inatokana na kukosekana kwa fikra pevu miongoni mwa viongozi, anaandika Regina Mkonde.

Waitara ambaye pia ni Mwenyekiti wa Uongozi Maalum wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Dar es Salaam amesema hayo leo katika kipindi cha ‘Tuongee Asubuhi’ kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha Star TV.

“Anachofanya Rais Magufuli ni kuzuia siasa za CHADEMA ili tusijiimarishe huku yeye akisuka mipango ya CCM kusikika peke yake pia anadhibiti vyombo vya habari vinavyoandika ukweli, hii ni siasa ya kitoto,” amesema na kuongeza;

“Maamuzi yaliyofanyika si ya haki, Magufuli amezuia mikutano ya CHADEMA anaruhusu ya CCM tu, mwanzo alikataza mikutano ya hadhara lakini alipoona chama chake kitahitaji kufanya mikutano akaruhusu wabunge kufanya kwenye maeneo yao, jambo hili si sawa.”

Waitara amesema kuwa inashangaza kuona hata tamko la kuwataka wabunge na madiwani peke yao kufanya siasa katika Kata na Majimbo yao likikiukwa kwa kuwaruhusu viongozi wakuu wa CCM kufanya mikutano lakini viongozi wa upinzani wakizuiliwa.

“Christopher Ole Sendeka ni msemaji wa CCM na siyo Mbunge, amefanya mkutano mkoani Arusha na polisi walimlinda wala hawakumzuia, lakini ukiacha hilo vyama visivyo na wabunge au madiwani vitajijenga vipi na kupata wabunge wapya bila mikutano?” Amehoji.

Katika hatua nyingine, Waitara amesisitiza adhima ya CHADEMA kufanya mikutano na maandamano nchi nzima kuanzia Septemba Mosi mwaka huu ili kupinga viashiria vya udikteta ambavyo vimeanza kuonekana katika serikali ya awamu ya tano.

“Kufanya mikutano ya hadhara ni haki ya kikatiba na kisheria kwa vyama vyote vya siasa, na UKUTA upo pale pale kwasababu hii ni nchi ya vyama vingi, kama CHADEMA hatufanyi mikutano ya maendeleo watuache, waitishe ya kwao na watushitaki kwa wananchi,” amesema.
MWITA Waitara, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Dar es Salaam amesema, marufuku ya vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara nchini inatokana na kukosekana kwa fikra pevu miongoni mwa viongozi, anaandika Regina Mkonde.

Waitara ambaye pia ni Mwenyekiti wa Uongozi Maalum wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Dar es Salaam amesema hayo leo katika kipindi cha ‘Tuongee Asubuhi’ kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha Star TV.

“Anachofanya Rais Magufuli ni kuzuia siasa za CHADEMA ili tusijiimarishe huku yeye akisuka mipango ya CCM kusikika peke yake pia anadhibiti vyombo vya habari vinavyoandika ukweli, hii ni siasa ya kitoto,” amesema na kuongeza;

“Maamuzi yaliyofanyika si ya haki, Magufuli amezuia mikutano ya CHADEMA anaruhusu ya CCM tu, mwanzo alikataza mikutano ya hadhara lakini alipoona chama chake kitahitaji kufanya mikutano akaruhusu wabunge kufanya kwenye maeneo yao, jambo hili si sawa.”

Waitara amesema kuwa inashangaza kuona hata tamko la kuwataka wabunge na madiwani peke yao kufanya siasa katika Kata na Majimbo yao likikiukwa kwa kuwaruhusu viongozi wakuu wa CCM kufanya mikutano lakini viongozi wa upinzani wakizuiliwa.

“Christopher Ole Sendeka ni msemaji wa CCM na siyo Mbunge, amefanya mkutano mkoani Arusha na polisi walimlinda wala hawakumzuia, lakini ukiacha hilo vyama visivyo na wabunge au madiwani vitajijenga vipi na kupata wabunge wapya bila mikutano?” Amehoji.

Katika hatua nyingine, Waitara amesisitiza adhima ya CHADEMA kufanya mikutano na maandamano nchi nzima kuanzia Septemba Mosi mwaka huu ili kupinga viashiria vya udikteta ambavyo vimeanza kuonekana katika serikali ya awamu ya tano.

“Kufanya mikutano ya hadhara ni haki ya kikatiba na kisheria kwa vyama vyote vya siasa, na UKUTA upo pale pale kwasababu hii ni nchi ya vyama vingi, kama CHADEMA hatufanyi mikutano ya maendeleo watuache, waitishe ya kwao na watushitaki kwa wananchi,” amesema.
UKUTA sio Chama cha Siasa
 
Naona imekuwa wakati muafaka kwa kila kila mbunge wa chadema kupata kick kwa kutumia jina la magufuli.
Taifa la vilaza Rais anavunja sheria waziwazi lakini kwa sababu ya umbumbu wenu hamlioni hilo. Tutaendelea kuwa masikini wa hali na mali mpaka mwisho wa dunia tukisindikiza wenzetu wanaojitambuwa. Hivi ukisema rais hili umekosea utakufa?
 
Hakuna ukweli wowote nilioambiwa hapo, ukweli tutaujua 2019 na 2020.Waitara akirudi mnikate kidole mimi mkurya mwenzake lakini dalili za kumng'oa zimeshaonekana.

Usimfananishe waitara na vitu vya kijinga kama CCM
 
Ningekuwa Magufuli ningewapiga stop hata kwenye media maana sasa kero wamezihamiashia huko, kila siku kwenye TV, full kuuza sura.
Mwambie rais Magufuli afute vyama vya siasa vya upinzani ibaki CCM peke yake. Italeta maana zaidi.
 
Back
Top Bottom