Zipuwawa
JF-Expert Member
- Nov 28, 2010
- 3,053
- 653
Katika kusoma soma Blog nimekutana na hili hapa sasa naomba kujua kutoka kwenu hili linaukweli? Aliyefanya utafiti alikuja na majibu haya si mimi naombeni mnifumbue macho ....
''Ni vitu gani ambavyo mwanamke anaviangalia kwanza anapokutana na mwanaume? Je,anaangalia sura? Je,anaangalia tabasamu? Anaangalia au anavutiwa na nini hasa?Hapa najaribu kuzungumzia vitu ambavyo vinaangaliwa kwa mtizamo wa haraka haraka kabla mambo mengine hayajawekwa kwenye mstari kama vile kujua mtizamo wa mtu katika maisha,ndoto alizonazo,imani,anavyojali na kupenda maisha nk.
Miaka takribani miwili iliyopita,niliwahi kuketi katika kundi la wanawake,nikawauliza kwa haraka haraka huwa wanaangalia vitu gani wanapokutana na mwanaume kwa mara ya kwanza iwe ni kazini,katika party,club nk?
Majibu waliyonipa yalikuwa mengi. Lakini miongoni mwa majibu mengi,ilikuwa wazi kabisa kwamba kuna vitu vinne ambavyo wengi miongoni mwa wanawake niliokuwa nao katika genge lile huviangalia ni Saa aliyovaa,mkanda wake(hususani kama unaonekana-maana anaweza kuwa kachomolea),viatu alivyovaa na kisha manukato au anavyonukia(akinuka hiyo ni habari nyingine kabisa)
Kwa namna fulani,naurejesha huu mjadala hapa.Je,wewe kama mwanamke,ukikutana na mwanaume hivi leo,kabla hujamjua zaidi,unaangalia vitu gani?
Majibu yenu yanahitajika hapa ili wanaume wawe wanajua mnapenda nini hasa?
Read more: SAA,MKANDA,VIATU NA MANUKATO-UNAJALI? - BongoCelebrity
''Ni vitu gani ambavyo mwanamke anaviangalia kwanza anapokutana na mwanaume? Je,anaangalia sura? Je,anaangalia tabasamu? Anaangalia au anavutiwa na nini hasa?Hapa najaribu kuzungumzia vitu ambavyo vinaangaliwa kwa mtizamo wa haraka haraka kabla mambo mengine hayajawekwa kwenye mstari kama vile kujua mtizamo wa mtu katika maisha,ndoto alizonazo,imani,anavyojali na kupenda maisha nk.
Miaka takribani miwili iliyopita,niliwahi kuketi katika kundi la wanawake,nikawauliza kwa haraka haraka huwa wanaangalia vitu gani wanapokutana na mwanaume kwa mara ya kwanza iwe ni kazini,katika party,club nk?
Majibu waliyonipa yalikuwa mengi. Lakini miongoni mwa majibu mengi,ilikuwa wazi kabisa kwamba kuna vitu vinne ambavyo wengi miongoni mwa wanawake niliokuwa nao katika genge lile huviangalia ni Saa aliyovaa,mkanda wake(hususani kama unaonekana-maana anaweza kuwa kachomolea),viatu alivyovaa na kisha manukato au anavyonukia(akinuka hiyo ni habari nyingine kabisa)
Kwa namna fulani,naurejesha huu mjadala hapa.Je,wewe kama mwanamke,ukikutana na mwanaume hivi leo,kabla hujamjua zaidi,unaangalia vitu gani?
Majibu yenu yanahitajika hapa ili wanaume wawe wanajua mnapenda nini hasa?
Read more: SAA,MKANDA,VIATU NA MANUKATO-UNAJALI? - BongoCelebrity