Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
WAISLAMU WA JIMBO LA MTWARA VIJIJINI WAMUOMBEA DUA MBUNGE SHAMSIA MTAMBA KUENDELEA KWA MIAKA MITANO IJAYO
Waislamu wa jimbo la Mtwara Vijijini wameonyesha msaada na upendo mkubwa kwa mbunge wao, Shamsia Aziz Mtamba, huku wakimwombea aendelee kupewa dhamana na wananchi wa jimbo hilo kuwa kiongozi wao kwa kipindi cha miaka mitano inayoendelea.
Wahumini hao wa dini ya Kiislamu wameelezea kuridhishwa kwao na utendaji kazi wa mbunge huyo katika kipindi cha uongozi wake, na wamekuwa na matumaini makubwa ya kuona maendeleo zaidi yakifikiwa chini ya uongozi wake.
Katika maombi yao, wahumini hao walionyesha matumaini kwamba Shamsia Aziz Mtamba atachaguliwa tena kuwa mbunge kwa kipindi cha pili, wakisema kuwa amekuwa kiongozi wa mfano na amefanya kazi kubwa katika kuleta maendeleo kwa jamii ya Mtwara Vijijini.
Wanajumuiya wa dini ya Kiislamu walikusanyika katika msikiti Masjid Jamiya ambao mbunge mtamba amesaidia kujenga hadi kukamilika kwake.
Waislamu wa jimbo la Mtwara Vijijini wamesema kuwa kazi nzuri aliyoifanya Mbunge Shamsia Aziz Mtamba imekuwa wazi kwa kila mmoja, na kwamba kiongozi huyo amekuwa na usikivu wa kipekee kwa matatizo ya wananchi.
Wamesema kwamba licha ya changamoto mbalimbali zinazokabili jimbo hilo, kama vile ukosefu wa huduma bora za afya, miundombinu hafifu, na changamoto za kijamii, Mbunge Mtamba ameweza kujitahidi kutatua baadhi ya matatizo hayo na ameonyesha dhamira ya kweli katika kuleta mabadiliko.
“Shamsia Mtamba amekuwa mbunge ambaye amesikiliza na kutatua kero za wananchi wa Mtwara Vijijini.
Vilevile, wahumini waliongezea kuwa Shamsia Aziz Mtamba amekuwa kiongozi ambaye amefungua milango ya mazungumzo na mashauriano na jamii, ambapo ameweza kushirikiana na viongozi wa dini na jamii kwa ujumla katika kutatua matatizo yanayowakabili wananchi.
Uongozi wake wa uwazi na usikivu umejenga imani kubwa kwa wananchi wa jimbo la Mtwara Vijijini, na hivyo kuleta matumaini ya kulipeleka mbele jimbo hilo.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Waislamu wa jimbo la Mtwara Vijijini wameonyesha msaada na upendo mkubwa kwa mbunge wao, Shamsia Aziz Mtamba, huku wakimwombea aendelee kupewa dhamana na wananchi wa jimbo hilo kuwa kiongozi wao kwa kipindi cha miaka mitano inayoendelea.
Wahumini hao wa dini ya Kiislamu wameelezea kuridhishwa kwao na utendaji kazi wa mbunge huyo katika kipindi cha uongozi wake, na wamekuwa na matumaini makubwa ya kuona maendeleo zaidi yakifikiwa chini ya uongozi wake.
Katika maombi yao, wahumini hao walionyesha matumaini kwamba Shamsia Aziz Mtamba atachaguliwa tena kuwa mbunge kwa kipindi cha pili, wakisema kuwa amekuwa kiongozi wa mfano na amefanya kazi kubwa katika kuleta maendeleo kwa jamii ya Mtwara Vijijini.
Wanajumuiya wa dini ya Kiislamu walikusanyika katika msikiti Masjid Jamiya ambao mbunge mtamba amesaidia kujenga hadi kukamilika kwake.
Waislamu wa jimbo la Mtwara Vijijini wamesema kuwa kazi nzuri aliyoifanya Mbunge Shamsia Aziz Mtamba imekuwa wazi kwa kila mmoja, na kwamba kiongozi huyo amekuwa na usikivu wa kipekee kwa matatizo ya wananchi.
Wamesema kwamba licha ya changamoto mbalimbali zinazokabili jimbo hilo, kama vile ukosefu wa huduma bora za afya, miundombinu hafifu, na changamoto za kijamii, Mbunge Mtamba ameweza kujitahidi kutatua baadhi ya matatizo hayo na ameonyesha dhamira ya kweli katika kuleta mabadiliko.
“Shamsia Mtamba amekuwa mbunge ambaye amesikiliza na kutatua kero za wananchi wa Mtwara Vijijini.
Vilevile, wahumini waliongezea kuwa Shamsia Aziz Mtamba amekuwa kiongozi ambaye amefungua milango ya mazungumzo na mashauriano na jamii, ambapo ameweza kushirikiana na viongozi wa dini na jamii kwa ujumla katika kutatua matatizo yanayowakabili wananchi.
Uongozi wake wa uwazi na usikivu umejenga imani kubwa kwa wananchi wa jimbo la Mtwara Vijijini, na hivyo kuleta matumaini ya kulipeleka mbele jimbo hilo.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025