Wabunge wetu wa CCM na maigizo Bungeni

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,468
23,745
Utawaona baadhi wanatokwa povu, wanatokwa jasho, wanawaka hasa kukemea ubadhirifu uliobainishwa na CAG. Wakimaliza mjadala maisha yanaendelea kama kawaida.

Wanasubiri tena mwaka ujao. Napo watawaka sana na kutokwa jasho, kisha maisha yanataendelea mpaka mwaka ujao. Haya ni maigizo tu yasiyo na tija kwa taifa.

Mimi nashauri kusiwe na CAG kabisa maana anatumia tu pesa akitoa report yake hakuna kinachofanyiwa kazi. Business as usual. Watanzania wanaendelea kuibiwa tu na viongozi hawa hawa ambao hawawezi kufikiri kuwasaidia watanzania zaidi ya kuwakandamiza zaidi. Na tozo zisizo na kichwa wala miguu.
 
Ufisadi sio wizi wa fedha tu,hats wizi was kura ni ufisadi tu! Sasa ni mbunge gani wa CCM anaweza kukemea ufisadi. Kama yuko serious basi huyo atakuwa anaaga bungeni maana 2025 watamkaanga Kwa mafuta yake mwenyewe!
 
Ufisadi sio wizi wa fedha tu,hats wizi was kura ni ufisadi tu! Sasa ni mbunge gani wa CCM anaweza kukemea ufisadi. Kama yuko serious basi huyo atakuwa anaaga bungeni maana 2025 watamkaanga Kwa mafuta yake mwenyewe!
Halafu ukifuatilia kwa makini majibu ya mawaziri wameishawajulia wote wakijibu"haya ni matokeo mazuri ya nh. Rais kutaka ukaguzi wa wazi " kila ukisikia anayejibu lazima aguse hapo kwa namna yake utafikiri wamekaririshwa, na wao wakisikia hilo wanaanza tumsaidie rais wanaishiwa upepo kabisa.
 
Back
Top Bottom