Wabunge wote nitashirikiana nao hata na hako kanakotokana na CHADEMA

Wabunge wote nitashirikiana nao hata na hako kanakotokana na CHADEMA

"Wabunge wote nitashirikiana nao hata na hako kanakotokana na CHADEMA (Kasuku Bilago) katakuwemo tu, ila Buyungu siku nyingine mchague vizuri, huyu mbunge ananiomba maji kama ana uwezo si alete yeye? Miradi yote inaletwa na CCM" JPM, Kakonko, 21/07/2017.

"Zitto ni mpinzani lakini anapenda maendeleo. Na mimi nitaleta maendeleo kwa sababu mbunge wenu anachapa kazi, hachapi maneno. Tatizo la maji hapa litakuwa historia" JPM, Kigoma, 22/07/2017.

MyTake:
Wabunge wawili, tena wote wa upinzani. Mmoja anabaguliwa, anadhihakiwa, anabezwa hadharani na kuitwa "ka mbunge ka Chadema", mwingine anasifiwa na kuitwa "mchapakazi, anayependa maendeleo". Halafu mtu huyohuyo anaomba aombewe na kusema anapenda haki na usawa. Anyway Mungu yupo.!!
Zitto ana damu ya Burundi Magufuli ya Rwanda connect the dots.
 
Maneno ya KIBAGUZI hapo angelisema mwingine maneno kama "....... hako kanakotokana na CHADEMA (Kasuku Bilago) katakuwemo tu, ila Buyungu siku nyingine mchague vizuri, huyu mbunge ananiomba maji kama ana uwezo si alete yeye? Miradi yote inaletwa na CCM" JPM, Kakonko, 21/07/2017.

Simpingi Mtukufu Mkuu wetu wa nchi ila sitaki kuamini kwamba CCM ndio pekee wanaolipa KODI ambazo zinaleta maendeleo ya nchi yetu adhimu. MKUU ANGELIFUTA VYAMA LIBAKI LICCM PEKE YAKE ili tupate fursa za kunyamaza tukijua hakuna tena demokrasia wala katiba inayoviunda vyama na utashi wa kukosoana.


Kweli mkuu
 
mpaka kufika 2020 tutakuwa tumesikia mengi ya ajabu kutoka kwa watu tuliokuwa tunawategemea kutuletea maendeleo
 
Kama hii kauli imetolewa na rais, basi ningeshaur tuwe na Magogoni Modern Taarabu kabisa manake, najisikia aibu kama kweli rais wa nchi aliongea kauli ya hovyo namna hii!!! Halafu wakitokea watu wakamtolea lugha chafu na maudhi, wanatokea wapumbavu wengine wanasema eti Rais anapaswa kuzungumziwa kwa staa wakati yeye mwenyewe ulimi wake umekosa staa!!!

Ingawaje sheria inataka Rais aheshimiwe lakini assumption ni kwamba Rais mwenyewe atakuwa ni mtu wa kuheshimu watu wake. Kauli ni moja ya heshima za Kiafrika. Huwezi kuita mwanadamu mwenzako anayestahili utu na kuheshimiwa eti "hako...!"
Karma inasema "positive attracts positive" and "negative attracts negative".
 
Kwa maneno kama hayo huoni Lissu kukaa ndani ni uonevu na matumizi mabaya ya madaraka. Ni vizuri kaongea haya sasa wakati Lissu yupo ndani ili watetezi wa mkulu waje watuambie hiyo lugha anayotumia mkuu iko kundi la mtakatifu nani. Mbona hatuoni makamu wa rais au waziri mkuu wakijibiwa kwa kejeli?

Cc: nyani ngabu, jingalao, wakudadavua
 
JPM anaongea as if kuwatumikia wananchi wa maeneo ya upinzani ni favour! In wajibu wake kuwatumikia wananchi wote bila kuangalia wananchi hao walimpigia nani kura.
 
Kiuhalisia muda flani mkulu hatumii busara! hayo sio maneno ya kuongea kwa kiongozi mkubwa wa nchi!!

Kwa haraka naona...

1. Dharau

2. Uchama

3. na kauli za kuleta utengano katika jamii!!

Nadhani ningekua huyo mbunge nisinge kaa kimya, hapo hapo ningempa ukweli wake!!!

Magufuli anajitahidi kama rais ila ni vyema akaangalia kauli zake kwa watanzania!!
Kama watu wenye akili timamu wataendelea kutarajia kauli bora zaidi ya aina hiyo toka kwa sizo basi watambue kumekucha na ndoto zao haziwezi kuendelea!
 
Umenukuu maneno mwenyewe halafu unashindwa kabisa kuyaelewa!!! Kuna maneno gani ya Ubaguzi hapo? "hata hako ka Chadema nitashirikiana nako" hapa kwanza amemsifia mbunge wa Chadema kwa kutumia kiambishi pendezeshi cha "Ka"

Lakini ili huyo mbunge anayemsifia kwa kutumia kiambishi pendezeshi cha "ka" asilewe sifa, akaamua kumweka wazi kuwa japo atashirikiana nae lakini siku nyingine asirudie kuwadanganya Raia kuwa ana uwezo wa kuleta maji wakati uwezo huo hana.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
IMG_9870.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu ibariki Tanzania na umpe kauli thaabit Rais kwa maana hakuna kiongozi aliechaguliwa na watu wake akawa na kauli chafu na za kuudhi kiasi hicho pia uwape hekima viongozi wa dini wale ambao wanapoongea maneno machafu viongozi wa kiserikali wanajichekesha kwa uoga ila yanapotolewa maneno makali dhidi ya viongoz hao bas wanatumia hata misiba kuwanyooshea vidole wazungumzaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Wabunge wote nitashirikiana nao hata na hako kanakotokana na CHADEMA (Kasuku Bilago) katakuwemo tu, ila Buyungu siku nyingine mchague vizuri, huyu mbunge ananiomba maji kama ana uwezo si alete yeye? Miradi yote inaletwa na CCM" JPM, Kakonko, 21/07/2017.

"Zitto ni mpinzani lakini anapenda maendeleo. Na mimi nitaleta maendeleo kwa sababu mbunge wenu anachapa kazi, hachapi maneno. Tatizo la maji hapa litakuwa historia" JPM, Kigoma, 22/07/2017.

MyTake:
Wabunge wawili, tena wote wa upinzani. Mmoja anabaguliwa, anadhihakiwa, anabezwa hadharani na kuitwa "ka mbunge ka Chadema", mwingine anasifiwa na kuitwa "mchapakazi, anayependa maendeleo". Halafu mtu huyohuyo anaomba aombewe na kusema anapenda haki na usawa. Anyway Mungu yupo.!!

Dua la kuku halimpati mwewe.
 
Kiuhalisia muda flani mkulu hatumii busara! hayo sio maneno ya kuongea kwa kiongozi mkubwa wa nchi!!

Kwa haraka naona...

1. Dharau

2. Uchama

3. na kauli za kuleta utengano katika jamii!!

Nadhani ningekua huyo mbunge nisinge kaa kimya, hapo hapo ningempa ukweli wake!!!

Magufuli anajitahidi kama rais ila ni vyema akaangalia kauli zake kwa watanzania!!
 
Hahahahaha, Daa Mkulu ni noma. Hotuba hizo zinachekesha sana. Anakwambia "Zitto anachapa kazi na hachapi maneno" hivi ni nani aliyesema kuwa magufuli siyo mwana siasa? Magufuli mbali ya kuwa Rais lakini ni mwana siasa. acheni afanye siasa bana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nitafurahi siku akisema sitaki kutuona huto tukodi twa wapinzani kwenye serikali yangu. Hii itahalalisha ccm kujivunia kutumia kodi zake kuleta maendeleo.
 
Back
Top Bottom