Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,468
- 23,745
Utawaona baadhi wanatokwa povu, wanatokwa jasho, wanawaka hasa kukemea ubadhirifu uliobainishwa na CAG. Wakimaliza mjadala maisha yanaendelea kama kawaida.
Wanasubiri tena mwaka ujao. Napo watawaka sana na kutokwa jasho, kisha maisha yanataendelea mpaka mwaka ujao. Haya ni maigizo tu yasiyo na tija kwa taifa.
Mimi nashauri kusiwe na CAG kabisa maana anatumia tu pesa akitoa report yake hakuna kinachofanyiwa kazi. Business as usual. Watanzania wanaendelea kuibiwa tu na viongozi hawa hawa ambao hawawezi kufikiri kuwasaidia watanzania zaidi ya kuwakandamiza zaidi. Na tozo zisizo na kichwa wala miguu.
Wanasubiri tena mwaka ujao. Napo watawaka sana na kutokwa jasho, kisha maisha yanataendelea mpaka mwaka ujao. Haya ni maigizo tu yasiyo na tija kwa taifa.
Mimi nashauri kusiwe na CAG kabisa maana anatumia tu pesa akitoa report yake hakuna kinachofanyiwa kazi. Business as usual. Watanzania wanaendelea kuibiwa tu na viongozi hawa hawa ambao hawawezi kufikiri kuwasaidia watanzania zaidi ya kuwakandamiza zaidi. Na tozo zisizo na kichwa wala miguu.