Wachina wajivunia utaifa na uzalendo, miaka 50 baada ya kurejeshewa kiti halali cha China katika Umoja wa Mataifa

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
NA CAROLINE NASSORO

VCG21gic6409869.jpg

Wananchi wa China wamevamia mitandao ya kijamii wakitoa heshima kwa mashujaa waliojitoa mhanga kwa ajili ya amani na ustawi wa taifa hilo, na pia kwa China kujitolea kulinda utaratibu wa kimataifa na amani ya dunia.

Hayo yamefanika wakati wa kumbukumbu ya miaka 50 tangu Jamhuri ya Watu wa China kurejeshewa kiti chake halali katika Umoja wa Mataifa, jambo hili limefanya hisia za utaifa na uzalendo kuongezeka kwa kiwango cha juu zaidi kwa Wachina.

Novemba 15, 1971, wakiongozwa na Qiao Guanhua, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje ya China kwa wakati huo, ujumbe wa China uliingia katika Ukumbi wa Mikutano wa Umoja wa Mataifa. Mara baada ya kuingia, ujumbe huo ulifuatiliwa kwa karibu katika mkutano wa 26 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Alipoulizwa anajisikiaje kuwa katika ukumbi huo, Qiao alicheka kwa sauti kubwa na kuwashangaza wajumbe wote waliokuwa kwenye mkutano huo. Siku chache kabla ya hapo, Oktoba 25, 1971, haki zote za Jamhuri ya Watu wa China zilirejeshwa kwa msaada wa nchi zinazoendelea za Asia, Afrika na Latin Amerika.

Katika kumbukumbu ya siku hiyo mwaka huu, picha na video za Qiao Guanhua, ambaye wakati huo alikuwa, zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ya China, huku kishikizo (hashtag) “miaka 50 ya kurejeshwa kwa kiti halali cha China katika Umoja wa Mataifa” ikitamba kwenye mitandao hiyo.

Kupitia mitandao yao ya kijamii, Wachina wengi wanaona kuwa hatua ya China kurejeshewa kiti chake halali katika Umoja wa Mataifa ulikuwa mwanzo wa ukurasa mpya, na ni hatua kubwa katika diplomasia ya China, kwani kuanzia hapo, China ilijiunga karibu na mashirika yote ya kimataifa na kusaini zaidi ya mikataba 600 ya kimataifa.

Mmoja wa watumiaji wa mitandao hiyo anasema, China imekuwa ikishikilia bila kusita utaratibu wa kimataifa chini ya mfumo wa Umoja wa Mataifa, na tofauti na nchi fulani, haijawahi kuchana ama kujitoa kwenye makubaliano yoyote.

Kwa ufupi, tunaweza kuona jinsi Wachina wanavyojivunia taifa lao, na wanavyofuatilia masuala ya kimataifa, hususan yanayoendana na maslahi ya taifa lao. Mshikamano na umoja wa taifa hili umedhihirika mara nyingi katika masuala mbalimbali, mfano wa karibuni ni wakati mlipuko wa janga la COVID-19 ulipotokea. Wananchi walikuwa na imani na uongozi wao, na walifuata miongozo iliyotolewa, na kuiwezesha nchi hiyo kudhibiti kwa mafanikio maambukizi ya virusi vya Corona.

Wakati tukiipongeza China kwa kurejeshewa kiti chake halali katika Umoja wa Mataifa, tunapaswa pia kuipongeza China kwa kuendelea kupaza sauti ya nchi zinazoendelea katika majukwaa ya kimataifa, ikiwemo Umoja wa Mataifa.

Pongezi kwa China kwa kuendelea kudumisha utaratibu wa kimataifa chini ya mfumo wa Umoja wa Mataifa, na kwa kutetea haki za wanyonge katika nchi zinazoendelea.
 
  • Kicheko
Reactions: BAK
Chaguzi zao si huru wala za haki. Vyombo vya habari haviko huru. Wachina hawako huru kuikosoa Serikali yake na waliomo ndani ya Serikali na Wachina wengi wanatamani sana kuhamia nchi za Magharibi na wengi wamefanya hivyo.
 
Back
Top Bottom