Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
Kuna mama aliifiwa na mumewe miaka takriban 20 iliyopita. Alikuwa kwenye 30’s miaka hiyo. Mume wake alimuacha na nyumba pamoja na pesa na mali za kutosha. Alisomesha watoto, alicheza harusi, sasa amebaki nyumbani mwenyewe na house boy.
Amepata boy friend yuko kwenye 40’s hivi, mama amenogewa na penzi. Baadae alikuja kugungua mpenzi alimpendea hela, kwani mama alikuwa na vitega uchumi vya kumwaga. Kuanzia nyumba za kupangisha na bed and breakfast.
Sasa mama ameshikwa na Homa kali ghafla, kwa taratibu za hospitali aliyofika wagonjwa wanapimwa kila kitu ili kurahisisha tiba. Mama amekutwa HIV+ akiwa 57yrs.
Ana haha jinsi ya kuwafahamisha wanae.
Amepata boy friend yuko kwenye 40’s hivi, mama amenogewa na penzi. Baadae alikuja kugungua mpenzi alimpendea hela, kwani mama alikuwa na vitega uchumi vya kumwaga. Kuanzia nyumba za kupangisha na bed and breakfast.
Sasa mama ameshikwa na Homa kali ghafla, kwa taratibu za hospitali aliyofika wagonjwa wanapimwa kila kitu ili kurahisisha tiba. Mama amekutwa HIV+ akiwa 57yrs.
Ana haha jinsi ya kuwafahamisha wanae.