Wachagga na Kahawa

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
21,142
30,493
Nimekuwa na kawaida siku hizi kuwa ninaposoma Makala ya historia basi huenda kwenye kazi zangu zilizopita na kuangalia nini nimeandika.

Ndugu yangu Abdulkarim Ally ameandika makala (haipo hapa) iliyonivutia sana kuhusu siasa za Uchaggani wakati wa ukoloni.

Imesadif kuwa mimi nilitafiti na kuandika kitabu kuhusu maisha ya Rajabu Ibrahim Kirama kutoka Nkuu, Machame.

Katika maisha ya Mzee Rajabu ambae alizaliwa miaka ya mwishoni 1800 na kufariki mwaka wa 1962 maisha yake yaliingiliana na watu ambao

Abdulkarim Ally kawataja katika makala yake.
Abdulkarim kamtaja Sir Charles Dundas.

Nimemweleza Charles Dundas kwa maneno haya:

Charles Dundas:

‘’Historia ya Wachagga imeandikwa kwenye upeo wa hali ya juu na Wazungu kiasi cha kumstaajabisha msomaji.

Inawezekanaje kwa Mzungu kutoka Ulaya mtu mgeni kuijua historia kwa undani wa kiasi kuweza kueleza mambo yaliyotokea miaka mingi sana iliyopita.

Mwandishi Mwingereza Charles Dundas ameandika historia ya Wachagga kwa kiwango cha kustaajabisha.

Charles Dundas ameelezea mengi ambayo mtu hupata tabu hata kuyafikiri achilia mbali kuyajua hadi awe ameyasoma.

Wachagga wana hulka pale wanapompenda mgeni basi watampa lakabu inayoendana na heshima ya kabila lao.

Charles Dundas walimwita, Wasaoye-o-Wachagga, yaani Mzee wa Kichagga.’’

Joseph Merinyo:

‘’Kaka yake jina lake Ngulelo waliochangia mama mmoja akawa Mangi wa Machame na Ngulelo alitawala hadi 1916 na ulipofika mwaka wa 1917 Waingereza wakamtoa kuwa Mangi wakampeleka uhamishoni Kismayu, Somaliland.

Taarifa nyingine zinasema alipelekwa Lamu, Kenya na kuwekwa kifungoni hapo kisiwani.

Waingereza wakamweka Joseph Merinyo kushika nafasi ile kwa muda.
Joseph Merinyo ana historia ya pekee katika siasa za Wachagga.

Joseph Merinyo alikuwa amesafiri hadi Ujerumani wakati huo akifanya kazi kwa Mjerumani ambaye ndiye aliyemchukua hadi Ulaya.

Kwa miaka ile kwa Mwafrika kufika Ulaya ilikuwa ni elimu tosha.

Joseph Merinyo akaja kuwa mkulima wa kahawa katika wakulima wa mwanzo Uchaggani kuingia katika kilimo hicho na alitajirika.

Mchagga mwingine aliyekuwa mkulima wa kahawa nyakati zile alikuwa Petro Njau.

Ngulelo alipokuwa kifungoni ndiyo akasilimu na kuwa Muislam akachagua jina la Selemani.

Ngulelo akawa Muislam wa kwanza katika ukoo wa machifu wa Kichagga.

Aliporudi kutoka kifungoni Ngulelo sasa akijulikana kama Mangi Selemani akaishi Machame mahali panaitwa Ng’ambo kwa kuwa kufika huko ilikuwa lazima uvuke bonde.

Inasemekana kuwa alipokuwa mtawala wa Machame Ngulelo hakuwa na uhusiano mzuri na Wamishionari ambao walikuwa wamedekezwa sana chini ya utawala wa Shangali.’’

Wapo wengi aliowataja Abdulkarim Ally ambao wako katika kitabu hicho hapo chini.

Hapa nimeweka machache kiasi.

1715283074775.jpeg


Alichoandika Abdulkarim Ally:

Mr A. L. B. (Ben) Bennett DFC.( Distinguished Flying Cross) Alikuwa Rubani Wa Ndege za kivita katika Jeshi la Anga la Uingereza Royal Air force katika wakati Wa vita ya Kwanza ya Dunia .

Mwaka 1927 A. L. B. (Ben) Bennett DFC pichani, rubani wa kivita katika Vita vya Kwanza vya Dunia kutoka Uingereza alifika Kilimanjaro kama Afisa Kazi.

Kwa kushirikiana na Sir Charles Dundas aliekuwa Mkuu Wa wilaya ya Moshi walisaidia wazawa kuunda Umoja wao kwa mujibu wa kanuni za ushirika ambazo zilisisitiza haja ya kuwa na Vyama vya Ushirika vya Msingi.

1932 Vyama vya msingi 11 vilisajiliwa, ambavyo ni Kibong’oto, Uru Central, Kilema, Kibosho Central, Kibosho East, Kibosho West, Machame Central, Mamba, Tarakea, Mkuu Rombo, and Useri.

Uundaji wa Vyama hivi vya Msingi ulifungua njia ya kuanzishwa kwa Kilimanjaro Native Cooperative Union kwa mujibu wa sheria ya Ushirika.

Kahawa ilipandwa kwa mara ya kwanza huko Kilema na Wamisionari Wakatoliki mwaka 1898, na baadaye Walowezi wa Ujerumani.

Wenyeji wa Kilimanjaro hawakuruhusiwa kupanda kahawa badala yake walifanya kazi kwenye mashamba ya Settlers.

Ilikuwa hadi mwisho wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia mwaka 1918 ambapo Ujerumani ilishindwa vita hivyo ikapoteza makoloni yake ikiwa ni pamoja na Tanganyika ya wakati huo.

Mwanzilishi wa Vyama vya Wazawa wa Kilimanjaro alikuwa wakati huo Mkuu wa Wilaya ya Moshi wa kwanza Mwingereza Sir Charles Cecil Farquharson Dundas (1884 - 1956) aliwaruhusu wazawa kulima kahawa kama zao la biashara.

Alieneza uzalishaji wa kahawa katika eneo hilo, na akapewa jina la Wasaoye-o-Wachagga (Mzee wa Wachagga) na Arthur Bennett akapewa Jina la heshima la Mbuya -o- Wachanga yaani Rafiki Wa Wachagga.

Kuruhusiwa kulima kahawa wenyeji walipata mbegu kutoka kwa makanisa ambako kahawa ilikuzwa.

Walipanda mazao lakini hawakuwa na ujuzi wa zao hilo.

Vita vya Kidunia vilikuwa vimesababisha uhitaji mkubwa wa kahawa huko Uropa kwa hivyo wanunuzi wengi walikuwa walowezi wa kizungu wanaoiuza nje. Wenyeji walitumia ndoo, mifuko na njia nyinginezo kubebea kahawa kwa walowezi.

Machafuko ya kijamii na kiuchumi yaliyoletwa na White Settlers na wafanyabiashara wa Asia wakati wa biashara yaliwalazimisha wakulima wadogo kuanzisha vyama vya ushirika kwa ajili ya ukombozi wa kijamii na kiuchumi.

Mwaka 1925 wenyeji waliunda Kilimanjaro Native Planters Association (K.N.P.A) huku Joseph Melinyo, kiongozi wa kwanza wa chama hicho akiwa mpinzani wa White Settlers.

Kwa hivyo, nyingi za jamii za ushiriks ziliundwa ndani ya vituo vilivyoanzishwa vya machifu.

Na baadhi yao walipewa ardhi na “Mangi” (Kiongozi wa Jadi).

Baada ya muda, zao hilo lilienea katika eneo lote za jamii hizi zilihudumiwa na KNCU.

Vijiji vingi vya miteremko ya Mlima Kilimanjaro vilikuza kahawa na kahawa ikawa zao la jadi kwa Wachaga.
 
Historia ya Wachagga imeandikwa sana. Ukiisoma ndiyo utafahamu kwa nini Wachaga kuna wasomi na matajiri wengi kuliko makabila mengine.
 
Mzee historia ya wachagga umegusa sehem ndogo sana tena ukitaka kirama ajulikane katika historia za wachagga yumo. Kama wewe ni mwanahistoria huwez kuanza alipokuja mzungu mzee. Utaanzia nyuma watu wametoka wapi waliishi vip, ilikuwaje wakawa hapo na tawala na mawasiliano. Sasa unakuta mtu anakomaa history historia kumbe ana hadithi za babu zake hapo gerezan
 
Mzee historia ya wachagga umegusa sehem ndogo sana tena ukitaka kirama ajulikane katika historia za wachagga yumo. Kama wewe ni mwanahistoria huwez kuanza alipokuja mzungu mzee. Utaanzia nyuma watu wametoka wapi waliishi vip, ilikuwaje wakawa hapo na tawala na mawasiliano. Sasa unakuta mtu anakomaa history historia kumbe ana hadithi za babu zake hapo gerezan
Kitali,
Umesema kweli kabisa.

Historia ya Rajabu Ibrahim Kirama ni sehemu ndogo katika historia ya Wachagga.

Historia kubwa ni historia ya baba yake Muro Mboyo rudi nyuma kwa babu zake ambao ndiyo walikuwa majemadari wa vita jeshi la Mangi katika utawala wa Wamachame.

Jeshi hili na mengine ya watawala wa Wachagga lilivunjwa na Wajerumani walipoingia Kilimanjaro.

Kitu kilichompa umaarufu Rajabu Ibrahim Kirama ni kwa yeye kusilimu katika miaka ya 1930s na kwa mara ya kwanza kuuingiza Uislam Machame Nkuu.

Kitendo hiki kilizua ugomvi mkubwa baina yake na Chief Abdiel Shangali.

Kisa hiki nimekieleza kwa kirefu kitabuni.
 
Mzee wangu Ahmed kweli umaarufu wa mtu ni kwa sababu ya kusilimu?
Ndoto,
Hapana kusilimu hakuwezi kumfanya mtu akawa maarufu.

Rajabu Ibrahim Kirama kasilimu mahali ambapo hapakuwa na Muislamu hata mmoja.

Baada ya kusilimu akajenga msikiti na shule.

Kisha akafunga safari hadi Zanzibar kuleta walimu kusomesha Qur'an.

Wachagga wa Machame wakaanza kuingia katika Uislam na kuwapeleka watoto wao kusoma Muslim School ya Nkuu.

Shule hii ipo hadi leo halikadhalika msikiti.

Haya ndiyo yaliyompa umaarufu mkubwa Rajabu Ibrahim Kirama.
 
Mzee historia ya wachagga umegusa sehem ndogo sana tena ukitaka kirama ajulikane katika historia za wachagga yumo. Kama wewe ni mwanahistoria huwez kuanza alipokuja mzungu mzee. Utaanzia nyuma watu wametoka wapi waliishi vip, ilikuwaje wakawa hapo na tawala na mawasiliano. Sasa unakuta mtu anakomaa history historia kumbe ana hadithi za babu zake hapo gerezan
Kitali,
Nakushauri usome kitabu kwanza ndiyo utakuwa katika hali ya kufanya mjadala.

Huwezi kujadili kitu usichokijua.

Historia ya ukoo wa Nkya ambao ndiyo anatoka Rajabu Kirama inakwenda nyuma miaka 300 na wameweza kuhifadhi historia hii kutoka kizazi kimoja hadi kingine.

Baada ya kuingia wamishionari Uchaggani na kufungua shule historia hii iko katika nyaraka zinakwenda nyuma miaka 100.

Nimesoma nyaraka hizi katika utafiti wangu na ndiyo zilizojenga msingi wa Mimi kumjua Rajabu Kirama na nyakati zake.
 
La
Kitali,
Nakushauri usome kitabu kwanza ndiyo utakuwa katika hali ya kufanya mjadala.

Huwezi kujadili kitu usichokijua.

Historia ya ukoo wa Nkya ambao ndiyo anatoka Rajabu Kirama inakwenda nyuma miaka 300 na wameweza kuhifadhi historia hii kutoka kizazi kimoja hadi kingine.

Baada ya kuingia wamishionari Uchaggani na kufungua shule historia hii iko katika nyaraka zinakwenda nyuma miaka 100.

Nimesoma nyaraka hizi katika utafiti wangu na ndiyo zilizojenga msingi wa Mimi kumjua Rajabu Kirama na nyakati zake.
Labda nikusaidie labda kwa wasiotaka kufuatilia historia zao. Kwa mchagga yeyote historia yake ina zaid ya miaka mia nne coz yapo mashina yote yenye kuonyesha namna ukoo ulivyoanza mpaka na huyu mmiliki wa huo ukoo alivyouanzisha na umashuhur wake pale kijijin. So kupata historia ya kirama miaka hiyo sio yeye tu kila mtu uchaggan iko hivyo. Mwambie yeyote mchagga afanye utafiti koo zilianzaje. Na wale wazee walikuwa na shule kwa vijana ambazo ni alama kwa kwa kutumia fimbo. So hiyo umechukua history ya mtu ukaifanya ya wachagga. Pili miaka hiyo mangi ndio alikuwa mtawala na jaji so ukitaka chochote lazima uende kwa mangi so Kirama kwenda kwa mangi kudai kitu ni suala la kawaida kwa raia wa wakati huo sio jambo kuubwa. Mi Babu mzaa Babu yetu alikuwa nchili wa mangi Sina yaan mshaur so sikuambii vitu kwa kubahatisha. Nikipata muda nitakuwekea hapa namba ya mtu anaeuza kitabu cha historia halisi ya uchaggan. Kiuchumi kijamii na kisiasa. Acha hiyo yako ya kirama. Chagga land lilikuwa taifa kabisa Mzee sio hizo porojo zako za kuchagua cha kuandika. Tatizo lako unachagua pa kufanyia historia na watu wa kukupa historia. Hufanyi tafiti. Fanya jumla ya Mambo yote. Wachagga walitokea wapi wakafikaje tawala za mangi zilikuwaje kijamii kisiasa nk. Coz kuna mangi wakuu na wadogo. Kuna wachili kuna fumba kite kuna vipengele vingi mno ni kama utawala wa nchi ulivyosasa. Halafu uje shule na malumbo. Miaka hiyo kabla ya wazungu. Halafu mila na destur, miiko, vita na nk. Sasa wewe ukisimama ni kirama kirama kaleta uislam so what. Unajua wachagga walikuwa na baloz ujeruman nyakati za ujeruman inatawala nchi wewe. Na ni vigumu kuwatenganisha wachagga na kanisa maana mpaka kesho mafaili yapo namna kanisa likiwasaidia kupata elim. Japo kabla ya kanisa mfalme wa Zanzibar alikuwa na mahusiano mazur na mamangi maana alikuwa anatuma misfara inapita kwaajili ya biashara zake kiulinz. So kuna mengi hujui wewe endelea kuandika historia ya kirama maana hutakosa wa kumkamata. Lakin kwangu na kukatalia kama mwanzo. Huijui historia ya wachagga. Ungetuelezea hata historia ya Koo kubwa tu ningekuelewa. Na malumbo hivyo tu.
 
kwani yeye amesema ameandika historia yote ya Wachaga?

Jamani hebu kuweni na busara, mtu akiandika kitu haina maana hiyo ndiyo mwisho wa uandishi, atakuja mwingine kuandika kivyengine na kadhalika. Mfano tu, raisi aliyekuwa wa Marekani Abraham Lincoln, au Kennedy mpaka leo historia zao zinaandikwa katika mantiki tafauti tafauti.

Sasa hebu na nyinyi ambao ni wajuaji sana kaeni muandike hicho munachokijua muweze kuchangia kwenye literature ya historia ya Wachaga siyo kupiga kelele na kulalamika tu.
 
La

Labda nikusaidie labda kwa wasiotaka kufuatilia historia zao. Kwa mchagga yeyote historia yake ina zaid ya miaka mia nne coz yapo mashina yote yenye kuonyesha namna ukoo ulivyoanza mpaka na huyu mmiliki wa huo ukoo alivyouanzisha na umashuhur wake pale kijijin. So kupata historia ya kirama miaka hiyo sio yeye tu kila mtu uchaggan iko hivyo. Mwambie yeyote mchagga afanye utafiti koo zilianzaje. Na wale wazee walikuwa na shule kwa vijana ambazo ni alama kwa kwa kutumia fimbo. So hiyo umechukua history ya mtu ukaifanya ya wachagga. Pili miaka hiyo mangi ndio alikuwa mtawala na jaji so ukitaka chochote lazima uende kwa mangi so Kirama kwenda kwa mangi kudai kitu ni suala la kawaida kwa raia wa wakati huo sio jambo kuubwa. Mi Babu mzaa Babu yetu alikuwa nchili wa mangi Sina yaan mshaur so sikuambii vitu kwa kubahatisha. Nikipata muda nitakuwekea hapa namba ya mtu anaeuza kitabu cha historia halisi ya uchaggan. Kiuchumi kijamii na kisiasa. Acha hiyo yako ya kirama. Chagga land lilikuwa taifa kabisa Mzee sio hizo porojo zako za kuchagua cha kuandika. Tatizo lako unachagua pa kufanyia historia na watu wa kukupa historia. Hufanyi tafiti. Fanya jumla ya Mambo yote. Wachagga walitokea wapi wakafikaje tawala za mangi zilikuwaje kijamii kisiasa nk. Coz kuna mangi wakuu na wadogo. Kuna wachili kuna fumba kite kuna vipengele vingi mno ni kama utawala wa nchi ulivyosasa. Halafu uje shule na malumbo. Miaka hiyo kabla ya wazungu. Halafu mila na destur, miiko, vita na nk. Sasa wewe ukisimama ni kirama kirama kaleta uislam so what. Unajua wachagga walikuwa na baloz ujeruman nyakati za ujeruman inatawala nchi wewe. Na ni vigumu kuwatenganisha wachagga na kanisa maana mpaka kesho mafaili yapo namna kanisa likiwasaidia kupata elim. Japo kabla ya kanisa mfalme wa Zanzibar alikuwa na mahusiano mazur na mamangi maana alikuwa anatuma misfara inapita kwaajili ya biashara zake kiulinz. So kuna mengi hujui wewe endelea kuandika historia ya kirama maana hutakosa wa kumkamata. Lakin kwangu na kukatalia kama mwanzo. Huijui historia ya wachagga. Ungetuelezea hata historia ya Koo kubwa tu ningekuelewa. Na malumbo hivyo tu.
La

Labda nikusaidie labda kwa wasiotaka kufuatilia historia zao. Kwa mchagga yeyote historia yake ina zaid ya miaka mia nne coz yapo mashina yote yenye kuonyesha namna ukoo ulivyoanza mpaka na huyu mmiliki wa huo ukoo alivyouanzisha na umashuhur wake pale kijijin. So kupata historia ya kirama miaka hiyo sio yeye tu kila mtu uchaggan iko hivyo. Mwambie yeyote mchagga afanye utafiti koo zilianzaje. Na wale wazee walikuwa na shule kwa vijana ambazo ni alama kwa kwa kutumia fimbo. So hiyo umechukua history ya mtu ukaifanya ya wachagga. Pili miaka hiyo mangi ndio alikuwa mtawala na jaji so ukitaka chochote lazima uende kwa mangi so Kirama kwenda kwa mangi kudai kitu ni suala la kawaida kwa raia wa wakati huo sio jambo kuubwa. Mi Babu mzaa Babu yetu alikuwa nchili wa mangi Sina yaan mshaur so sikuambii vitu kwa kubahatisha. Nikipata muda nitakuwekea hapa namba ya mtu anaeuza kitabu cha historia halisi ya uchaggan. Kiuchumi kijamii na kisiasa. Acha hiyo yako ya kirama. Chagga land lilikuwa taifa kabisa Mzee sio hizo porojo zako za kuchagua cha kuandika. Tatizo lako unachagua pa kufanyia historia na watu wa kukupa historia. Hufanyi tafiti. Fanya jumla ya Mambo yote. Wachagga walitokea wapi wakafikaje tawala za mangi zilikuwaje kijamii kisiasa nk. Coz kuna mangi wakuu na wadogo. Kuna wachili kuna fumba kite kuna vipengele vingi mno ni kama utawala wa nchi ulivyosasa. Halafu uje shule na malumbo. Miaka hiyo kabla ya wazungu. Halafu mila na destur, miiko, vita na nk. Sasa wewe ukisimama ni kirama kirama kaleta uislam so what. Unajua wachagga walikuwa na baloz ujeruman nyakati za ujeruman inatawala nchi wewe. Na ni vigumu kuwatenganisha wachagga na kanisa maana mpaka kesho mafaili yapo namna kanisa likiwasaidia kupata elim. Japo kabla ya kanisa mfalme wa Zanzibar alikuwa na mahusiano mazur na mamangi maana alikuwa anatuma misfara inapita kwaajili ya biashara zake kiulinz. So kuna mengi hujui wewe endelea kuandika historia ya kirama maana hutakosa wa kumkamata. Lakin kwangu na kukatalia kama mwanzo. Huijui historia ya wachagga. Ungetuelezea hata historia ya Koo kubwa tu ningekuelewa. Na malumbo hivyo tu.
Kitali,
Naona umeghadhibika.
Unasema unataka kunisaidia.

Hakika ningeshukuru kama ungetoa msaada kwa kueleza yale ambayo mimi sikuyaandika katika histroria ya Rajab Ibrahim Kirama.

Lakini nikueleze ukweli ili tufahamiane.

Mimi nimeandika vitabu kadhaa katika miradi ya historia ya Oxford University Press Nairobi (2007) na Oxford University Press New York (2011).

Nipo pia katika Cambridge Journal of African History (1998).

Najua ninachokifanya.

Sasa anaehitaji msaada wa kujua historia zinavyoandikwa si mimi bali ni wewe.

Historia ya Wachagga inaanza toka dunia ilipoumbwa lakini mimi nimeandika historia ya Rajabu Ibrahim Kirama aliyefariki mwaka wa 1962 akiwa na umri wa zaidi ya miaka 100.

Kaburi lake lipo hapo Nkuu pembeni ya msikiti aliojenga.

Hivi sasa kwenye ardhi hiyo unajengwa msikiti mkubwa utakaoshinda misikiti yote ya Uchaggani.

Jina la msikiti huu ni Msikiti wa Mzee Rajabu.

Hiki ni moja ya vielelzo vingi vya umaarufu na umuhimu wa Rajabu Ibrahim Kirama.

Mimi nimeandika historia ya Rajabu Kirama sikuandika historia ya Wachagga.

Kitabu cha Ibrahim Kirama kilizinduliwa Muslim University of Morogoro (MUM).

Nakushauri usome kitabu hiki.
Usijadili kitu ambacho hukijui.

Si busara.

Huna haja ya kunielekeza wapi nitapata vitabu nimekuwa member wa Library of Congress, Washington DC katika miaka ya 1990s kwa kutunikiwa kwa ajili ya utafiti na uandishi wangu.

Unataka kuniletea no. ya simu ya mtu anaeuza vitabu leo.

Ningekushukuru kama ungenipa orodha ya vitabu vya historia ya Wachagga nivitafute nisome.

Nakueleza.

Katika utafiti wa maisha ya Rajabu Ibrahim Kirama nimesoma vitabu vya historia ya Wachagga na nimefika hadi Kidia, Old Moshi kwenye Maktaba ya Kidia Mission.

Hili kuwa Wachagga walikuwa na Ubalozi Berlin wakati wa utawala wa German Ostafrika ndiyo leo nalisikia kutoka kwako.

Nilikuwa Zentrum Moderner Orient, Berlin kwa utafiti.

Hii ni taasisi kubwa duniani katika utafiti wa historia na nimekuta mengi kutoka Tanganyika lakini hili la ubalozi sikujaaliwq kuliona.

Naomba taarifa zaidi ili nifuatilie tupate uhakika.

1715402521804.jpeg

Library of Congress, Washington DC, 2011
1715402596542.jpeg

Zentrum Moderner Orient, Berlin, 2011​
 
Huyu Mzee hajui chochote kuhusu uchagan alichofanya ni kwenda nyumba ya kiislam kuomba kujua uliingiaje ndio akatunga kitabu.
Kitali,
Sikwenda nyumba ya mtu yeyote.
Mimi nilitafutwa kufanya utafiti huu.
 
Umefanya vizur kusema ni historia ya Rajabu Kirama na
Kitali,
Naona umeghadhibika.
Unasema unataka kunisaidia.

Hakika ningeshukuru kama ungetoa msaada kwa kueleza yale ambayo mimi sikuyaandika katika histroria ya Rajab Ibrahim Kirama.

Lakini nikueleze ukweli ili tufahamiane.

Mimi nimeandika vitabu kadhaa katika miradi ya historia ya Oxford University Press Nairobi (2007) na Oxford University Press New York (2011).

Nipo pia katika Cambridge Journal of African History (1998).

Najua ninachokifanya.

Sasa anaehitaji msaada wa kujua historia zinavyoandikwa si mimi bali ni wewe.

Historia ya Wachagga inaanza toka dunia ilipoumbwa lakini mimi nimeandika historia ya Rajabu Ibrahim Kirama aliyefariki mwaka wa 1962 akiwa na umri wa zaidi ya miaka 100.

Kaburi lake lipo hapo Nkuu pembeni ya msikiti aliojenga.

Hivi sasa kwenye ardhi hiyo unajengwa msikiti mkubwa utakaoshinda misikiti yote ya Uchaggani.

Jina la msikiti huu ni Msikiti wa Mzee Rajabu.

Hiki ni moja ya vielelzo vingi bya umaarufu na umuhimu wa Rajabu Ibrahim Kirama.

Mimi nimeandika historia ya Rajabu Kirama sikuandika historia ya Wachagga.

Kitabu cha Ibrahim Kirama kilizinduliwa Muslim University of Morogoro (MUM).

Nakushauri usome kitabu hiki.
Usijadili kitu ambacho hukijui.

Si busara.

Huna haja ya kunielekeza wapi nitapata vitabu nimekuwa member wa Library of Congress, Washington DC katika miaka ya 1990s kwa kutunikiwa kwa ajili ya utafiti na uandishi wangu.

Unataka kuniletea no. ya simu ya mtu anaeuza vitabu leo.

Ningekushukuru kama ungenipa orodha ya vitabu vya historia ya Wachagga nivitafute nisome.

Nakueleza.

Katika utafiti wa maisha ya Rajabu Ibrahim Kirama nimesoma vitabu vya historia ya Wachagga na nimefika hadi Kidia, Old Moshi kwenye Maktaba ya Kidia Mission.

Hili kuwa Wachagga walikuwa na Ubalozi Berlin wakati wa utawala wa German Ostafrika ndiyo leo nalisikia kutoka kwako.

Nilikuwa Zentrum Moderner Orient, Berlin kwa utafiti.

Hii ni taasisi kubwa duniani katika utafiti wa historia na nimekuta mengi kutoka Tanganyika lakini hili la ubalozi sikujaaliwq kuliona.

Naomba taarifa zaidi ili nifuatilie tupate uhakika.

View attachment 2987380
Library of Congress, Washington DC, 2011
View attachment 2987382
Zentrum Moderner Orient, Berlin, 2011​
Umefanya vizur kusema ni historia ya kirama na sio ya wachagga so jitahd kama unataka kuwa mwanahistoria utenganishe historia ya dini na jamii au historia ya mtu na jamii. Kwenda kutoa mhadhara vyuo flan flan Europe haikupi uhalali wa kupotosha.
 
Umefanya vizur kusema ni historia ya Rajabu Kirama na

Umefanya vizur kusema ni historia ya kirama na sio ya wachagga so jitahd kama unataka kuwa mwanahistoria utenganishe historia ya dini na jamii au historia ya mtu na jamii. Kwenda kutoa mhadhara vyuo flan flan Europe haikupi uhalali wa kupotosha.
Kitali,
Sipendi kujibizana na mtu ambaye tayari nimeshamtambua.

Sijisikii raha hata kidogo kumuona mwenzangu anafedheheka na mimi niwe ndiyo sababu ya fedheha yake.

Najua unataka kujikosha.

Ushatambua kuwa mtego wako umenasa chui.

Huwezi kuusogelea mtego wako.

Lakini unashindwa hata kurudi kimya kimya kinyumenyume.

Unaona aibu.
Jibu lililokupa limekutosha.

Ati nimefanya vizuri kusema ni historia ya Rajabu Kirama.

Kwani uliposoma post yangu hukusoma wala hukuona picha ya kitabu?

Ati nitenganishe historia ya dini na jamii?

Umepata wapi kuwa historia ya dini haiwezi kuandikwa na historia ya jamii?

Unadhani catalogue ya kitabu cha Rajabu Kirama imeaandikwa nini?

''History, Chagga, Islam.''

Ushamsoma Bergen (1981) na Sivalon (1992)?

Ati napotosha.

Ukivukwa nguo unachutama.
 
Nje ya mada, naomba kufahamu machache kukusu mkuu...
Mzee wetu Mohamed Said una umri gani?
Unawezaje kuhimili mihemko(matusi, kejeli, dharau na dhihaka) ya vijana mitandaoni, hasa hapa JF??

Nini malengo yako juu ya hizi historia unazoandika hapa jf?
Je unataka hizi historia zisaidie kwa namna gani hii jamii.?

Ulishakumbata na upinzani wowote kisheria ama kutofautiana na serikali ya nchi yoyote juu ya vitabu na makala zako za historia, hasa kwa kuuhusisha uislam??

kuna yeyote anaefuata nyayo zako juu ya kufukukunyua historia,?

Swali la nyongeza, kuna mtu anakusaidia kutype, kwa umri wako wenzio wengi kutype kwa simu ni changamoto achilia mbali pc.
Wewe unaandika bila kukosea hata herufi, ipi siri ya mafanikio.?

Nb. Kama kuna link naweza kujibiwa haya maswali(labda ulifanya interview au uliandika makala nk), ila ningependa iwe maelezo tu na sio video.
 
Nimekuwa na kawaida siku hizi kuwa ninaposoma Makala ya historia basi huenda kwenye kazi zangu zilizopita na kuangalia nini nimeandika.

Ndugu yangu Abdulkarim Ally ameandika makala (haipo hapa) iliyonivutia sana kuhusu siasa za Uchaggani wakati wa ukoloni.

Imesadif kuwa mimi nilitafiti na kuandika kitabu kuhusu maisha ya Rajabu Ibrahim Kirama kutoka Nkuu, Machame.

Katika maisha ya Mzee Rajabu ambae alizaliwa miaka ya mwishoni 1800 na kufariki mwaka wa 1962 maisha yake yaliingiliana na watu ambao

Abdulkarim Ally kawataja katika makala yake.
Abdulkarim kamtaja Sir Charles Dundas.

Nimemweleza Charles Dundas kwa maneno haya:

Charles Dundas:

‘’Historia ya Wachagga imeandikwa kwenye upeo wa hali ya juu na Wazungu kiasi cha kumstaajabisha msomaji.

Inawezekanaje kwa Mzungu kutoka Ulaya mtu mgeni kuijua historia kwa undani wa kiasi kuweza kueleza mambo yaliyotokea miaka mingi sana iliyopita.

Mwandishi Mwingereza Charles Dundas ameandika historia ya Wachagga kwa kiwango cha kustaajabisha.

Charles Dundas ameelezea mengi ambayo mtu hupata tabu hata kuyafikiri achilia mbali kuyajua hadi awe ameyasoma.

Wachagga wana hulka pale wanapompenda mgeni basi watampa lakabu inayoendana na heshima ya kabila lao.

Charles Dundas walimwita, Wasaoye-o-Wachagga, yaani Mzee wa Kichagga.’’

Joseph Merinyo:

‘’Kaka yake jina lake Ngulelo waliochangia mama mmoja akawa Mangi wa Machame na Ngulelo alitawala hadi 1916 na ulipofika mwaka wa 1917 Waingereza wakamtoa kuwa Mangi wakampeleka uhamishoni Kismayu, Somaliland.

Taarifa nyingine zinasema alipelekwa Lamu, Kenya na kuwekwa kifungoni hapo kisiwani.

Waingereza wakamweka Joseph Merinyo kushika nafasi ile kwa muda.
Joseph Merinyo ana historia ya pekee katika siasa za Wachagga.

Joseph Merinyo alikuwa amesafiri hadi Ujerumani wakati huo akifanya kazi kwa Mjerumani ambaye ndiye aliyemchukua hadi Ulaya.

Kwa miaka ile kwa Mwafrika kufika Ulaya ilikuwa ni elimu tosha.

Joseph Merinyo akaja kuwa mkulima wa kahawa katika wakulima wa mwanzo Uchaggani kuingia katika kilimo hicho na alitajirika.

Mchagga mwingine aliyekuwa mkulima wa kahawa nyakati zile alikuwa Petro Njau.

Ngulelo alipokuwa kifungoni ndiyo akasilimu na kuwa Muislam akachagua jina la Selemani.

Ngulelo akawa Muislam wa kwanza katika ukoo wa machifu wa Kichagga.

Aliporudi kutoka kifungoni Ngulelo sasa akijulikana kama Mangi Selemani akaishi Machame mahali panaitwa Ng’ambo kwa kuwa kufika huko ilikuwa lazima uvuke bonde.

Inasemekana kuwa alipokuwa mtawala wa Machame Ngulelo hakuwa na uhusiano mzuri na Wamishionari ambao walikuwa wamedekezwa sana chini ya utawala wa Shangali.’’

Wapo wengi aliowataja Abdulkarim Ally ambao wako katika kitabu hicho hapo chini.

Hapa nimeweka machache kiasi.

View attachment 2986173

Alichoandika Abdulkarim Ally:

Mr A. L. B. (Ben) Bennett DFC.( Distinguished Flying Cross) Alikuwa Rubani Wa Ndege za kivita katika Jeshi la Anga la Uingereza Royal Air force katika wakati Wa vita ya Kwanza ya Dunia .

Mwaka 1927 A. L. B. (Ben) Bennett DFC pichani, rubani wa kivita katika Vita vya Kwanza vya Dunia kutoka Uingereza alifika Kilimanjaro kama Afisa Kazi.

Kwa kushirikiana na Sir Charles Dundas aliekuwa Mkuu Wa wilaya ya Moshi walisaidia wazawa kuunda Umoja wao kwa mujibu wa kanuni za ushirika ambazo zilisisitiza haja ya kuwa na Vyama vya Ushirika vya Msingi.

1932 Vyama vya msingi 11 vilisajiliwa, ambavyo ni Kibong’oto, Uru Central, Kilema, Kibosho Central, Kibosho East, Kibosho West, Machame Central, Mamba, Tarakea, Mkuu Rombo, and Useri.

Uundaji wa Vyama hivi vya Msingi ulifungua njia ya kuanzishwa kwa Kilimanjaro Native Cooperative Union kwa mujibu wa sheria ya Ushirika.

Kahawa ilipandwa kwa mara ya kwanza huko Kilema na Wamisionari Wakatoliki mwaka 1898, na baadaye Walowezi wa Ujerumani.

Wenyeji wa Kilimanjaro hawakuruhusiwa kupanda kahawa badala yake walifanya kazi kwenye mashamba ya Settlers.

Ilikuwa hadi mwisho wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia mwaka 1918 ambapo Ujerumani ilishindwa vita hivyo ikapoteza makoloni yake ikiwa ni pamoja na Tanganyika ya wakati huo.

Mwanzilishi wa Vyama vya Wazawa wa Kilimanjaro alikuwa wakati huo Mkuu wa Wilaya ya Moshi wa kwanza Mwingereza Sir Charles Cecil Farquharson Dundas (1884 - 1956) aliwaruhusu wazawa kulima kahawa kama zao la biashara.

Alieneza uzalishaji wa kahawa katika eneo hilo, na akapewa jina la Wasaoye-o-Wachagga (Mzee wa Wachagga) na Arthur Bennett akapewa Jina la heshima la Mbuya -o- Wachanga yaani Rafiki Wa Wachagga.

Kuruhusiwa kulima kahawa wenyeji walipata mbegu kutoka kwa makanisa ambako kahawa ilikuzwa.

Walipanda mazao lakini hawakuwa na ujuzi wa zao hilo.

Vita vya Kidunia vilikuwa vimesababisha uhitaji mkubwa wa kahawa huko Uropa kwa hivyo wanunuzi wengi walikuwa walowezi wa kizungu wanaoiuza nje. Wenyeji walitumia ndoo, mifuko na njia nyinginezo kubebea kahawa kwa walowezi.

Machafuko ya kijamii na kiuchumi yaliyoletwa na White Settlers na wafanyabiashara wa Asia wakati wa biashara yaliwalazimisha wakulima wadogo kuanzisha vyama vya ushirika kwa ajili ya ukombozi wa kijamii na kiuchumi.

Mwaka 1925 wenyeji waliunda Kilimanjaro Native Planters Association (K.N.P.A) huku Joseph Melinyo, kiongozi wa kwanza wa chama hicho akiwa mpinzani wa White Settlers.

Kwa hivyo, nyingi za jamii za ushiriks ziliundwa ndani ya vituo vilivyoanzishwa vya machifu.

Na baadhi yao walipewa ardhi na “Mangi” (Kiongozi wa Jadi).

Baada ya muda, zao hilo lilienea katika eneo lote za jamii hizi zilihudumiwa na KNCU.

Vijiji vingi vya miteremko ya Mlima Kilimanjaro vilikuza kahawa na kahawa ikawa zao la jadi kwa Wachaga.
Dundas hakuwa Muingereza bali Muskochi yaani Scottish!
 
Mma...
Umri wangu miaka 72.

Mtu akinikejeli au Kunitukana huwa namkwepa nasitisha mjadala na yeye.

Lengo langu kuandika JF ni kusomesha jamii yetu historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika na mchango wa Waislam katika kuunda TANU.

Nilipishana na Marekani kuhusu ugaidi na wakaniorodhesha kama, "terrorist sympathiser" na pasi yangu ikawekewa alama ya siri ili nitambulike uwanja wa ndege wa nchi ninayoingia.

Hiki ni kisa kirefu na iliyoniponza ni mada niliyotoa University of Ibadan, Nigeria mwaka wa 2007 kuhusu Tanzania na suala la ugaidi.

Marekani ilileta taarifa zangu nyumbani na nikakamatwa baada ya muda uwanja wa ndege nikitokea Iran kwenye mkutano.

Sijui kama kuna mtu anaefuata nyayo zangu.

Nikimaliza kuandika nasoma na kusahihisha makosa.
 
Back
Top Bottom