Siku moja nimewahi mtembelea mzee wangu mstafu ambae kastafu mwaka jana katika taasisi fulani ya serikali.. Aliniambia neno moja Tz hakuna upinzani wengi wa viongozi na wabunge wa CHADEMA ni mamluki wa CCM wako katika kupoza kuwa Tz ionekane ina vyama vya upinzani.na akanieleza wazi wabunge wa CHADEMA ndio wako mstari wa mbele kuharibu mstabali wa upinzani Tanzania ili watu waone CHADEMA ni wafanya fujo ,wanahatarisha amani.
Kwa haya yanayofanywa na wabunge wa CHADEMA bungeni ukweli kabisa yananipa picha ya wazi kuwa hawa ni mamluki wako katika kuharibu CHADEMA kionekane chama cha wahuni wasiokuwa na maadili ya uongozi.. Ukiwatazama Wenje, Lisu, Mbilinyi, Lema etc kwa akili ndogo unaweza jua wanakijenga CHADEMA lakini ukitafakari kama kweli unaakili timamu na sio mshabiki wa kila kitu utagundua hawajengi chama bali ukwei wanakibomoa tena kwa kasi ya ajabu..CHADEMA sasa kinaonekani chama cha wahuni hakina uongozi imara wa kusimamia watumishi wake hasa hawa wabunge vijana.
Ukweli leo kila ukipita kijiwe story ni za Wenje jana na watuna wanaeleza wazi hiki chama mbona hakina watu wenye maadili wenye kueleza vitu vya maana kila siku vurugu tu bungeni ,matusi etc... Wako kama watoto wadogo wasiojua nini cha kusema na nini sicho cha kusema mbele za watu..
Mbowe ,Slaa hebu jaribuni kuwa makini chama kinapoteza sifa tena kwa kasi kubwa ..kumbukeni binadamu akibadilika kumrudisha katika imani ile ya kwanza ni ngumu sana..mfano mimi 2010 kura zangu zote zilikwenda CHADEMA lakini sasa imani inatoweka mana naona kama hiki chama wamejaa wahuni wanaharakati tu..