Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,600
- 218,001
Mgombea udiwani wa Kata ya Gulwe kwa tiketi ya Chadema na wenzake wanne , Walikamatwa 13/9/2020 kwa amri ya WAKUBWA na kubambikiwa kesi ya uongo ya unyang'anyi wa kutumia silaha , Wakaswekwa rumande bila dhamana ili kusaidia Mgombea wa ccm kupita bila kupingwa .
Yaani Uchaguzi wa kata , tena kata yenyewe ya huko porini Mpwapwa inasababisha mtu ambaye hajawahi hata kumiliki bisibisi ya kufungulia feni anapewa kesi nzito ya unyang'anyi wa kutumia silaha ! Unyama kama huu ndio waliofanyiwa Wagombea wote wa Chadema Nchi nzima , Huu ndio Uchaguzi huru na wa haki uliosimamiwa na Dr Mahera , Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi ambaye sasa anapigiwa chapuo ya kuongoza TUME HURU YA UCHAGUZI , KWA DEBE LA CCM na mshirika wao ACT .
Bali kama tulivyosema siku zote kwamba SHETANI HAJAWAHI KUMSHINDA MUNGU , ndivyo ilivyotokea kwa Watuhumiwa hawa wa Kesi ya Uongo LEO WAMEACHIWA HURU NA MAHAKAMA YA WILAYA YA MPWAPWA .
Tunachopaswa kujua ni kwamba , KILA UBAYA ULIOWATENDEA WENZAKO IKO SIKU UTALIPWA , muda ndio mwamuzi .