Ukishavuna utaenda kuyauzia wapi??Wayafunge tuu, Mfanyabiashara yoyote lazima uwe na plan A na B, A ikishindikana unakwenda B. Mi nimefunga naenda kulima na kufuga.
Mwanza mtaa wa rwagasore maduka hayana wateja wamachinga wamepanga vitu barabarani nje ya maduka yani wanauza kila kitu ambacho kipo dukani mbaya zaidi hawalipi kodi wala hawana leseni sasa unategemea wenye maduka wafanye nini!?Ni sehemu gani na mkoa gani na mtaa gani maduka yamefungwa? Kama wameona ni vyema kufunga wafunge....
Hamjamwelewa Minja. Yeye kasema maduka ni biashara rasmi na inayolipa kodi na kufuata taratibu zote za kibiashara. Lakini wanasumbuliwa sanawakati sasa hivi wapo wanaoitwa wamachinga lakini anabiashara inajaa kontena na hatoi risiti bali yeye anapanga biashara zake nje usiku anakusanya.Wafunge wale nini! Jeuri hiyo wanayo?
Wafunge tuu, tuone upande mwingine wa shillingi!!!!!!Wafunge tu maana hata wateja hakuna wafunge hata mwezi mmoja hivi
Embu tutajie makusanyo ya TRA ya mwezi Novemba 2016Wigo wa kodi ni mpana sana na biashara ni kama daladala wengine wanafunga wengine wanafungua. Wengi wa hao wanaofunga hawakuwa wanalipa kodi hivyo serikali mapato yako vile vile tena yanaongezeka sab wigo umezidi kupanuliwa kwa mfano maduka mengi yanatumia efd mahotel yote siku hizi ukienda na mchepuko unapata efd makampuni ya huduma za kuzoa takataka wanatoa risiti za efd baadhi ya daladala wanatoa risiti za efd hebu angalia wigo huo.
Kawaulize TRAEmbu tutajie makusanyo ya TRA ya mwezi Novemba 2016
Wewe utakuwa mshabiki maandazi wa chama chako cha kijaniKawaulize TRA
Hakuna chama kingine cha kushabikia sab wapinzani hawajitambui. Wanapinga ufisadi huku wanakumbatia ufisadi. Wanatetea demokrasia wakati kwenye vyama vyao migogoro kila kukicha huku chaguzi zao zikikosa mwelekeo wa kidemokrasia. Wanapinga ukabila udini na ukanda huku wameupa kibali kwenye vyama vyao.Wewe utakuwa mshabiki maandazi wa chama chako cha kijani
Aliposema wafanyabiashara 2000 wamefunga maduka alimaanisha hali ikiendelea hivi, wenye maduka wote watageuka machinga na serikali itayakosa mamilioni ya kodi kutoka kwao...Wakifunga watakuwa wamemkomoa nani?
Kumbuka ukifunga biashara yako wewe ni hasara kwako na familia yako.
Serikalit itaendelea kupata mapato yake vile vile kwa sababu wateja waliokuwa wananunua bidhaa kwako watakwenda kununua kwa mtu mwingine.
Hivyo utakuwa umejikaanga wewe mwenyewe.
Ukweli ni kwamba hakuna biashara. Wachukue likizo. Waajiriwa wao wawape likizo bila malipo Kama sheria inaruhusu. Wasisahau kutoa taarifa TRA wasije wakadaiwa kwa muda wasiofanya biashara.Wafunge tu maana hata wateja hakuna wafunge hata mwezi mmoja hivi