Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,026
- 1,621
Baadhi ya Wafanyabiashara wa Mahindi kutoka Mikoa mbalimbali wamefunga mpaka wa Tanzania na Zambia upande wa Tunduma mkoani Songwe kwa zaidi ya masaa mawili, kwa kuegesha magari yao, wakishinikiza serikali ya Tanzania kukaa meza moja na serikali ya Zambia, ili iwapatiwe mahindi yao zaidi ya tani 1,200 ambayo wamedai kununua kwa njia halali lakini yameshikiliwa kwa zaidi ya miezi mitano ,licha ya kuwa na vibali halali vya kununulia na kusafirishia mazao hayo kutoka nchini humo.
Akielezea tukio hilo na hatua zilizochukuliwa na serikali,, Mkuu wa wilaya ya Momba Bw. Fakii Lulandala ,amesema tayari serikali ya Zambia imewataka wafanyabiashara hao ambao wamenunua kihalali kuuza mahindi hayo ndani ya Zambia na si vinginevyo, huku akiwataka kuwa watulivu kwa kipindi hiki wakati suala hilo linatafutiwa ufumbuzi wa kudumu.
Chanzo: ITV
Akielezea tukio hilo na hatua zilizochukuliwa na serikali,, Mkuu wa wilaya ya Momba Bw. Fakii Lulandala ,amesema tayari serikali ya Zambia imewataka wafanyabiashara hao ambao wamenunua kihalali kuuza mahindi hayo ndani ya Zambia na si vinginevyo, huku akiwataka kuwa watulivu kwa kipindi hiki wakati suala hilo linatafutiwa ufumbuzi wa kudumu.
Chanzo: ITV