Wabunge wanaendelea kupokea mishahara

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
Jamani nimesoma kwenye magazeti kuwa wabunge waliomaliza muda wao bado wanapokea mishahara na posho zao kama kawaida wakati bunge limeshavunjwa. Hii imekaaje si ufujaji wa mali ya umma.
 
Hii inawezekana Tanzania tu...:smile-big:
Sidhani kama mahala pengine duniani unaweza kukuta majitaka ya aina hii yanatendeka!
 
LICHA ya wabunge waliomaliza muda wao baada ya Bunge kuvunjwa kulipwa kiinua mgongo kipatacho Sh milioni 43 kila mmoja na baadhi yao kuacha kutetea nafasi hiyo, imebainika bado wamekuwa wakiendelea kulipwa mshahara na posho kila mwezi.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah, alithibitisha jana kuwa wabunge hao wanaendelea kulipwa mishahara na posho mbalimbali na wanastahili kulipwa wakati huu ambao Bunge limevunjwa na Rais.

Hata hivyo, wachambuzi wa mambo wanadai kuwa kitendo cha mbunge kulipwa mshahara na posho hizo, kinaweza kumfanya akazitumia fedha hizo kuwalaghai wapiga kura wakati wapinzani wake hawana uwezo wa kufanya hivyo kutokana na ufinyu wa rasilimali uliopo.

Dk. Kashilillah alipotakiwa kueleza kwa kina kwa nini wabunge wanastahili kulipwa wakati tayari Bunge limeshavunjwa alisema, “wanaowalipa wabunge ni Hazina kwa hiyo ndio wenye mamlaka ya kuzungumzia suala hilo.”

Alisisitiza kuwa kama ni masuala ya sheria, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) ndiye yuko kwenye nafasi nzuri ya kuyafafanua na kuongeza, “nakushauri uwasiliane na AG atakufafanulia vizuri.”

Rais Jakaya Kikwete kupitia gazeti la Serikali toleo namba 272 la Julai 28, alitoa tamko la kulivunja Bunge kuanzia Agosti mosi siku chache kabla ya uteuzi wa wagombea udiwani, ubunge na urais kufanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Baada ya tangazo hilo, majimbo yote yalikuwa wazi hivyo kutoa fursa ya Watanzania wenye sifa kujitokeza kugombea ubunge kupitia vyama mbalimbali vya siasa vilivyo na usajili wa kudumu.

Mwanasheria Mkuu Jaji Frederick Werema alipoulizwa alisema Katiba ya nchi inatamka kuwa uhai wa Bunge ni miezi 60 hivyo wabunge wanastahili kulipwa mishahara kwa kipindi hicho kilichotajwa kwenye Katiba.

“Mishahara kwa wabunge ni lazima iendelee kulipwa na huu sio ufisadi,” alisema Jaji Werema na kuongeza kuwa, “Wanalipwa kwa vile bado wanafanya kazi katika maeneo yao.”

Alipoulizwa kwa nini walipwe mishahara wakati tayari shughuli za Bunge zimeshakoma alisema,“hiyo ni ‘advantage’ (faida) kwao kwani malipo hayo yanatambulika kisheria.”
“Unakuta watu wanalalamika eti kwa nini Rais anatumia magari ya Serikali, ni lazima atumie kwa kuwa yuko madarakani na hiyo ndio ‘advantage’ yake,” alisema Jaji Werema.

Aliongeza kuwa sheria nyingine inayowafanya wabunge waendelea kulipwa mishahara ni Sheria ya Maslahi ya Wabunge ambayo inaeleza kuwa ubunge unakoma baada ya kulitumikia Bunge kwa miezi 60.

Mwanasheria huyo alisema kibaya ni kwa Wabunge hao kutumia mishahara hiyo kuwarubuni wapiga kura ili wamchague tena.

“Kama kuna wabunge wanaofanya hivyo tutaarifuni kwa kuwa watakuwa wanakiuka sheria.”

Mbunge mmoja ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini, alikiri kuwa wanaendelea kupokea mshahara wao kila mwezi wa Sh milioni mbili na Sh milioni tano ambazo wanalipwa kama posho za jimbo.

Licha ya malipo hayo, mbunge huyo alisema wabunge pia hulipwa posho za mafuta ambayo ni lita 70 kila wiki.

Kutokana na wabunge kupata mishahara na marupurupu, kazi hiyo imevutia watu wengi wakiwemo wasomi wanaofundisha katika vyuo vikuu ambao mara nyingi wamekuwa tayari kuacha kazi zao na kugombea ubunge.

Kabla ya Rais kulivunja Bunge, Hazina iliwalipa wabunge hao mafao yasiyopungua Sh milioni 43 kila mbunge ikiwa ni asilimia 40 ya mshahara wa mbunge huyo aliyelitumikia Bunge kwa miaka mitano.


Source: Habari Leo
 
Mwanasheria Mkuu Jaji Frederick Werema alipoulizwa alisema Katiba ya nchi inatamka kuwa uhai wa Bunge ni miezi 60 hivyo wabunge wanastahili kulipwa mishahara kwa kipindi hicho kilichotajwa kwenye Katiba.

"Mishahara kwa wabunge ni lazima iendelee kulipwa na huu sio ufisadi," alisema Jaji Werema na kuongeza kuwa, "Wanalipwa kwa vile bado wanafanya kazi katika maeneo yao."

Alipoulizwa kwa nini walipwe mishahara wakati tayari shughuli za Bunge zimeshakoma alisema,"hiyo ni ‘advantage' (faida) kwao kwani malipo hayo yanatambulika kisheria."

"Unakuta watu wanalalamika eti kwa nini Rais anatumia magari ya Serikali, ni lazima atumie kwa kuwa yuko madarakani na hiyo ndio ‘advantage' yake," alisema Jaji Werema.

Aliongeza kuwa sheria nyingine inayowafanya wabunge waendelea kulipwa mishahara ni Sheria ya Maslahi ya Wabunge ambayo inaeleza kuwa ubunge unakoma baada ya kulitumikia Bunge kwa miezi 60.
Habari ndo hiyooooooo:becky:
 
Afu sasa cha kushangaza....news kama hizi hazitustui wala nini!
maana watu bado tunaendelea tu kukaa tunasikilizia....mwe!
 
Laiti wanachi wangekua na uchungu na hii nchi haya yote yasingekuwepo!! Millioni 5 + Milioni mbili? hata kama umebwaga ubunge unaendelea kuzipata!! duh!!! Tutaendelea kuitwa mbayuyuwayu mpaka ukamilifu wa Dahari!!:confused2::confused2::confused2:
 
jamani kwani leo ni tarehe moja April.
Mbona mnaleta utani hivi?
Mbunge kuendelea kulipwa wakati ameshamaliza muda wake haiwezekani hata kidogo.
ooh! yes! yes! kwa Tanzania inawezekana bila shaka yeyote.
 
jamani kwani leo ni tarehe moja April.
Mbona mnaleta utani hivi?
Mbunge kuendelea kulipwa wakati ameshamaliza muda wake haiwezekani hata kidogo.
ooh! yes! yes! kwa Tanzania inawezekana bila shaka yeyote.

Umesahau taratibu za nchi yetu nini......
"Proud to be Tanzanian! :becky::becky:"
 
Ndugu Kashililah anaudanganya umma, Hazina hawalipi mpaka wapewe taarifa za kufanya malipo na kwa mantiki hii mpira huu bado upo kwenye ofisi yake Kashililah maana wao ndio wanarekodi za kutambua ni lini ajira za wabunge zinafikia kikomo. Mfumo wa utawala wa nchi kwa kweli umeoza na inasikitisha kusikia mtu mwenye uzoefu na sheria kama Jaji Werema akizungumza vitu vya kipuuzi hivi. Wakati mwingine kama hana jibu ni bora tu aseme "No Comment" au azime simu zake.
 
Ndio maana tunahitaji mabadiliko ya KATIBA itakayokuwa ikiangalia mambo ya wengi na wala sio wachache kama ifanyikavyo sasa,Kama bunge lilivunjwa inamaanisha hatuna wawakilishi kwa kipindi hiki sasa huyo mbunge anapata hizo pesa 2m na laki 5 kwa kazi ipi? Mwanasheria ansema hiyo na faida kweo,huyu ni mwanasheria gani kwani mimi ni mfanyakazi wa serikari ENGINEER msahahara wangu ni laki 405.nakatwa kodi elfu47 na hizo kodi zangu ndio anapewa mbunge ambae hata mda wake wa uwakilishi umeisha nashindwa kuelewa juu ya hii nchi.
TUNAHITAJI MABADILIKO KUANZIA UONGOZI WA JUU MPAKA KATIBA
Dah huyu kaongea kwa uchungu sana!!
 
Hii ndio TZ zaidi ya uijuavyo.Hebu jaribu kutafakari majibu ya afisa wa bunge na manasheria mkuu,ni majibu ya kiburi sana.Kwa hiyo kwa sababu muda wa bunge ni miezi sitini hata ukifa baada ya mwaka mmoja utaendelea kulipwa tu mpaka miaka mitano ipite.Na hizo za maendeleo zinafanyiwa nini sasa au ni za kampeni?Eti serikali haina pesa za kusomesha raia wake bure.Hii nayo inatokea Kenya au Uganda jamani naomba kujua.Hivi kuvunja bunge maana yake nini?
 
Dr Slaa anvyoongelea kuandika katiba mpya watu wanakuwa hawamwelewi anachomaanisha.
Hawa akina Werema na Kashililah wanatumia udhaifu huo kuidhinisha ufisadi kama huu, kuendelea kuwanyonya wananchi wanaolipa kodi.
Tangu lini mtu aliyestaafu kazi yake na kulipwa mafao yake yote (in lump sum), then akaendelea kulipwa na mshahara wake pia.
I mean, this is pathetic- kama walivyosema walionitangulia- only happening in Tanzania!!
I'm out!!
 
Back
Top Bottom