Wafuatao wajiuzulu sasa

Wafuatao wajiuzulu sasa

ni kweli tupu, mh abubakar (cuf)wazir wa katiba na sheria smz amesema wazi kibanda maiti.

Nataka kufahamu nini msimamo wa makamu wa kwanza wa Rais Znz?
Ni bora Cuf kwa kupitia swala hili la katiba wafanye wawezavo warudishe Imani kwetu Sisi wananchi! Maana chama kilikua kinaenda kupoa!
 
Ndani ya ccm na serikali kuna vimtu vichache vinajifanya nunda kwa nn hamvitemi?
 
Mkuu habari za lumumba bhana , Tambwe hiza hajambo ? Naam , baada ya salaam naomba nikwambie kwamba hakujawahi kutokea mwanaccm kujiuzuru kwa hiyari yake , labda tuwatimue .
Tupo poa.Kwa hili,kuna mtu atawajibishwa.Subiri uone!
 
Hapa ungependa nani awajibishwe? Na kwa kosa gani? Ebu dadavua kidogo!
Mkuu Ntuzu,umesoma bandiko langu vizuri? Tafadhali soma ili upate majibu ya maswali yako
 
Last edited by a moderator:
Sahihisho: ... Muswada huo uliopitishwa 'kiujingaujinga'. ..

Nimeso vizuri ila nilipenda kupata maoni toka kwako Mkuu! Ungependa nani ajiuzuru? Warema au Chikawe au na Yule alieruhusu maafisa wa Polisi kuingia bungeni na kumbeba Sugu mzobemzobe!?
 
Ccm kwa uongo ni namba moja, nawapongeza wapinzani kwa kuwa wazalendo wa kweli kwa taifa letu, hongera kamanda mpambanaji lissu kwa kusema ukweli!
 
Katika Mkutano wa watanzania wapigania Katiba bora uliofanyika Viwanja vya Kibanda Maiti-Zanzibar,mambo yamekuwa mambo. CCM na Serikali yake imedhalilishwa,imeumbuliwa na kuchafuka. Hata Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar nayo iko hatarini kutawanywa na upepo mkali wa Katiba mpya. Mkutano husika ulihudhuriwa na kuhutubiwa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa nchini.Lakini,Waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar naye alikuwepo.Ni Ndugu Abubakar Khamis Bakari.

Huyu ndiye ninayemlenga. Akiwa jukwaani Kibanda Maiti leo,Ndugu Bakari amesema kuwa Waziri Mathias Chikawe (Katiba na Sheria) na Naibu Spika Job Ndugai ni waongo na wamelipotosha Taifa.Walidai kuwa Wazanzibari walisikilizwa wakati wa mchakato wa kuandaa Muswada wa Sheria ya Katiba mpya uliopitishwa 'kimagumashi' Bungeni Dodoma. Ingawa hawa hawakutajwa na Waziri Bakari,lakini mkumbo wa 'uongo' wa kuwasikiliza Wazanzibari ni pamoja na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Idd pamoja na Waziri Mkuu Pinda.

Balozi Idd alialikwa Dodoma(inasemekana na Waziri Mkuu Pinda) kwenda kutamka kuwa Zanzibar imesikilizwa na Muswada umeandaliwa ipasavyo. Akafanya hivyo.Akapigiwa makofi sana.Wapinzani wakabezwa na kuonekana wakorofi. Leo,Waziri ambaye ni mhusika wa kwanza wa masuala ya Sheria Zanzibar (Ndugu BAKARI) amepasua jipu. Amekanusha.Ametofautiana na Makamu wake wa pili wa Rais wa Zanzibar-Balozi Idd.Amesema Zanzibar haikuwahi kusikilizwa.Muswada ni batili!

Kukanusha maneno ya Balozi Idd ni kuuharibu na kuusawajisha msimamo wa CCM na Serikali yake kuwa Wazanzibari walisikilizwa(na kutoa maoni yao juu ya Muswada huo). Ni kuiumbua Serikali na chama. Ni aibu kubwa kwa chama na Serikali.

Kama maneno ya Waziri Bakari hayatakanushwa kwa ushahidi mujarabu,nategemea wafuatao wajiuzulu mara moja:Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar,Waziri Mkuu, Waziri Chikawe,Mwanasheria Mkuu-Jaji Fredrick Mwita Werema na wote walioshupalia kuwa Wazanzibari walisikilizwa.Halafu,Rais Kikwete hana haja ya kusaini Muswada huo uliopitishwa 'kiujanjaujanja'. Na kama Waziri Bakari amesema uongo leo Viwanja vya Kibanda Maiti-Zanzibar,basi naye ajiuzulu haraka.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Mbali na ujumbe murua uliotupa mzee 2pa 2pa ila mimi siku zote navutiwa na jinsi unavyomaliziaga kwa utambulisho wako ha ha ha ha
 
Nimeso vizuri ila nilipenda kupata maoni toka kwako Mkuu! Ungependa nani ajiuzuru? Warema au Chikawe au na Yule alieruhusu maafisa wa Polisi kuingia bungeni na kumbeba Sugu mzobemzobe!?
Mkuu, naamini hii ilikuwa ni syndicate/tactical game within the rulling party. Kwa hiyo kama ni kujiuzulu, basi iwe kule vichwani (kiongozi wa bunge/speaker & majority leader). Ila siku hizi kujiuzulu imekuwa kibwagizo tu/hajiuzulu mtu ng'o!
 
Nimemsikia Nape analeta uongo kijana mdogo lakini mpuuzi kwamba Katiba si Uchaguzi .Yaani sikuelewa kwamba jamaa ana akili au ? Nadhani CCM wanaumia na matamshi yake na anaiuwa CCM maana kila Mtanzania sasa anajua maisha yake ni Katiba yenye usawa na si zaidi .
 
serikal sikivu leo vp tena kuumbuana hivyo ila Zanzibar hawana ujnga ujnga wa kuburuzwa km huku bara leo kuna raia wanaamn kuwa CCM iko sahh ktk swala hl la katiba bdala ya kuungana na wanaotaka mabadlko ktk vpengele vya rasmu hyo maana katiba ndio kla k2 hawa viongoz wa TZ walxhakuwa Mngu wa2 kwa 7b katiba haiwabani
 
huo msamiati 'kujiudhuru' hii nchi bado hatuufahamu vema !
Umenena kweli pia hata neno Duble Chris nalo wewe ndo founder hatukuwahi kulisikia.Lugha ni mawasiliano ndo maana hata wakati mwingine tunatumia ishara kuwasiliana hivyo kama wewe hujaelewa ilo sisi halituhusu kwani sometimes kuna kitu tunaita code name au code language.
 
CCM wabaya jamani, wanamsaliti hadi mwana CCM mwenzao!

Prof Lipumba
jangwani
 
Back
Top Bottom