Wabunge wamkalia kooni bosi TANROADS

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Kizitto Noya, Dodoma

KAMATI ya Bunge ya Miundombinu imeitaka serikali kutoa tamko kuhusu tuhuma zinazomkabili mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara (Tanroads), Ephraem Mrema kwamba mkataba wake wa kazi umekwisha.

Mbunge wa viti maalum (CCM), Joyce Masunga, akizungumza kwa niaba ya mwenyekiti wa kamati hiyo Mohammed Missanga, alisema tuhuma hizo zinaathiri ufanisi na utendaji wa Tanroads.
Masunga alisema hayo alipokuwa akiwasilisha maoni ya kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu katika makadirio ya matumizi ya Wizara ya Miundombinu.

“Kamati yangu inasikitishwa sana na malumbano yanayoendelea kwa muda mrefu sasa kuhusu mtendaji mkuu wa Tanroads kwamba mkataba wake wa ajira umekwisha,” alisema Masunga.

“Lakini wakati malumbano hayo yakiendelea, serikali imekaa kimya bila kutoa ufafanuzi na ukweli wa madai hayo yanayoandikwa magazetini siku hadi siku. Kamati ingependa serikali ieleze ukweli wa madai hayo kwani yanaathiri ufanisi na utendaji katika wakala huo.”

Alisema katika kulipatia ufumbuzi suala hilo, kamati iliwakutanisha watendaji wakuu wa wizara, bodi ya Tanroads na Mrema kubaini kama kulikuwa na tatizo, lakini bado mijadala na malumbamo hayo haijakwisha.

Katika mikutano hiyo, Masunga alisema, kamati ilibaini kuwapo kwa makundi yaliyokuwa yakichagizwa na wafanyakazi waliokuwa Tanroads na ambao wamesimamishwa kazi au kumaliza muda wao wa utumishi na wengine hawakuridhika na kuenguliwa kwao katika nafasi zao za uongozi.

“Kamati yangu kwa kutumia busara na ili kuepusha malumbano yasiyo na tija katika kipindi kinachopaswa kukamilisha miradi, iliishauri wizara kukaa pamoja na bodi ya Tanroads na watendaji wake wakuu kujadili masuala yanayowahusu, hasa yale ya mchakato wa kujaza nafasi za watendaji,” alisema.

“Kamati ilishauri kuwa ili miradi isisimame wakati mchakato huo unaendelea, mtendaji mkuu awateue wale wote wanaoshilikia nafasi hizo wakaimu hadi watakapopatikana wa kujaza nafasi hizo kulingana na muundo mpya wa wakala ambao ulishakamilika na kuridhiwa na idara kuu ya utumishi.”

Katika hatua nyingine kamati hiyo ya miundombinu imeelezea kuridhishwa kwake na utendaji wa mkurugenzi huyo kwa kila ilichoeleza kuwa amefanya kazi nzuri tangu aingie madarakani Juni mwaka 2007.

“Wakati anaingia madarakani wakala ulikuwa na miradi 10 tu lakini, sasa kuna mikataba zaidi ya 40. Mabadiliko yalianza kuonekana kwa kasi ikilinganishwa na mtendaji aliyepita,” alisema.


“Mrema alipoanza kazi kulikuwa na mikataba 18 iliyokamilika, miradi 4 alianza nayo yeye na kuikamilisha ambayo ni Kigoma- Kidahwe, Usagara- Sengerema na Masasi- Mangaka,” alisema.
Masunga alitaja miradi mingine iliyokamilika katika kipindi cha uongozi wa Mrema kuwa ni barabara 18 , miradi 10 aliyoirithi kutoka kwa mtangulizi wake na miradi minne kutoka wizarani

“Leo hii ni miradi zaidi ya miradi 54 ya barabara za kitaifa ambayo ameisimamia pamoja na miradi ya madaraja na vivuko kama vile vya Busisi, Kigamboni, Pangani, Kilombero, Utegi na vingine.”

Awali Spika wa Bunge Samuel Sitta alimpa pole mtendaji mkuu huyo wa Tanroads na kumtia moyo kwamba aendelee kuvumilia katika kipindi hicho kigumu cha tuhuma katika utendaji wake wa kazi.

Wabunge wamkalia kooni bosi Tanroads


HAWA WANA WAZIMU? wanahoji na hapo hapo kupongeza!!!!! Huu uchaguzi utatufanya watu tubebeshwe makapi watu wanatafuta fedha za uchaguzi.... Jamani Mwenyekiti Mohamed Misanga, ana gari jipya kabisa!!!!!
 
Hivi hii bajet imepita kweli? ile ishu ya madeni bil 300 imeishia wapi?
 
Hayo ya Tanroads yanatuchosha, mtendaji mkuu bwana Mrema anafahamika wazi ni mvurugaji lakini watu kama akina Misanga wanamkingiia kifua kwa kuwa ni watu weny urojo kwa kuhongwa pesa na bwana huyo Misanga tunamfahamu tangu anaishi chang"ombe ..... ah basi sisemi mengi nanymaza alkini akiendelea kumkingia kifua bwana Mrema atabidi tuseme kama kama tulivyoambia bubu hutaka kusema mambo yanapomzidia.
 
Hayo ya Tanroads yanatuchosha, mtendaji mkuu bwana Mrema anafahamika wazi ni mvurugaji lakini watu kama akina Misanga wanamkingiia kifua kwa kuwa ni watu weny urojo kwa kuhongwa pesa na bwana huyo Misanga tunamfahamu tangu anaishi chang"ombe ..... ah basi sisemi mengi nanymaza alkini akiendelea kumkingia kifua bwana Mrema atabidi tuseme kama kama tulivyoambia bubu hutaka kusema mambo yanapomzidia.

Divele ni aibu nchi yetu, eti Waziri anasema wanachunguza, uchunguzi gani toka 2008? Halafu mtu kama hana sifa kwa mujibu wa tangazo unachunguza nn? kama mkataba unapingana na barua ya uteuzi unahitaji AG akwambie nini hapo na kwa miaka miwili?
 
Mbona naona dalili za chuki kubwa juu ya huyu bwana? Kuna Data zimetolewa kama unataka kupinga si ndiyo mahali pazuri pa kupingia hapo? uonyeshe na wewe data zako ambazo zinakufanya umwone Mrema kama unavyomwona. Tukiendeleza haya mambo ya chuki inayotokana na watu majeruhi wa mfumo na wachache wenye midomo ya kusemea kuchafua watu wengine hatutapiga hatua hata kidogo. Kazi iliyofanyika imetajwa Mzee mwanakijiji tupe data tofauti. Ungekuwa wewe au mtoto wako anaandikwa kila siku na ushahidi hautoki na watu wanataka aondolewe tu basi, ungejisikiaje?

Niliwahi kuandika humu kuwa ni vibaya sana kutumia huu uhuru wetu kutuhumu watu na kupiga kelele za asulubiwe! asulubiwe! wakati hatujawapa haki ya msingi ya kujitetea, na wala hatutaki kusikia kabisa ukweli.

Mimi niko sehemu ambayo napata ukweli wa hili jambo lakini sijawahi hata siku moja kuleteta kauli ya utetezi kwakuwa nilijua wapo watu wa kulijibia, angalao sasa wameanza kuona kuwa wana wajibu wa kutekeleza. Sisi wengine humu tunatakiwa kufanya research ya kutosha kabla hatuaamua kumsulubisha mtu bila kosa lolote.

Respect Wakuu.
 
Mbona naona dalili za chuki kubwa juu ya huyu bwana? Kuna Data zimetolewa kama unataka kupinga si ndiyo mahali pazuri pa kupingia hapo? uonyeshe na wewe data zako ambazo zinakufanya umwone Mrema kama unavyomwona. Tukiendeleza haya mambo ya chuki inayotokana na watu majeruhi wa mfumo na wachache wenye midomo ya kusemea kuchafua watu wengine hatutapiga hatua hata kidogo. Kazi iliyofanyika imetajwa Mzee mwanakijiji tupe data tofauti. Ungekuwa wewe au mtoto wako anaandikwa kila siku na ushahidi hautoki na watu wanataka aondolewe tu basi, ungejisikiaje?

Niliwahi kuandika humu kuwa ni vibaya sana kutumia huu uhuru wetu kutuhumu watu na kupiga kelele za asulubiwe! asulubiwe! wakati hatujawapa haki ya msingi ya kujitetea, na wala hatutaki kusikia kabisa ukweli.

Mimi niko sehemu ambayo napata ukweli wa hili jambo lakini sijawahi hata siku moja kuleteta kauli ya utetezi kwakuwa nilijua wapo watu wa kulijibia, angalao sasa wameanza kuona kuwa wana wajibu wa kutekeleza. Sisi wengine humu tunatakiwa kufanya research ya kutosha kabla hatuaamua kumsulubisha mtu bila kosa lolote.

Respect Wakuu.

Mkuu heshima sana...............

Mrema anafahamika tangu wakati ule wa miradi iliyokuwa chini ya OPM. Hakuna anayemuonea chuki kwa kuwa kwake CEO wa TANROADS....isipokuwa ni kwenye background yake na jinsi alivyoupata huo u-CEO na pia madudu yake kwenye miradi tangu alipoingia pale............

Kufanya miradi hata 100...........does not make sense kama katika hiyo miradi imejaa Rushwa, Cost Overuns, na hasara nyingine za kimikataba.............unaweza ukawa na miradi hata 1000 (depending na contracts amounts) lakini gharama za hasara uliyoingizia Taifa kutokana na miradi michache inaweza kulingana au hata kuzidi hiyo miradi yako 100.......ukiangalia kwa angle za kiuchumi in Detail.........huyu bwana anatakiwa kuwa Keko.................

Kama mnamuona huyu mwema basi akina Mgonja/Mramba/Yona/EL ni Malaika Wakuu..........Watanzania tusipende sana kufumbia macho uozo/kuoneana haya...............mpaka mnafikia kumpongeza huyu bwna Bungeni!!!!!!!!!!!!!!!.........eti mnampa pole..........ONLY IN TANZANIA............
 
Back
Top Bottom