Dr Matola PhD
Platinum Member
- Oct 18, 2010
- 61,429
- 108,580
Bwana we si nikatokea kumpenda mkaka mmoja hapa ofisini, muda mrefu tu umepita, sema kila nikijipendekeza alikuwa haelewei somo, basi nikaamua kuacha na hizo mambo za kumuwinda winda kila mara, miaka miwili ikapita ghafla na yeye akaanza kujiweka karibu na mimi, kwa vile nampenda sana sikuweza kuresist basi nikarespond nikamchukulia kama rafiki wa karibu tu sio mpenzi.
Sasa katika mazoea haya ya urafiki mwenzangu sijui anahisi yupo na mke wake, kila siku anataka apate chakula cha jioni kwangu, basi nitajipikilisha wee jamaa anakuja anakula anasepa, huyu jamaa anapenda vyakula vya kuchemsha tu, visiungwe hata, na mimi napenda kukaanga ile mbaya,akaanza visa akikuta tumepika chakula asichopenda matusi yatamtoka huyo utafikiri alitoa hela halafu nikanunua vitu vingine.
Kujifanya kuimiliki nyumba utafikiri anajua hata kodi ya nyumba ni sh ngapi, akifika home basi itabidi muangalie vipindi anavyotaka yeye tu, maongezi yawe anayotaka yeye tu, feni izimwe.
Nimemwambia mara kadhaa kuwa yupo selfish sana anaona kama namtania vile nimfanyeje huyu mtu jamani?
Unaishi mkoa gani?