"Wabunge wote nitashirikiana nao hata na hako kanakotokana na CHADEMA (Kasuku Bilago) katakuwemo tu, ila Buyungu siku nyingine mchague vizuri, huyu mbunge ananiomba maji kama ana uwezo si alete yeye? Miradi yote inaletwa na CCM" JPM, Kakonko, 21/07/2017.
"Zitto ni mpinzani lakini anapenda maendeleo. Na mimi nitaleta maendeleo kwa sababu mbunge wenu anachapa kazi, hachapi maneno. Tatizo la maji hapa litakuwa historia" JPM, Kigoma, 22/07/2017.
MyTake:
Wabunge wawili, tena wote wa upinzani. Mmoja anabaguliwa, anadhihakiwa, anabezwa hadharani na kuitwa "ka mbunge ka Chadema", mwingine anasifiwa na kuitwa "mchapakazi, anayependa maendeleo". Halafu mtu huyohuyo anaomba aombewe na kusema anapenda haki na usawa. Anyway Mungu yupo.!!