Wagonjwa 60 wa moyo wanatarajia kufanyiwa upasuaji katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete

Donatila

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,557
21,512
moyo(1).jpg
Jopo la madaktari bingwa wa Moyo toka nchini Saudi Arabia kwa kushirikiana na madaktari wa taasisi ya magonjwa ya moyo ya jakaya kikwete wanatarajia kuwafanya upasuaji wa moyo kwa njia ya kuzibua mishapa zaidi ya wagonjwa sitini kwa muda wa siku tano.

Dokta Tulizo Shemu ni mmoja wa madaktari bingwa wa Moyo katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ambaye amesisitiza ushirikiano huo utasaidia kuwajengea uwezo ikiwemo matumizi ya teknolojia za sasa na pia utaokoa zaidi ya shilingi bilioni 2.4 iwapo wagonjwa hao wamesafirishwa nje ya nchi ikiwemo India kwa ajili ya upasuaji wa moyo kama huo.

Bwana Bader al Anezi ni mtaalamu wa mishipa ya Moyo na mwalimu toka nchini Saudia Arabia amesema taasisi ya kimataifa ya misaada ya kiislamu inalenga kutoa huduma ya matibabu ya Moyo na kubadilisha uzoefu na wataalamu wa matibabu wa Moyo wa kitanzania na kusisitiza moja ya changamoto zinazowakabili ni taratibu ngumu za utoaji wa matibabu ya Moyo hususani katika operesheni.

Akizungumza na ITV mmoja wa wagonjwa wa Moyo waliokwisha mfanyiwa matibabu amepongeza jitihada zinazofanywa na madaktari hao katika kutibu magonjwa ya Moyo kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya kwenye mishipa ya damu badala ya kupasua kifua ambapo amewataka watanzania kutumia taasisi hiyo na kuondokana na dhana ya kufuata matibabu ya moyo nje ya nchi.


ITV
 
Back
Top Bottom