Idimulwa
JF-Expert Member
- May 27, 2011
- 4,503
- 1,722
Ni aliyekuwa mgombea wa udiwani kata ya Kirumba kupitia CCM bwana Jackson Robert maarufu kama Masamaki.Hajalipa mishahara ya wafanyakazi wa kampuni ya ulinzi anayoimiliki iitwayo Victoria Support Services kwa takribani miezi minne sasa.Kwa sasa wafanyakazi wamezingira ofsini kwake pale mtaa wa Nera jijini Mwanza na jamaa kaingia mitini...Kwa sasa wanapanga kuandamana kwenda kwa RC.
Jamaa ameripotiwa kuyumba ki uchumi baada ya kutumia kiasi kikubwa cha fedha kwenye kampeni kuupata udiwani na kuambulia patupu baada ya wana Mwanza,kata ya Kirumba kula CCM kama kawaida yao na hatimaye kupiga kura yao CDM na kumwezesha mgombea wa CDM kuibuka kidedea.
MY TAKE:Ni bora uongozi wa CCM ukaandaa utaratibu wakuwa unawawezesha wagombea wao hasa wafanyabiashara wanapofikia hatua ya kufulia kwa manufaa ya chama chao.
Source:Mimi mwenyewe nimepita viunga vile vya mitaa ya Nera,picha sikupiga kwani nilihisi uvunjifu wa amani kutokea maana jamaa walikuwa na hasira sana.
Jamaa ameripotiwa kuyumba ki uchumi baada ya kutumia kiasi kikubwa cha fedha kwenye kampeni kuupata udiwani na kuambulia patupu baada ya wana Mwanza,kata ya Kirumba kula CCM kama kawaida yao na hatimaye kupiga kura yao CDM na kumwezesha mgombea wa CDM kuibuka kidedea.
MY TAKE:Ni bora uongozi wa CCM ukaandaa utaratibu wakuwa unawawezesha wagombea wao hasa wafanyabiashara wanapofikia hatua ya kufulia kwa manufaa ya chama chao.
Source:Mimi mwenyewe nimepita viunga vile vya mitaa ya Nera,picha sikupiga kwani nilihisi uvunjifu wa amani kutokea maana jamaa walikuwa na hasira sana.