Wabunge wa Upinzani watoka bungeni wakiwa wameziba midomo yao

Hivi hawa ukawa kweli wana akili sawa sawa leo naona wame-edit staili yao ya kutoka bungeni kwa kubandika makaratai kwenye midomo yao sasa sijui hasa walichokuwa wanamaanisha wakati tuliambiwa hakuna aliye wazuia kuingia bungeni ni utashi wao wenyewe

Sasa naanza kuliona kaburi la upinzani 2020 sijui kama watatoboa tena hawa dah kweli za kuambiwa changanya na zako tangu wameaambiwa hawataki kuchanganya zao
Acha kufikiri kama uko ndani ya chupa! Usichojua nini hapa! unahisi wamefunga midomo kwa sababu wamezuiwa kutembea, kula, au kunywa?. Kama wanamaanisha wamezuiwa kuingia bungeni waliingiaje na wanatoka wapi?
 
Mi nawaza mkutano Mkuu wa ccm tarehe 23.07.2016.....wala hawa ukawa hawatupi tabu
 
BUNGENI: Wabunge wa upinzani waziba midomo yao kwa karatasi na utepe na kutoka nje ya Ukumbi wa Bunge wakigomea kushiriki vikao vinavyoongozwa na Naibu Spika.

Hii staili ya leo ya wapinzani kutoka bungeni imenipa maswali mengi sana, imenitisha mpaka namehisi kitu flani hivi hapa nilipo. Hii ni staili mpya kabisa.

Sasa naona tunakoelekea sio kizuri, huu utaratibu wa kufanya maamuzi kwa ubabe mwisho wa siku hua hakuna mshindi. Hii ni aibu kubwa sana ambayo ameipata Naibu spika.Nimtake tu atafute suluhu na wabunge hawa zaidi atazidi kudhalilishwa pasina sababu.



Hawa wote wanamkimbia mtu mmoja?
 
Hivi hawa ukawa kweli wana akili sawa sawa leo naona wame-edit staili yao ya kutoka bungeni kwa kubandika makaratai kwenye midomo yao sasa sijui hasa walichokuwa wanamaanisha wakati tuliambiwa hakuna aliye wazuia kuingia bungeni ni utashi wao wenyewe

Sasa naanza kuliona kaburi la upinzani 2020 sijui kama watatoboa tena hawa dah kweli za kuambiwa changanya na zako tangu wameaambiwa hawataki kuchanganya zao
Kwani una umri gani? Mbona hilo ni jambo la kawaida dunia hii. Kabla ya kuandika jaribuni kutafuta ufahamu kwingine. Ukishindwa uliza ueleweshwe.
 
walishaelewa wenzao wanataka nini sema wamewakazia tu, basi tuombe hii njia ieleweke na bunge lifike muafaka lasivyo kila ujumbe utachukuliwa kama mzaha
 
Natamani DR Tulia aendelee kukalia hicho kiti tu. Ujinga wao utakoma. Walisema Tanzania ilipofikia inataka kiongozi mkali, Mungu katuletea JPM
 
Hawa wabunge kumbe hawana hoja yeyote ya msingi wanayozungumza kwani hata ukimsikiliza mbatia anaongea kwa kushika lile na kurukia lile, mara magufuli anataka fikra zake ziheshimiwe, mara tulia anagandamiza, mara wabunge wa ccm wanatukana wapinzani, mara wakimwaga damu zetuwatoto wetu wapo,

1. Mbatia hakuna mtu mwenye kutaka damu yako wala magufuli hana haja na damu yako acha kutapatapa

2. Tuelezi hoja inayosababisha mtoke nje

3. Kama wabunge wa ccm wamewatukana mswafiche na mseme matusi mliyotukanwa badala ya kugeneralize

3. Mpaka sasa mmeshindwa kujieleza sababu za kutoka nje, badala yake mnatapatapa tuuuuuuuuuuuu, mboye anasema yake, mbatia yake,

4. Elezenezi faida kwa wananch kwa nyie kukaaa nje ya bunge
 
Tulia afute adhabu ya wabunge waliofukuzwa, Zitto aachiwe huru, bajeti ijadiliwe freedom of speech mkulu alegeze kamba vinginevyo serikali itashindwa huko mbele. Hawa watu wawili wapunguze kiburi na kukomoana vinginevyo nchi itawafia mikononi
 
Hii style bwana mmmh...yaani mbatia anaongea kwa hasira kweli kweli...tafsiri hii bwana Ni kwamba bungeni wamezibwa midomo na nnje wamezibwa midomo
 
Hivi hawa ukawa kweli wana akili sawa sawa leo naona wame-edit staili yao ya kutoka bungeni kwa kubandika makaratai kwenye midomo yao sasa sijui hasa walichokuwa wanamaanisha wakati tuliambiwa hakuna aliye wazuia kuingia bungeni ni utashi wao wenyewe

Sasa naanza kuliona kaburi la upinzani 2020 sijui kama watatoboa tena hawa dah kweli za kuambiwa changanya na zako tangu wameaambiwa hawataki kuchanganya zao

Tena I litakuwa wafunike Kabisa midomo na macho....maana hata kuona live Haki imesiginwa
Huyu naibu hatadum Kama Ana KIBUri hivi watamchoka hata CCM ..ni mchanga


H
 
BUNGENI: Wabunge wa upinzani waziba midomo yao kwa karatasi na utepe na kutoka nje ya Ukumbi wa Bunge wakigomea kushiriki vikao vinavyoongozwa na Naibu Spika.

Hii staili ya leo ya wapinzani kutoka bungeni imenipa maswali mengi sana, imenitisha mpaka namehisi kitu flani hivi hapa nilipo. Hii ni staili mpya kabisa.

Sasa naona tunakoelekea sio kizuri, huu utaratibu wa kufanya maamuzi kwa ubabe mwisho wa siku hua hakuna mshindi. Hii ni aibu kubwa sana ambayo ameipata Naibu spika.Nimtake tu atafute suluhu na wabunge hawa zaidi atazidi kudhalilishwa pasina sababu.



Hawa jamaa sasa kwa hii hali ni kama wamechanganyikiwa.
Kwenye dunia ya sasa katika siasa kila kitu kina sheria, ina maana wameshindwa kabisa sheria na naibu spika na kuanza mbinu za kitoto kama hizo?
Maisha sasa ni magum sana kwa wananchi wanavyoona watetezi wao katika hali hiyo wananchi wanakosa tumaini kabisa la maisha.
Wapinzani bungeni jaribuni kubadilika na mipango yenu, sababu tunajua hii nchi serikali bila kupata upinzani imara mambo mengi ya nchi hayawezi kwenda.
 
Kwa mwenendo huu, wa kutafuta sababu za kutowawakilisha wananchi wao, kama wanavyofanya wabunge wa ukawa ni kutengeneza tabaka la kinyonyaji katika Taifa.

Wabunge baada ya kushinda uchaguzi, wanakua wasemaji wakuu wa wananchi Bungeni wakiwawakilisha waliowachagua na wasiowachagua, hilo ndilo jukumu la kwanza kubwa na la msingi sana.

Sioni sababu ya kupeleka matakwa binafsi na ya chama, katika kiti cha mbunge, jambo linalipelekea kushindwa Kutimiza wajibu huu mkubwa.

Wabunge wakumbuke kwamba mishahara wanayopokea ni matokeo ya kodi za wananchi wa Tanzania waliokatwa katika mishahara na biashara zao.

Wabunge hawaoni aibu wala hawaoni kama wanawajibu wa kutimiza majukumu yao. Sidhani kama kila mwananchi anafurahi kuona mbunge wake, aliyemchagua hata kama hajamchagua akiacha kuingia Bungeni kutokana na kutanguliza mbele maslahi ya Chama na matakwa binafsi.

Wabunge wanafanya hivyo makusudi, kwakua hakuna namna ya kuwawajibisha mpaka miaka mitano ipite, wakijua kwamba mpaka hiyo miaka mitano ifike tutakua tumeshasahau kila ovu walilokua wakilifanya kwa kipindi chote walichokua Bungeni.

Jambo la kufanya sasa ni kubadili katiba ili Mbunge asiyetimiza wajibu wake ipasavyo ikiwa ni pamoja na kutohudhuria mikutano ya Bunge, awajibishwe.

Vile vile, uwepo utaratibu wa wazi wa kupata Hansards za Bunge, ili iwe rahishi kwa mwananchi wa kawaida kuona yaliyofanyika na kusemwa Bungeni , ili wakati hawa wanaodharau wajibu wao wakija kutuomba tena kura, tuwe na ushahidi wa kuwaonesha kwa yale waliyoyasema au kuyafanya Bungeni.

Lazima kuwe na namna ya kucontrol hili tabaka jipya la wanyonyaji.
 
Wabunge wa upinzani ni wadhaifu...wameshindwa kumtoa Tulia kwa hoja wala kwa kutumia sheria sasa wanakimbilia kufunika midomo
 
Back
Top Bottom