Waislamu mnijibu tafadhali

Waislamu mnijibu tafadhali

Hakuna "Xmass", kuna Christmass.
Sikukuu ya kukumbuka kusulubiwa na kufa kwa YESU KRISTO sio Christmass, ni Pasaka.
Dini haijakataza kushirikiana wala kuishi na wasio waislam ila dini inakataza baadhi ya mambo. Mfano kusherehekea sikukuu zenu.

Mfano xmass, akija kusherehekea nawe xmaa maana yake anakubali kuwa yesu alisurubjwa msalabani na kuuwawa kinyume na utaratibu (imani) ya dini kuhusu tukio lile, ila ikiwa ndani ya siku hiyo hiyo ikawa umemualika aje na familia, zipate kuonana, kufahamiana nakdhalika hapo hakuna kosa,
Sijui kama umenielewa.

Ni kama kungekuwa na 9/dec na wengine wanaamin ilitokea 12/jan hivyo wa 9/dec akila na wa januari maana yake ameamini ya Januari.

Hivyo kama unampa futari mpe tu kama siku nyingine isiwe kwa nia ya KUSHEREHEKEA,
 
“Chakula kilichoandaliwa kwa ajili ya uzushi ni haraam kukila,
Hii fatwa ya sheikh fawzaan ina walaakinj mkubwa sana kwangu inanipa shida sana na hii fatwa..

Kwa sababu zifuatazo..
Chakula kilichoandaliwa kwa ajili ya uzushi ni haraam kukila
Uharamu wa kitu haufanyi vitu vya halali kuwa haramu mfano uharamu wa disco BAA haufanyi chipsi zinazouzwa pale ziwe haramu.

Mimi nikienda baa kununua chipsi au muuza baa akaniletea chipsi sitakiwi kula eti kwa kuwa nikila ninazidi kuipa nguvu ile baa izidi kukuwa ?

Uharamu wa bidaa haufanyi chakula kinachopikwa katika bidaa hhiyo kiwe haramu hata siku moja.


kwa sababu hakikuandaliwa chakula hicho ila kwa ajili ya kuhuisha Bid-‘ah (jambo la uzushi)
Wanaopika wali kwenye bidaa huo wali haujapikwa kwa ajili ya kuhuisha kwa sababu bidaa ipo hata kabla ya chakula.

Kuna bidaa zinafanyika kama vile adhkari za sauti baada ya sala na wala hakuna chakula pale lakini kila siku zinakuwa nyingi.

Kuna bidaa ya kunuti alfajiri katika sala wala hakuna chakula na bidaa hiyo ipo inahuishwa siku zote.

Kwa hiyo sio kweli kwamba hiko chakula kinapikwa kwa ajili ya kuhuisha bidaa.

Hata hivyo mtume anasema "matendo kuhukumiwa kwa nia..."

Kama mtu anakula chakula hicho sio kwa lengo la kuhuisha tatizo lake liko wapi ?
Mimi maadamu umeniletea nnakula

lakini pia kama wao lengo lao ni kuhuisha bidaa mimi nikila huku siikubali bidaa hiyo je lengo lao la kuhuisha bidaa linakuwa limefanikiwa kivipi ?
kula chakula chao, ni kuwapa nguvu kuwasaidia na kukiri juu ya jambo lao la uzushi wanalolifanya
Hapa shekhe anaposema kwamba "NI KUKIRI" ina maana anawajibia wale wanaokula chakula.

Wakati huo ilitakiwa wao wenyewe ndio wajibu na sio shekhe fauzani.

Mimi leo ukiniletea chakula nitakula kwa sababu umeniletea na wala sitakula kwa kutia nia kwamba nakiri krismasi niko pamoja nayo.

Kama nia yangu sio kukiri vipi shekhe aseme k2amba ukila tu inakuwa automatiki umekiri ?

Katoa wapi uswlubu huu allaamah al fawzaan ?
 
Mimi binafsi nakula hiko chakula kama ni cha halali kuliwa.

Sili kwa lengo la kusherehekea sikukuu hiyo bali nakula kwa lengo la kuitikia wema niliofanyiwa na ndugu huyo.

Wakristo wakiowana alafu wakasilimu basi hawaambiwi waowane tena kisa tu ndoa yao ilikuwa haikubaliki na uislamu hapana.

Ndoa yao itakubalika na hakuna haja ya ndoa mpya maadamu kitendo cha ndoa kwao kilifanyika hata kama kwa taratibu zao za kikristo.

Sasa kama uislamu unakubali ndoa za wakristo kwa taratibu zao inakuwaje leo uislamu ukatae chakula tu cha mkristo eti kisa kimepikwa siku ya sikukuu yao ?
Kwa hiyo wewe hata chakula chá matambiko unakula
 
Amesema Shaykh Swaalih Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)
“Chakula kilichoandaliwa kwa ajili ya uzushi ni haraam kukila, kwa sababu hakikuandaliwa chakula hicho ila kwa ajili ya kuhuisha Bid-‘ah (jambo la uzushi). Kwa hiyo haifai kushirikiana nao, wala kula chakula chao kwenye siku hiyo, kwa sababu tendo la kushirikiana nao ama kula chakula chao, ni kuwapa nguvu kuwasaidia na kukiri juu ya jambo lao la uzushi wanalolifanya.”
NA ALLAAH ANAJUA ZAIDI

[Fataawaa Shaykh Swaalih Bin-Fawzaan Al-Fawzaan: Swawtiyaat Sabab Tahriym Twa’aam Al-Bid’ah Ka-Bid’ah Al-Mawlid An-Nabawiy]
Umeongea ukweli
 
Kwa hiyo wewe hata chakula chá matambiko unakula
Shida ni chakula au shida ni matambiko ?

Kama nakula chakula kilichopikwa kwenye ngoma why nisile kilichopikwa kwenye matambiko ?

Kama kula ni kufanya tambiko basi sitakula.
 
Umeongea ukweli

Shida ni chakula au shida ni matambiko ?

Kama nakula chakula kilichopikwa kwenye ngoma why nisile kilichopikwa kwenye matambiko ?

Kama kula ni kufanya tambiko basi sitakula.
Pole ndugu,kuna Uisilamu wa kusoma na wa kurithishwa unabaki kuwa sababu wazazi walisome dini,wewe husomi. Unajua Muisilamu hata ukiwa safarini ni hatali kulakula nyama ovyo sababu hujui aliyechinja
 
Ni msimamo wa waislamu walio wengi kuwa sikukuu za tofauti na dini zao kushiriki kwa namna yeyote ile ni dhambi
Anasema anataka kumfutarisha, nenda kwenye ya hoja yake, mbona unakuwa mzito wa kuelewa hoja.?
 
Pole ndugu,kuna Uisilamu wa kusoma na wa kurithishwa unabaki kuwa sababu wazazi walisome dini,wewe husomi. Unajua Muisilamu hata ukiwa safarini ni hatali kulakula nyama ovyo sababu hujui aliyechinja
Unanifurahisha sana mkuu badala ya kujibu hoja zangu unaanza kunishambulia kuwa sisomi.

Kama wewe ni msomi unatakiwa ujibu comment yangu kielimu ili nijione huo ujinga wangu.

Huo uislamu wako ndio wakurithi fatwa za watu ambazo huzichambui na kuona ukweli wake.

Mimi sipo katika zama hizo,mimi sasa hivi nilishavuka hizo steji za kusomewa dini mimi nasoma dini sisomewi na shekhe wala fulani.
 
Unanifurahisha sana mkuu badala ya kujibu hoja zangu unaanza kunishambulia kuwa sisomi.

Kama wewe ni msomi unatakiwa ujibu comment yangu kielimu ili nijione huo ujinga wangu.

Huo uislamu wako ndio wakurithi fatwa za watu ambazo huzichambui na kuona ukweli wake.

Mimi sipo katika zama hizo,mimi sasa hivi nilishavuka hizo steji za kusomewa dini mimi nasoma dini sisomewi na shekhe wala fulani.
Mbona kuna mtu kamaliza mjadala amefafanua vizuri kabisa kuhusu chakula cha kukalibishwa na wakristo,kwanza kidesturi sio vizuri,hivi ukifika kabla hujaanza kula utauliza huyu kuku kachinja nani?kiujumla waisilamu wanaojielewa ni ngumu sana
 
Kuna uzi humu sikumbuki heading yake ila content ina ujumbe kuwa; muislam hatakiwi kula futari iliyoandaliwa na mke ambaye hajafunga nae ndoa, nadhani kwa mantiki hii unatakiwa usimpelekee kwakuwa haijaandaliwa na mkewe, ila mdau akauliza, je futari inayouzwa migahawani yote imeandaliwa na walioolewa kwa ndoa halali?

Hatimaye nimeupata
"Haujamuoa" ungeelewa hilo neno usingekupa shida, rudia tena kusoma heading ya hiyo mada, ukishindwa kuelewa tena nitajua kumbe shida yako ulikuwa mzito sana shule kwenye mahesabu.
 
Mbona kuna mtu kamaliza mjadala amefafanua vizuri kabisa kuhusu chakula cha kukalibishwa na wakristo,kwanza kidesturi sio vizuri,hivi ukifika kabla hujaanza kula utauliza huyu kuku kachinja nani?kiujumla waisilamu wanaojielewa ni ngumu sana
Mtume alipokaribishwa kula mbuzi aliyealikwa na yule asiyekuwa muislamu aliuliza kwanza nani kachinja ndio akala ?
 
Unanifurahisha sana mkuu badala ya kujibu hoja zangu unaanza kunishambulia kuwa sisomi.

Kama wewe ni msomi unatakiwa ujibu comment yangu kielimu ili nijione huo ujinga wangu.

Huo uislamu wako ndio wakurithi fatwa za watu ambazo huzichambui na kuona ukweli wake.

Mimi sipo katika zama hizo,mimi sasa hivi nilishavuka hizo steji za kusomewa dini mimi nasoma dini sisomewi na shekhe wala fulani.
Na kunavyakula vingine inawezakana ikawa Halamu kutokana na pato lá huyo mkristo,mfano anaishi kwa biashara ya Guest,au anafanya biashara ya bar,ni hatali kula chakula chake
 
Mtume alipokaribishwa kula mbuzi aliyealikwa na yule asiyekuwa muislamu aliuliza kwanza nani kachinja ndio akala ?
Pole sana kwa maswali yako,wenda utakuwa sio Muisilamu.au ndiyo wale ukiona nyama,wewe twende tu
 
Na kunavyakula vingine inawezakana ikawa Halamu kutokana na pato lá huyo mkristo,mfano anaishi kwa biashara ya Guest,au anafanya biashara ya bar,ni hatali kula chakula chake
Wewe ni kilaza sana kwenye hii dini.

samahani lakini.
 
Back
Top Bottom